Mbona Takukuru wanakamata wagombea ubunge wa CCM pekee ina maana Chadema hakuna rushwa?

Mbona Takukuru wanakamata wagombea ubunge wa CCM pekee ina maana Chadema hakuna rushwa?

Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!
Ndiko rushwa ilipoanzia na ndipo ilipo tangu uhuru, CDM safiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!
 
CCM sehemu kubwa wanachomana wao kwa wao kutokana na ushindani.

Pia Chadema bado wapo wachache nikimaanisha wengi ni Washangiliaji lakini unakuta mwenye nguvu ni mmoja na huyo huyo ndio atang'ang'ania kila uchaguzi akae yeye, mfano Lema, Sugu, Msigwa,Mdee n.k.
 
Ngoja tuone mwisho utakuwaje maana ccm wamekuea kama Mbwa. Wameiba Tl 1.5 yaani mpaka hasira.
 
Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!


Unashindwa kuelewa,Jiwe anataka kuondoa kada yote yenye akili kumzidi...

Hii ipo wazi

Wala huna haja ya kutumia akili kubwa..

Wanaoshikwa wote ni wale walio kwenye vibe tofauti na lake tu!
 
CCM ni Rushwa na Rushwa ni CCM.

Udugu wa CCM na rushwa ni zaidi ya udugu wa kurwa na doto.

Hivyo ni vigumu sana kutenganisha CCM na rushwa.
 
Huku Serukamba, kule Lusinde. Ukienda Manyovu Takukuru wana MTU washakula naye sahani moja.
Shinyanga watu wamekamatwa wakigawa kanga kufukuzia ubunge.
Yaani tuhuma nchi nzima, watu wa CCM wameshaanza kupikiwa ubwabwa ili wachague walio nunua huo ubwabwa.
Hii inaonyesha picha gani kuhusu CCM? Kwamba bila rushwa mambo yao hayaendi? Au na zile atowazo Rais Magufuli barabarani nazo ni rushwa? Jee na zile makanisani sijui kufadhili kwaya, kumalizia ujenzi nk hivi nazo sio Rushwa?
Hiki chama kingefungiwa walao kwa miaka miwili tuu kingerudi kuwa chama cha siasa tofauti na sasa kimekuwa genge la wahuni na matapeli watupu.
Msidanganyike, hii ni danganya toto ionekane CCM "wameshughulikiwa" kumbe hamna lolote.
 
Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!
Siku TAKUKURU wakimkamata Kamanda kwa rushwa hakika nchi itasimama waonekane wamefanya kazi nzuri,hata wao wanatamani ingekuwa hivyo maana wangepandishwa vyeo the same day.CDM kwa bahati waliyonayo,wanao wanachama safi,wasiojihusisha na rushwa kwa sababu wanauwezo wa kushawishi kura kwa sera ni watu wanaojitambua.
CCM kwa upande wao,siyo rahisi kupata uongozi bila kutoa rushwa,wengi wanakosa ushawishi.Wanajisifia miradi ya maendeleo iliyojengwa kwa kodi za Watanzania,kila siku kupiga picha kwa makundi yao waonekane wanawajali wananchi.Chama kikishachaguliwa ilani yake inakabidhiwa na kutekelezwa na serikali,kwa bajeti ya taifa na hivyo siyo sifa wala mali ya chama husika.Utekelezaji wa miradi na huduma za kijamii kama elimu,afya,maji,miundo mbinu inayojengwa sehemu mbali mbali siyo hisani bali wajibu wa serikali kwa kuwa ndiyo inayokusanya kodi zetu.
Tunahitaji Tume Huru na Jumuishi ya Uchaguzi kwa manufaa ya Watanzania ambayo itaandaa,kuendesha uchaguzi,kutenda haki kwa wote wanaohusika na zoezi la uchaguzi na kutoa matokeo halali ya kile walichoamua wananchi kupitia sanduku la kura.Hiyo ni haki yetu kama wananchi,kwa nini watawala hawataki Tume Huru.KUNANI?Mbona kuna kauli ya maendeleo hayana vyama?Acheni wananchi waongee kupitia sanduku la kura.Tekelezeni kauli ya maendeleo hayana vyama kwa vitendo na siyo maneno ya jukwaani.
 
Huku Serukamba, kule Lusinde. Ukienda Manyovu Takukuru wana MTU washakula naye sahani moja.
Shinyanga watu wamekamatwa wakigawa kanga kufukuzia ubunge.
Yaani tuhuma nchi nzima, watu wa CCM wameshaanza kupikiwa ubwabwa ili wachague walio nunua huo ubwabwa.
Hii inaonyesha picha gani kuhusu CCM? Kwamba bila rushwa mambo yao hayaendi? Au na zile atowazo Rais Magufuli barabarani nazo ni rushwa? Jee na zile makanisani sijui kufadhili kwaya, kumalizia ujenzi nk hivi nazo sio Rushwa?
Hiki chama kingefungiwa walao kwa miaka miwili tuu kingerudi kuwa chama cha siasa tofauti na sasa kimekuwa genge la wahuni na matapeli watupu.
Mzizi wa yote ni rushwa inayotolewa kwa wawakilishi wetu pale mjengoni,mishahara na marupurupu ya kutosha,halafu unamalizia miaka mitano na gratitude ya over 200 millions Tshs in cash instantly on last day of the fifth year.Ndiyo maana wapo tayari kwa lolote na kwa njia hata zile zisizo halali kuupata ubunge,watu wanaachia ofisi za umma zinazohitaji visomo vyao na kwenda kusema ndiyooo huku wakiishi kifalme,wanajipangia mishahara na posho nono na kusahau vipaumbele vya Watanzania.
Tunahitaji mabadiliko,tuseme inatosha kwa ukosefu wa umoja,mshikamano,usalama,uhuru wa maoni na kutofautiana kwa hoja bila kugombana.Sisi sote,bila kujali itikadi zetu ndiyo Watanzania,tunajenga nyumba moja,ya nini tugombee fito?Kila mmoja wetu ni potential,msijimilikishe ujenzi wa Taifa.Uongozi siyo Utawala bali Utumishi wa Wito.Hakuna aliye bora kuliko mwingine,usawa wa binadamu na haki za binadamu ni msingi wa UTU.
 
CCM imejengwa kwa misingi imara ya rushwa na hakuna wa kuweza kuitenganisha CCM na rushwa
 
Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!

Ni mtego huo, takukuru hawawezi kamata bossi zao ccm
 
Kigezo kitakachotumika kuwakata wagombea ni rushwa!tuhuma tu zinatosha!!Ndio mpango kazi wa jpm kuwaengua wagombea na kuwaweka wapya wa mfukoni!!

Nilisema jambo hili siku tatu zilizopita. TAKURURU inatumika kisiasa na ndio itakuwa chanzo cha kukata!! Jiulize anakamatwa Dodoma badala ya jimboni kwake Kigoma?? Huu ni mpango mahususi uliopangwa toka jimboni kwake na hao hao TAKURURU.
 
Mzizi wa yote ni rushwa inayotolewa kwa wawakilishi wetu pale mjengoni,mishahara na marupurupu ya kutosha,halafu unamalizia miaka mitano na gratitude ya over 200 millions Tshs in cash instantly on last day of the fifth year.Ndiyo maana wapo tayari kwa lolote na kwa njia hata zile zisizo halali kuupata ubunge,watu wanaachia ofisi za umma zinazohitaji visomo vyao na kwenda kusema ndiyooo huku wakiishi kifalme,wanajipangia mishahara na posho nono na kusahau vipaumbele vya Watanzania.
Tunahitaji mabadiliko,tuseme inatosha kwa ukosefu wa umoja,mshikamano,usalama,uhuru wa maoni na kutofautiana kwa hoja bila kugombana.Sisi sote,bila kujali itikadi zetu ndiyo Watanzania,tunajenga nyumba moja,ya nini tugombee fito?Kila mmoja wetu ni potential,msijimilikishe ujenzi wa Taifa.Uongozi siyo Utawala bali Utumishi wa Wito.Hakuna aliye bora kuliko mwingine,usawa wa binadamu na haki za binadamu ni msingi wa UTU.

Ubunge ndio biashara inayolipa kuliko zote hata ukisinzia bungeni pesa inaingia
 
CHADEMA wanatakiwa kuzidisha mara dufu umakini ktk kampeni zao za uchaguzi huu,Hii kamatakamata ya watia nia wa CCM si dalili nzuri wala si jambo la kufurahia hata kidogo kwa upande wao.

Muda huu wanajishughulikia wenyewe kwa wenyewe{kuwazuga},muda wa kampeni utakapofika watahamia kwenu na ndo itakuwa bye bye.{wamepita bila mpinzani wa kweli}
 
Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!
Usanii
 
Waseme tu wanaunga juhudi za kugawa zile trillion2, 4. wataachiwa na kupitishwa.
CCM Oyeeee..! Magufuli Oyeeee...!
 
Huko ndio rushwa ilizaliwa, kubatizwa, kulelewa na kukulia! kumbuka waliwahi kuibatiza na kuipa jina nzuri la 'takrima' 🤣
 
Najiuliza tu.

Maana kwanza alikamatwa Dr Kigwangalla akigawa baiskeli lakini akajitetea na kutoa vifungu vya sheria vinavyomlinda.

Kisha akakamatwa Kibajaji bado sijajua imeishaje lakini leo kakamatwa Serukamba.
Ndiposa najiuliza hiyo rushwa inatolewa huko chama tawala pekee?

Au CHADEMA bado wako kwenye uchumi mdogo?

Maendeleo hayana vyama!
Kwani akimatwa A ni lazima pia akamatwe B hadi Z au wanakata pale wanapohisi kuna uhalifu umefanyika na kwamba kuwakamata hao siyo kwamba ndiyo mwisho wa kazi yao?
 
Back
Top Bottom