Mbinu za Kuidhoofisha CCM

Mbinu za Kuidhoofisha CCM

Third Eye

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2012
Posts
373
Reaction score
210
Habari za asubuhi wanajamvi.

Nimekuwa nikitafakari sana hali ya kisiasa nchini. Ni ukweli ulio wazi kuwa Chama tawala (CCM) ni chama kikubwa, chenye rasilimali watu na fedha pamoja na kufanya kazi kwa ukaribu na vyombo vya ulinzi na usalama, bila kusahau tentacles zake ziko kwenye kila eneo la serikali. Hizi ni facts, ni hali halisi kwa ground ambazo hatuwezi kupingana nazo au kujidanganya kuwa hazipo.

Kwa kutambua hilo, mbinu zozote za kupambana na CCM ni lazima zijumuishe ukweli huo. Ningependa kupata mawazo ya wadau, kama una mbinu yoyote inayozingatia hali halisi niliyoeleza tushauriane hapa. Mimi naanza na moja;

Kwa kuwa CCM ina watu kwenye vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na serikali, nashauri vyama vya upinzani navyo kuanza ku-recruit au kupandikiza watu huko. Mfano, kunapotokea kuna ajira za polisi/TRA/Uhamiaji nk...vyama vya upinzani vichukue jukumu la dhati kuhakikisha kuwa vijana wa chama, wenye imani na vyama hivi wanapata nafasi hizo. Kuanzia kwenye kuhimiza wajiunge mpaka ku-lobby pale inapowezekana ili navyo viwe na watu wao huko.

Je, wewe unashauri mbinu gani itumike kuidhoofisha CCM na/au kuimarisha vyama vya upinzani?
 
Ndio maana ni vema kukaa chini na kufanya mazungumzo na wananchi ambao hawakupata bahati ya kuingia shule rasmi au waliosoma na kupata elimu ya msingi.

Wengi wao hawa wanaishi na sio pretenders,angalia huyu middle class baada ta kupigwa na upepo mwanana wa AC anakuja na mada kama hii!!, nchi inahitaji KATIBA mpya sio viraka au mawazo mfu kama haya ya mtoa mada.
 
Habari za asubuhi wanajamvi.

Nimekuwa nikitafakari sana hali ya kisiasa nchini. Ni ukweli ulio wazi kuwa Chama tawala (CCM) ni chama kikubwa, chenye rasilimali watu na fedha pamoja na kufanya kazi kwa ukaribu na vyombo vya ulinzi na usalama...
Hakuna uwezo huo.

Kitu pekee kilichobaki Ni aidha:

1- CCM yenyewe ife.

Hili litatokea endapo kama CCM ikitenga makundi yote ya kijamii ambayo kwasasa inayakumbatia.

Makundi hayo Ni kama Viongozi wa dini, vyombo vya usalama na ulinzi, wasanii, vyama vya wafanyakazi, wanawake, vijana, wasomi, wahadhiri, machinga n.k.

2. Option ya pili, Ni kuhamasisha mass ( watu wote) wa-turn against serikali yao.

Na hili Ni kuandamana kwa zaidi ya miezi 6 mfululizo ili serikali ianguke.

Na hili Mara nyingi kwa nchi nyingi hutokana na aidha dini au makabila. Hili la dini hata kwa wapinzani Zanzibar limewasaidia sana.

Vinginevyo, hakuna namna yoyote utaitoa CCM hata siku moja.

Maana Kwanza vyama vyenyewe vinavyopambana na CCM havina userious wowote zaidi ya kufanya vyama vyao kuwa sehemu ya biashara, connection na ajira kwa makundi ya watu wachache.
 
Ndio maana ni vema kukaa chini na kufanya mazungumzo na wananchi ambao hawakupata bahati ya kuingia shule rasmi au waliosoma na kupata elimu ya msingi,wengi wao hawa wanaishi na sio pretenders...
Zanzibar walipata Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi tena inayojumuisha watu kutoka vyama vyote vya siasa.

Lakini mpaka leo hawajapata wanachokitaka pamoja na kuwa serious kuliko kawaida yenyewe.
 
Hakuna uwezo huo.

Kitu pekee kilichobaki Ni aidha:
...

Shukrani sana, just a follow up kwa option ya 1. Je inawezekana ku-accelerate huo utengano? mfano - kuongeza nyufa kati ya makundi ya kijamii na CCM?
 
Zanzibar walipata Katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi tena inayojumuisha watu kutoka vyama vyote vya siasa.

Lakini mpaka leo hawajapata wanachokitaka pamoja na kuwa serious kuliko kawaida yenyewe.
Nadhani hii ni changamot kubwa tuliyonayo, mtu anasema tu Katiba Mpya, hatutaki kufikiria njia mbadala. I hope tutapata michanganuo zaidi.
 
Ndio maana ni vema kukaa chini na kufanya mazungumzo na wananchi ambao hawakupata bahati ya kuingia shule rasmi au waliosoma na kupata elimu ya msingi.

Wengi wao hawa wanaishi na sio pretenders,angalia huyu middle class baada ta kupigwa na upepo mwanana wa AC anakuja na mada kama hii!!, nchi inahitaji KATIBA mpya sio viraka au mawazo mfu kama haya ya mtoa mada.

1. Ume- assume mimi ni middle class, tena nikifanya kazi kwenye AC - hii haina msaada wowote kwenye kupata katiba wala kwenye hoja iliyoko mezani.

2. Ushauri wako wa kuzungumza na wananchi ndio nilichofanya kupata maoni yao. Je ungependa mjadala kama huo ufanyike wapi?
 
Shukrani sana, just a follow up kwa option ya 1. Je inawezekana ku-accelerate huo utengano? mfano - kuongeza nyufa kati ya makundi ya kijamii na CCM?
Ni ngumu.

Labda CCM wakiacha kuwapa keki hapo ndio itakuwa rahisi.

Mfano sasa hivi, vyama vya upinzani vinaungwa mkono na kundi gani la kijamii?

Hakuna.
 
Habari za asubuhi wanajamvi.

Nimekuwa nikitafakari sana hali ya kisiasa nchini. Ni ukweli ulio wazi kuwa Chama tawala (CCM) ni chama kikubwa, chenye rasilimali watu na fedha pamoja na kufanya kazi kwa ukaribu na vyombo vya ulinzi na usalama, bila kusahau tentacles zake ziko kwenye kila eneo la serikali. Hizi ni facts, ni hali halisi kwa ground ambazo hatuwezi kupingana nazo au kujidanganya kuwa hazipo.

Kwa kutambua hilo, mbinu zozote za kupambana na CCM ni lazima zijumuishe ukweli huo. Ningependa kupata mawazo ya wadau, kama una mbinu yoyote inayozingatia hali halisi niliyoeleza tushauriane hapa. Mimi naanza na moja;

Kwa kuwa CCM ina watu kwenye vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na serikali, nashauri vyama vya upinzani navyo kuanza ku-recruit au kupandikiza watu huko. Mfano, kunapotokea kuna ajira za polisi/TRA/Uhamiaji nk...vyama vya upinzani vichukue jukumu la dhati kuhakikisha kuwa vijana wa chama, wenye imani na vyama hivi wanapata nafasi hizo. Kuanzia kwenye kuhimiza wajiunge mpaka ku-lobby pale inapowezekana ili navyo viwe na watu wao huko.

Je, wewe unashauri mbinu gani itumike kuidhoofisha CCM na/au kuimarisha vyama vya upinzani?
Labda wachukue wale wenye mafunzo ya jeshi wanarandaranda huko mtaani hawana kazi waunde jeshi lao(lakini sio hapa tz)sasa sijui wataliundia wapi.
Ila kwa usemacho hakiwezekani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM kuachia nchi ni pale asilimia kubwa ya wananchi watakapo jitambua vizuri kiakili (ELIMU), watu wengi wakielimika na kua na uwezo wa kuhoji na kuchukua hatua. Watu wakijua kipi serikali inapaswa kuwatendea kwenye huduma za afya, maji, umeme, haki hawa CCM watafukuzwa mapema sana kupitia sanduku la kura, elimu ni silaha pekee itakayo watoa hawa majizi. Ndio maana yana ajiri walimu failure na huduma ya elimu hayataki kuiboresha ipasavyo
 
Hiyo mbinu yako imefanyika sana sana 2015 kurudi nyuma kabla siasa haijawa vita.
Option zilizobaki zote ni ngumu kwa upinzani uliopo kutoboa ila ninachujua CCM itakufa tu haitaishi milele
 
Habari za asubuhi wanajamvi.

Nimekuwa nikitafakari sana hali ya kisiasa nchini. Ni ukweli ulio wazi kuwa Chama tawala (CCM) ni chama kikubwa, chenye rasilimali watu na fedha pamoja na kufanya kazi kwa ukaribu na vyombo vya ulinzi na usalama, bila kusahau tentacles zake ziko kwenye kila eneo la serikali. Hizi ni facts, ni hali halisi kwa ground ambazo hatuwezi kupingana nazo au kujidanganya kuwa hazipo.

Kwa kutambua hilo, mbinu zozote za kupambana na CCM ni lazima zijumuishe ukweli huo. Ningependa kupata mawazo ya wadau, kama una mbinu yoyote inayozingatia hali halisi niliyoeleza tushauriane hapa. Mimi naanza na moja;

Kwa kuwa CCM ina watu kwenye vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na serikali, nashauri vyama vya upinzani navyo kuanza ku-recruit au kupandikiza watu huko. Mfano, kunapotokea kuna ajira za polisi/TRA/Uhamiaji nk...vyama vya upinzani vichukue jukumu la dhati kuhakikisha kuwa vijana wa chama, wenye imani na vyama hivi wanapata nafasi hizo. Kuanzia kwenye kuhimiza wajiunge mpaka ku-lobby pale inapowezekana ili navyo viwe na watu wao huko.

Je, wewe unashauri mbinu gani itumike kuidhoofisha CCM na/au kuimarisha vyama vya upinzani?
acha kuzuga watu, dawa ya CCM ni katiba mpya - kingine ni kujichosha tu.
 
CCM kuachia nchi ni pale asilimia kubwa ya wananchi watakapo jitambua vizuri kiakili (ELIMU), watu wengi wakielimika na kua na uwezo wa kuhoji na kuchukua hatua. Watu wakijua kipi serikali inapaswa kuwatendea kwenye huduma za afya, maji, umeme, haki hawa CCM watafukuzwa mapema sana kupitia sanduku la kura, elimu ni silaha pekee itakayo watoa hawa majizi. Ndio maana yana ajiri walimu failure na huduma ya elimu hayataki kuiboresha ipasavyo
Shukrani sana kwa mchango wako. Umesema 1. elimu ndio suluhisho na 2. CCM inarudisha nyuma elimu kwa makusudi; Je tutumie mbinu gani kakabiliana na hili?
 
Kama walivyofanya ACT?

Post yangu inaomba michango ya nini kifanyike? ACT ni chama kimojawapo, wana haki ya kutumia mbinu wanayoona inawafaa. Vipi kwa vyama na wadau wengine, je wao watumie mbinu gani?
 
Hiyo mbinu yako imefanyika sana sana 2015 kurudi nyuma kabla siasa haijawa vita.
Option zilizobaki zote ni ngumu kwa upinzani uliopo kutoboa ila ninachujua CCM itakufa tu haitaishi milele
Nimetoa mfano tu wa mawazo yangu, je wewe unadhani tutumie mbinu gani? iwe ngumu au laini.
 
Back
Top Bottom