Mboga gani unaweza otesha nyumbani ili kukabiliana na mfumuko wa bei na ugumu wa maisha?

Mboga gani unaweza otesha nyumbani ili kukabiliana na mfumuko wa bei na ugumu wa maisha?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Infaltion inafanya maisha yanakuwa magumu sana. Athari kubwa zinakuwa upande wa lishe. Si vema kupata utapiamlo na hali unaweza solve kwa kuotesha mbogamboga hapo nyumbani. Tushirikishane juu ya mbogamboga na vyakula vingine ambavyo mtu anaweza kuzalisha nyumbani.

1. Kisamvu. Hapa nazungumzia ile miti ya kisamvu ambayo huwa mikubwa sana na haitois mihogo. Badala ya kupanda miti ya mapambo basi panda huu mti. Ukipata maji unatoa mboga mwaka mzima.
1675791173900.jpeg


2. Badala ya kupanda maua panda nyanya chungu. Hizi zinazaa mwaka mzima. Pia matunda na majani yake vyote ni mboga nzuri, so unavyosubiria matunda unakuwa unapata mboga za majani.
mqdefault.jpg

solanum%20aethiopicum.jpg


3. Otesha hoho. Pilipili hoho ukitunza vizuri zinazaa kwa muda mrefu sana.
pilipili-hoho-2.jpg

Pilipili-hoho-zimekomaa.jpg


4. Panda matembele. Matembele huwa yanadumu sana. Umwagilie tu.
59f557e110d30c47be3349d119e9007f.jpg

5. Hata nyanya unaweza panda na kuepuka. Itakusaidia pia kuepuka zenye madawa.
Domestication%20of%20the%20tomato%20was%20long%20believed%20to%20have%20happened%20from%20plants%20with%20cherry-sized%20fruits%2C%20but%20recent%20genetic%20research%20indicates%20otherwise..png

cherry-tomato.jpg

Cherry-Tomatoes-Growing-in-the-Garden.jpg

Mazao hawa unazalisha hata kwenye makopo. Si mpaka uwe na eneo kuuubwa.

6. Chakula gani kingine mtu anaweza kuzalisha nyumbani?
 
Sukuma wiki
Mchunga
Mlenda Pori
Pilipili za mwendokasi
Pilipili kichaa

Ongezea hapo
 
Mboga zote labda kasoro nyama na dagaa kamaa eneo n dogo sana otherwise mboga zote.
Mboga nyingi huwezi kuotesha kwa ufanisi. Kwanza inatakiwa iwe ya kudumu muda mrefu, si ya kuotesha miezi kadhaa halafu unang'oa kama mchicha na karoti. Pia inatakiwa iwezekane kuchuma kila baada ya muda kidogo au kila siku. Mfano Matembele au kisamvu unaweza kuchuma kila siku. Siku au baada ya siku chache tu.
 
Au ile mitungi ya sementi ya kupandia maua. Au hata vyungu vya maua.
Waweza kutumia madumu ya mafuta ya kula ya 20lts. Unakata ubavuni unatoboa matundu ubavu mwingine utakao kaa chini ili maji yapite yasituame kisha unaweka udongo na samadi.
Unaweza kutumia makopo ya maji ya 12ltr au ya water dispenser unakata nusu unatoboa matundu chini.
Unaweza kutumia mifuko ya cement au viroba vigumu, mifuko ya nylon migumu.
Unaweza kutumia makopo ya maji ya 1ltr au 1.5lt unayakata juu na chini au unakata nusu unatoboa chini matundu madogo unapanda maboga au kunde.
 
Back
Top Bottom