Mbinu za siri za kuishi Tanzania bila kuteseka

Mbinu za siri za kuishi Tanzania bila kuteseka

Naongezea;
Usimsimange boss wako;
Usimshirikishe yoyote mambo yako ya siri Hasa kuhusu utafutaji na riziki.
Fanya ibada.
Usiishi uswahilini sana utarogwa.
Usitembee na mke wa mtu hata akikutaka ,wala usijenge mazoea nao.
Ishi kulingana na pato lako.
Usitegemee marafiki wa ki tz wakusaidie kwenye njaa.
Jenga utaratibu wa kufanya saving.
Kaa mbali na vitu kama mirathi,uwe wa mwisho kuongeza.
Ukienda ugenini usiwe na pupa ya marafiki wapya,somo game kwanza.
Machawa wasikilize ,ila usifanya maamuzi kwa maneno yao.
 
Kwahiyo wewe mjinga maisha ni kula kunywa na kulala

Wajinga Kama nyie ambao mnaamini maisha ni kujairiwa serikalini kula kuvaa na kupata pango sehemu ya kuegesha mbavu mnazingua Sana
Mkuu bado hujaleta hoja naona unaghadhaba, wewe maisha yanawexa yakawa magumu sanaa ila haimanishi kwamba ni magumu kwa kila mtu, ukweli ni kwamba Tanzania ni nchi nyepesi kuishi bila kutumia akili sanaa labda kama una kasoro zako personally
 
Mkuu mbona 60,000 ni mbonge la pesa mtu anapata 30,000 kwa mwezi ila nakitambi anacho maisha hapa Tanzania ni mepesi sanaaa angalia idadi ya wa piga debe pale mbezi magufuli wote wanapata Rizki ya kutosha.


Inawezekana una exposer ndogo au kwa makusudi umeamua kufurahisha genge

Kama kula ilimradi umekula upo sahihi

Ila watanzania aslimia kubwa wanasukuma siku na sio kuishi

Huwa nashangaa sana mtu akisema Tanzania ina nafuu ya maisha itakuwa anafikiria maisha ni kula chochote , kulala popote na kuvaa chochote ila sio standard life.

Tanzania ili uwe na standard life is not easy hasa ukiwa unafanya shughuli halali.

Maneno kama yako huwa wanayaongea waajiriwa ambao wanatafutiwa ugali na mwajiri wao na sio kwa watu ambao wapo field wanapambana na maisha .
 
Wadau wa JF, heshima mbele!

Tunapita mitaani, tunaona nyuso zenye tabasamu, lakini mioyo mizito kama kokoto. Tanzania ni uwanja wa mapambano, na kila mtu ana njia yake ya kujikwamua. Wapo wanaotembea kwenye kamba nyembamba ya maisha, huku chini kukiwa na shimo refu la shida. Wapo wanaosafiri bila ramani, wakitegemea upepo uwape mwelekeo. Lakini kuna mbinu za siri, ambazo wachache wanazitumia kuishi bila kuteseka. Leo, nazifunua moja baada ya nyingine.

Kuwa Kivuli Badala ya Jua

Jua linapowaka, linachoma. Lakini kivuli hakina presha, hakina kazi kubwa, lakini kinahitajika kila siku. Katika maisha, usijitokeze sana kama jua, maana utakuwa na maadui wengi. Fanya mambo yako kimyakimya, acha matokeo yaongee.

Jenga Kisima Chako Kabla ya Kiangazi

Watu wengi hukimbilia kutafuta maji wakati kiangazi kimefika, lakini wenye busara walichimba visima vyao zamani. Usisubiri matatizo yajitokeze ndipo uanze kutafuta suluhisho. Jifunze kuweka akiba, tengeneza vyanzo vingi vya kipato, na usiishi kwa kutegemea mshahara pekee.

Usiwe Kuku Anayewika Asubuhi Kabla ya Muda

Kuna watu hujipa sifa kabla hata hawajafanikisha jambo. Ukiwa mtu wa makelele na kutangaza mipango yako kwa kila mtu, usishangae ukiona haitimii. Dunia inasikia na si kila anayekusikiliza anakuombea mema. Fanya kazi kimya, mafanikio yatangaze kazi yako.

Kuwa Kama Nyoka: Badili Ngozi Ukiwa na Wakati Mzuri

Nyoka hubadilisha ngozi yake kabla haijamchosha. Katika maisha, usisubiri hali iwe mbaya ndipo uanze kubadilika. Kama kazi haikulipi, tafuta mbadala mapema. Kama biashara inakufa, anzisha nyingine kabla ya kufilisika. Mabadiliko yanapaswa kuwa sehemu ya mpango wa maisha.

Tembea na Watu Wanaokupa Mwanga, Sio Kivuli

Katika safari ya maisha, ukitembea na vipofu, usishangae ukijikuta kwenye shimo. Rafiki zako wana mchango mkubwa katika maisha yako. Weka watu wanaokutia moyo, wanaokufundisha na kukusukuma mbele. Epuka wale wanaotumia muda mwingi kulalamika na kulaumu wengine.

Kuwa Na Macho ya Tai, Lakini Usiruke Kama Kuku

Tai huona mbali, kuku huona chakula tu kilicho karibu. Watu wanaoteseka ni wale wanaofikiria kesho tu, badala ya miaka 10 ijayo. Tafuta njia za kujijenga kwa muda mrefu. Usitumie pesa yote leo, fanya mipango ya kesho na kesho kutwa.

Kwa Ufupi, Hizi Ndizo Siri za Kuishi Bila Kuteseka Tanzania:
  • Fanya mambo yako kimya kimya, acha matokeo yaongee
  • Jipange kabla ya matatizo, weka akiba na vyanzo vya kipato
  • Epuka kutangaza mipango yako kabla haijakamilika
  • Usiogope mabadiliko, yatumie kwa manufaa yako
  • Chagua marafiki wanaokupa mwangaza, sio wanaokurudisha nyuma
  • Fikiria maisha ya miaka 10 ijayo, sio kesho tu

Wadau, Tanzania si mahali pa kuishi kwa mazoea. Yeyote anayeishi bila mpango, atateseka. Kuwa mwerevu, pambana kwa akili!

Karibuni kwenye mjadala, unadhani ni mbinu ipi inawafaa wengi zaidi?
Ukizaliwa Afrika automaticaly tayari maisha yashakupiga goli 1-0, kama hauna connection 2-0, ukioa 3-0. Hapo upige comeback shughuli yake sio ya kitoto
 
Inawezekana una exposer ndogo au kwa makusudi umeamua kufurahisha genge

Kama kula ilimradi umekula upo sahihi

Ila watanzania aslimia kubwa wanasukuma siku na sio kuishi

Huwa nashangaa sana mtu akisema Tanzania ina nafuu ya maisha itakuwa anafikiria maisha ni kula chochote , kulala popote na kuvaa chochote ila sio standard life.

Tanzania ili uwe na standard life is not easy hasa ukiwa unafanya shughuli halali.

Maneno kama yako huwa wanayaongea waajiriwa ambao wanatafutiwa ugali na mwajiri wao na sio kwa watu ambao wapo field wanapambana na maisha .
Mkuu wewe unategeme mpiga debe au muendesha bajaj ajenge ghorofa kwanza ndo yawe maisha mazuri? Neenda South Sudan robo ya raia wanalala nje hawana shelter wana kula mara moja neenda Ethiopia ujionee hata kupata kazi ya mpiga debe haipo.
 
Ukizaliwa Afrika automaticaly tayari maisha yashakupiga goli 1-0, kama hauna connection 2-0, ukioa 3-0. Hapo upige comeback shughuli yake sio ya kitoto
Ni kweli mkuu! Mfano mzuri ni mtu anayekulia kijijini bila connection , anaanza maisha akiwa tayari nyuma. Akimaliza shule hana ajira kwa sababu kazi nyingi zinapatikana kwa "mtu wangu yupo." Akioa mapema bila kuwa na msingi imara kifedha, majukumu yanaongezeka maradufu. Hapo comeback yake inahitaji akili, juhudi, na uvumilivu wa hali ya juu!
 
Aah kwani ungenena bila mafumbo tusingeelewa mkuu?
Kuna faida ya kutumia mafumbo. Moja ya faida ni kwamba concept inaeleweka kwa kina zaidi kuliko kusema moja kwa moja. Mafumbo yanachochea fikra, yanahimiza tafakuri na yanasaidia ujumbe kupenya kwa namna ya kipekee zaidi. Wanaojua, wataelewa haraka; wanaotaka kujua, watatafuta maana na hapo ndipo ujumbe unakaa kwenye akili zao kwa muda mrefu.
 
Inawezekana una exposer ndogo au kwa makusudi umeamua kufurahisha genge

Kama kula ilimradi umekula upo sahihi

Ila watanzania aslimia kubwa wanasukuma siku na sio kuishi

Huwa nashangaa sana mtu akisema Tanzania ina nafuu ya maisha itakuwa anafikiria maisha ni kula chochote , kulala popote na kuvaa chochote ila sio standard life.

Tanzania ili uwe na standard life is not easy hasa ukiwa unafanya shughuli halali.

Maneno kama yako huwa wanayaongea waajiriwa ambao wanatafutiwa ugali na mwajiri wao na sio kwa watu ambao wapo field wanapambana na maisha .
Tanzania na uenda Afrika kwa ujumla tumeshakua addicted na maisha ya shida kiasi kwamba tunaona huo ndio ustaarabu wa maisha ya binadamu.

Kwetu ufukara tumeutengenezea picha kama taswira ya uadilifu, uzalendo na hadhi nzuri. Haishangazi hata JPM alipata mashabiki wengi sana kwa kujiita Rais wa wanyonge.
 
Ni kweli mkuu! Mfano mzuri ni mtu anayekulia kijijini bila connection , anaanza maisha akiwa tayari nyuma. Akimaliza shule hana ajira kwa sababu kazi nyingi zinapatikana kwa "mtu wangu yupo." Akioa mapema bila kuwa na msingi imara kifedha, majukumu yanaongezeka maradufu. Hapo comeback yake inahitaji akili, juhudi, na uvumilivu wa hali ya juu!
Na iyo comeback inaweza iaifanyike kabisa. Matokeo yakabaki ivyo ivyo au maisha yakakupiga chuma cha 4
 
Ukishindwa kuishi Tanzania kwa neema zake naupesi wa maisha usijaribu kuenda Kenya Zibabwe Ethiopia na nchi nyingi kabisa, ukweli ni kwamba Tanzania unaweza ukaishi popote bila kutumia nguvu nyingi kabisa.........
Huko Kenya kuna matajiri, na watu wana kula bata si za kitoto..

Acha woga wako ndio umaskini wako.
 
Tanzania na uenda Afrika kwa ujumla tumeshakua addicted na maisha ya shida kiasi kwamba tunaona huo ndio ustaarabu wa maisha ya binadamu.

Kwetu ufukara tumeutengenezea picha kama taswira ya uadilifu, uzalendo na hadhi nzuri. Haishangazi hata JPM alipata mashabiki wengi sana kwa kujiita Rais wa wanyonge.
Na kila tajiri akamwita ni mpiga madili akaanza kumshughulikia. Akapoteza lengo la kuwaletea wananchi maisha bora akaishia na udikiteta tu
 
Tanzania na uenda Afrika kwa ujumla tumeshakua addicted na maisha ya shida kiasi kwamba tunaona huo ndio ustaarabu wa maisha ya binadamu.

Kwetu ufukara tumeutengenezea picha kama taswira ya uadilifu, uzalendo na hadhi nzuri. Haishangazi hata JPM alipata mashabiki wengi sana kwa kujiita Rais wa wanyonge.
,👊🏼
 
Na iyo comeback inaweza iaifanyike kabisa. Matokeo yakabaki ivyo ivyo au maisha yakakupiga chuma cha 4
Hapo ndo changamoto kubwa! Unaweza pigana comeback kwa nguvu zote, lakn kama mazingira hayabadiliki au mfumo unakukandamiza, unaweza jikuta matokeo yanabaki vile vile bora liende. Mbaya zaidi, ukijikwaa vibaya, maisha yanakupiga goli la 4, unakuwa officially umetoka kwenye game. Ndy maana comeback inahitaji siyo tu juhud, bali pia mbinu sahihi, bahati kidg, na connection za maana!
 
Mkuu sijaelewa hoja yako hapa unacho maanisha ni nini hasa, kwamba Tanzania ni ngumu sanaa kuishi au?
Baadhi ya maeneo ni ngumu sana kuishi, kwa mfano nenda Musoma mara ule mji mzunguko wake wa pesa unaendeshwa na upatikanaji wa samaki na dagaa, kipindi Cha Giza pesa ipo na inapatikana na wepesi ila kipindi Cha mbaramwezi mambo yanakuwa magumu sio kwa wauza nguo au wauza vyakula, Mimi nimeishi sehemu nyingi sana Tanzania hii
 
Mkuu sio kweli Tanzania ni nchi nyepesi kuishi hata kuliko Ulaya nchi kama Greece Portugal Spain Hungary, hata Kenya tu ni ngumu kuishi kama huna chanzio, ni Tanzania peke mtu anakula kila siku na kushiba ila hana kazi, ni Tanzania peke mtu mpaka anaota kitambi ila hana mshahara au shungli maalumu, thubutu Kenya ujionee mkuu.
Kenya ni nyoko kule amna mamb yakuombana chumvi/unga kule ndo ubepari Sasa.
 
Back
Top Bottom