John Magongwe
Member
- Jan 4, 2024
- 71
- 119
Mbinguni ni Wapi
Mbinguni ni Wapi
Katika Biblia, neno mbingu linatumiwa kwa maana zaidi ya moja kumaanisha mbingu halisi; makao ya kiroho, na cheo kilichokwezwa au kutukuka. Katika kila maana, hali iliyopo inasaidia kutambua ni maana gani iliyokusudiwa.
1. Mbingu halisi: Kitabu cha Mwanzo 1:20 kinaelezea uumbaji wa ndege ‘wanaoruka juu ya dunia kwenye uso wa anga la mbingu.’ Katika kisa hiki, neno “mbingu” linarejelea angahewa, yaani anga linaloonekana. Isaya 13:10 inataja “nyota za mbinguni na makundi-nyota yake ya Kesili”, ikirejelea anga za juu. Katika maana hii, mbingu zinawakilisha anga, mahali ambapo upepo unavuma, ndege wanaruka, mawingu yanatokeza mvua na theluji, na umeme. (Zaburi 78:26; Methali 30:19; Isaya 55:10; Luka 17:24). Ni anga liizungukalo dunia (Mwanzo 1:17; Ku. 24:10). Inaweza pia kumaanisha anga za juu, mahali ambapo kuna jua na mwezi na nyota (Kumb Torati 4:19).
2. Makao ya kiroho: Neno mbingu pia linawakilisha mbingu za kiroho, au makao ya kiroho, eneo ambalo liko juu zaidi na nje ya ulimwengu halisi wa kimwili (1Wafalme 8:27; Yohana 6:38). Mbingu hizo za kiroho ni makao ya Mungu Yehova, ambaye ni Roho (Yohana 4:24). Ni mahali ambapo Mungu huishi na nyumbani kwa Watakatifu baadaye (Mwa 28:12; Zab. 11:4; Mt. 6:9). Biblia inazumgumzia ‘makao ya mbinguni’ ya Mungu na pia inasema kuna ‘malaika mbinguni.’ (1Wafalme 8:30; Mathayo 18:10). Ni makao ya malaika ambao ni viumbe wa roho walioumbwa na Mungu (Mathayo 24:36). Utaona kuwa hapa neno “mbinguni” halijatumiwa kwa njia ya mfano, lakini linafafanua makao halisi. Mbinguni ni wazi kabisa kuwa siyo peponi, ambapo ni mahali pa muda kwa ajili ya roho aminifu za wale wote walioishi na kufa katika dunia hii.
Biblia pia inatumia neno mbingu kurejelea hasa sehemu fulani ya makao ya kiroho ambapo Yehova mwenyewe anakaa, “makao yake”. (1Wafalme 8:43, 49; Waebrania 9:24) Kwa mfano, Biblia ilitabiri kwamba shetani na malaika waovu wangetupwa kutoka mbinguni, na hawangeruhusiwa tena kuingia mbele ya Yehova. Hata hivyo, bado wangeendelea kuwa katika makao ya kiroho (Ufunuo 12:7-9, 12).
3. Cheo kilichokwezwa au kutukuka: Maandiko yanatumia pia neno mbingu kuwakilisha cheo kilichokwezwa, hasa kuhusiana na mamlaka ya kutawala. Ifuatayo ni mifano ya mamlaka hayo:
Mungu Yehova mwenyewe akiwa Muweza Yote na Mwenye Enzi Kuu (2Mambo ya Nyakati 32:20-22; Luka 15:21).
Ufalme wa Mungu, serikali itakayochukua mahali pa utawala wa wanadamu. Biblia inautaja Ufalme huo kuwa “mbingu mpya” (Isaya 65:17; 66:22; 2Petro 3:13).
Serikali za wanadamu zilizojitukuza juu ya raia wao (Isaya 14:12-14; Danieli 4:20-22; 2Petro 3:7).
Roho waovu ambao kwa sasa wanatawala juu ya dunia (Waefeso 6:12; 1Yohana 5:19).
Je, Mbinguni Kukoje
Makao ya kiroho yana utendaji mwingi sana. Yana mamia ya mamilioni ya viumbe wa roho “wanaolitenda neno lake Yehova” (Zaburi 103:20-21; Danieli 7:10).
Biblia inafafanua kuwa, mbinguni ni mahali palipo na nuru nyingi sana (1Timotheo 6:15-16). Nabii Ezekieli alipokea maono ya kimbingu yaliyokuwa na “mwangaza” uliong’aa sana. Naye Danieli aliona maono ya mbinguni yaliyokuwa na “mto wa moto” (Ezekieli 1:26-28; Danieli 7:9-10). Mbinguni ni mahali patakatifu, au safi, na maridadi (Zaburi 96:6; Isaya 63:15; Ufunuo 4:2-3).
Mandhari inayofafanuliwa katika Biblia kuhusu mbinguni ni yenye kustaajabisha (Ezekieli 43:2-3). Hata hivyo, haiwezekani kwa wanadamu kuelewa jinsi mbinguni kulivyo kikamili, kwa kuwa hisia zetu hazina uwezo wa kuelewa kabisa makao ya kiroho yalivyo.
Mbinguni ni mahali patakatifu. Mbinguni ni mahali safi na maridadi kwa viwango visivyoweza kueleweka kwa uwezo wa kawaida. Ni muhimu tu, kusogea karibu kabisa na Mungu ili kuwa kwenye nafasi ya kuweza kuingia mbinguni. Unasogea karibu na Mungu kwa kushika neno lake na kulitekeleza kwa bidi bila kuchoka.
Mbinguni ni Wapi
Katika Biblia, neno mbingu linatumiwa kwa maana zaidi ya moja kumaanisha mbingu halisi; makao ya kiroho, na cheo kilichokwezwa au kutukuka. Katika kila maana, hali iliyopo inasaidia kutambua ni maana gani iliyokusudiwa.
1. Mbingu halisi: Kitabu cha Mwanzo 1:20 kinaelezea uumbaji wa ndege ‘wanaoruka juu ya dunia kwenye uso wa anga la mbingu.’ Katika kisa hiki, neno “mbingu” linarejelea angahewa, yaani anga linaloonekana. Isaya 13:10 inataja “nyota za mbinguni na makundi-nyota yake ya Kesili”, ikirejelea anga za juu. Katika maana hii, mbingu zinawakilisha anga, mahali ambapo upepo unavuma, ndege wanaruka, mawingu yanatokeza mvua na theluji, na umeme. (Zaburi 78:26; Methali 30:19; Isaya 55:10; Luka 17:24). Ni anga liizungukalo dunia (Mwanzo 1:17; Ku. 24:10). Inaweza pia kumaanisha anga za juu, mahali ambapo kuna jua na mwezi na nyota (Kumb Torati 4:19).
2. Makao ya kiroho: Neno mbingu pia linawakilisha mbingu za kiroho, au makao ya kiroho, eneo ambalo liko juu zaidi na nje ya ulimwengu halisi wa kimwili (1Wafalme 8:27; Yohana 6:38). Mbingu hizo za kiroho ni makao ya Mungu Yehova, ambaye ni Roho (Yohana 4:24). Ni mahali ambapo Mungu huishi na nyumbani kwa Watakatifu baadaye (Mwa 28:12; Zab. 11:4; Mt. 6:9). Biblia inazumgumzia ‘makao ya mbinguni’ ya Mungu na pia inasema kuna ‘malaika mbinguni.’ (1Wafalme 8:30; Mathayo 18:10). Ni makao ya malaika ambao ni viumbe wa roho walioumbwa na Mungu (Mathayo 24:36). Utaona kuwa hapa neno “mbinguni” halijatumiwa kwa njia ya mfano, lakini linafafanua makao halisi. Mbinguni ni wazi kabisa kuwa siyo peponi, ambapo ni mahali pa muda kwa ajili ya roho aminifu za wale wote walioishi na kufa katika dunia hii.
Biblia pia inatumia neno mbingu kurejelea hasa sehemu fulani ya makao ya kiroho ambapo Yehova mwenyewe anakaa, “makao yake”. (1Wafalme 8:43, 49; Waebrania 9:24) Kwa mfano, Biblia ilitabiri kwamba shetani na malaika waovu wangetupwa kutoka mbinguni, na hawangeruhusiwa tena kuingia mbele ya Yehova. Hata hivyo, bado wangeendelea kuwa katika makao ya kiroho (Ufunuo 12:7-9, 12).
3. Cheo kilichokwezwa au kutukuka: Maandiko yanatumia pia neno mbingu kuwakilisha cheo kilichokwezwa, hasa kuhusiana na mamlaka ya kutawala. Ifuatayo ni mifano ya mamlaka hayo:
Mungu Yehova mwenyewe akiwa Muweza Yote na Mwenye Enzi Kuu (2Mambo ya Nyakati 32:20-22; Luka 15:21).
Ufalme wa Mungu, serikali itakayochukua mahali pa utawala wa wanadamu. Biblia inautaja Ufalme huo kuwa “mbingu mpya” (Isaya 65:17; 66:22; 2Petro 3:13).
Serikali za wanadamu zilizojitukuza juu ya raia wao (Isaya 14:12-14; Danieli 4:20-22; 2Petro 3:7).
Roho waovu ambao kwa sasa wanatawala juu ya dunia (Waefeso 6:12; 1Yohana 5:19).
Je, Mbinguni Kukoje
Makao ya kiroho yana utendaji mwingi sana. Yana mamia ya mamilioni ya viumbe wa roho “wanaolitenda neno lake Yehova” (Zaburi 103:20-21; Danieli 7:10).
Biblia inafafanua kuwa, mbinguni ni mahali palipo na nuru nyingi sana (1Timotheo 6:15-16). Nabii Ezekieli alipokea maono ya kimbingu yaliyokuwa na “mwangaza” uliong’aa sana. Naye Danieli aliona maono ya mbinguni yaliyokuwa na “mto wa moto” (Ezekieli 1:26-28; Danieli 7:9-10). Mbinguni ni mahali patakatifu, au safi, na maridadi (Zaburi 96:6; Isaya 63:15; Ufunuo 4:2-3).
Mandhari inayofafanuliwa katika Biblia kuhusu mbinguni ni yenye kustaajabisha (Ezekieli 43:2-3). Hata hivyo, haiwezekani kwa wanadamu kuelewa jinsi mbinguni kulivyo kikamili, kwa kuwa hisia zetu hazina uwezo wa kuelewa kabisa makao ya kiroho yalivyo.
Mbinguni ni mahali patakatifu. Mbinguni ni mahali safi na maridadi kwa viwango visivyoweza kueleweka kwa uwezo wa kawaida. Ni muhimu tu, kusogea karibu kabisa na Mungu ili kuwa kwenye nafasi ya kuweza kuingia mbinguni. Unasogea karibu na Mungu kwa kushika neno lake na kulitekeleza kwa bidi bila kuchoka.