Mbinu za kutoboa Ozone enzi hizo tuko shule.

PGM tulikuwa na kiumbe mmoja tunamwita Braniac aka abatan anasoma mpaka inafkia kpindi anageuza daftari juu chini anasoma tena mnaalewa nikisema juu chini? Sijui ndo kuchanganyikiwa huko

Anatumia mikono yote miwili kuandikia
 
Msuli tembo majibu sisimizi Kuna mwamba tulikuwa dom moja anaweza kunyoosha saa 3 mpaka aaubuhi mpaka kumi na moja matokeo yalivyokuja aibu...wakati naingia mzumbe a level kuna wakati nilitamani kukimbia school maana nilikuwa najiona mweupe kumbe mbwembwe za pindi
 
Duh nilishawahi toboa siku mbili, kilichofuata baada ya hapo nililala siku 4. Nikaona haina maana nikawa napiga msuli mpk saa6 nalala
 
Wengine tulikua tunalala tunaamka saakumi ndo imetoka mpaka kuna kucha #johnkusoma
 
Ebwana eheee cjawai teseka ivo saa mbili ucingiz adi nimefika chuo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]kwenye Dushe ndipo kuna msala
 
Ha ha haaa! maisha haya bwana! Watu tumapitia misoto hatari.

Hiyo ya kuweka miguu kwenye beseni niliijaribu aisee mida ya saa10 11 alfajili hiyo ndo mida ambayo unahisi baridi lenyewe!
 
Nilipokuwa uboyizi mbinu pekee niliyokuwa natumia ni kunywa maji mengi Sana

Yaani utanikuta na chupa la Kilimanjaro Lile kubwa kila baada ya sekunde tano nabugia maji tu .

Usingizi haunipati kabisa

Coz naenda kukoja mfululizo

Najikuta tu paaap!! Asubuhi hii hapa
 
Usiku ni usiku tu asikwambie mtu nishabadilsha sana ratba lkn wap....nikaja kugundua muhimu ni kuutumia mchana vzr tu bhs masaa 12 ya kusoma kwa siku yanatosha sana kufanya maajabu muhimu isipite siku ujapiga msuli

Kuna jamaa alikuwa na vitanda viwli madom tofauti bhs jamaa akawa anabdlsha shift za vitanda watu tunajua jamaa anapiga misuli mizito
 
Mimi sikuwahi kujaribu,kunakipindi nilikuanikishtuka kwenda kukojoa najikuta dom nimopekeyangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…