mbinu ya kupata gpa nzuri kwa chuo

mbinu ya kupata gpa nzuri kwa chuo

Ujanjawa ku apply ulichojifunza kwenye maisha mtaani ili ufanikiwe ndio kila kitu. GPA Mbwembwe tu.
 
wengine tuna ndoto ya kuja kuitwa PROF. so lazma tutake hzo GPA kubwa. thanks wale wote wanaotoa mawazo mazur..
 
We wacha kwanza upate chuo unaanza na G.P.A wakati hata haujachaguliwa chuo ukikosa je?unafanya mchezo na bodi ya mkopo na t.c.u ww?
 
Ndugu oil sumu huku mtaani maisha ni zaidi ya GPA na Point 3 za Advance!! Majita wangu kibao wamepiga GPA hadi 4.8 lakini majanga wana hela ya kula na dhamana ya kukopa kwa mangi tu!! Maisha ni kuumiza kichwa ili utoke we soma tu ili mladi umalize hata na kajontromen.
 
Last edited by a moderator:
Wasikukatishe tamaa jitahidi upate GPA nzuri at least hata 4.0 kwa scale ya 5.0 maximum. Ila usije ukawa na roho ya kumwaga damu kama Mr. Politician aka the first class economist in this country.
 
wakuu naomba ushauri ili nipate gpa nzur ktk masomo yangu ya chuo natarajia kuanza mwaka wa kwanza faculty ya b.a with education or (baed) asanteni

Kusoma na kupiga kwa makini assigment zinazounda course work zako
 
Wanafunzi wengi hawatilii mkazo course work. Hajiandai vizuri kwa vitest na assignment/lab work anawaachia wenzake wampigie kama ni group work au hatumii muda vizuri kufanya library work sawasawa. Matokeo yake unakuta hesabu ya course work inakuwa mbovu.

Kwenye UE anapiga kitabu sawia na anafaulu. Lakini akijumlisha na course work unakuta haendi kokote sana sana anaishia na makarai kama sio kula supu kabisa.

So ni vizuri kuweka mkazo kwenye course work usiachie watu wakufanyie kazi. Library kwa sana. Discussion etc kama walivyoshauri wadau.

Pata GPA nzuri. Ukitoka chuo ukagundua haina maana weka kwenye droo. Sio unapuuzia unaambulia pass then unakuja kugundua unaihitaji.
 
Jaribu kuupangilia muda wako vizuri, hasa ktk masomo
 
I would say..solve past papers kwa sana..walimu weng awana mda wa kutunga maswal..it's a good exam technique
 
Mdogo wangu hakuna fomula maalumu ya kupata GPA kubwa zaidi ya kutenda yaliyo mema, kutenda yaliyo mema kwako binafsi, kukitendea mema kitabu na kuwatendea mema waalimu na wanafunzi wenzako. Past papers kama walivyoshauri wadau ni muhimu pia ila si lazima uwe bundi! Ukipanga muda wako vizuri waweza pata GPA nzuri na unalala mapema kila siku na si kwa kuangalizia.
 
Back
Top Bottom