Mbosso hapendwi lakini nyimbo zake ndo tunalala nazo

Huyu mwana dada namkubar zahara anasaut
 
Hakuna kama mbosso kwa kweli!mbosso anajua,ana manjonjo kwenye uimbaji!Nadekezwa na Picha yake ni ngoma kaali sana.
 
Umeenda vizuri mpaka pale uliposema Nadekezwa pia bomu, nikaacha kusoma.
 
Lavalava na mbosso wanachokiimba hata siwaelewi..
Mimi naona labda wajaribu ma collabo labda yatawatoa.

Lkn kwa style hii ya kuimba kaswida bado hawajanipata kuzikubali ngoma zao
Binadamu ni viumbe vya Ajabu sana, Nyimbo anazoimba diamond siku izi mnasema amebaki kuimba matusi ,, Na nyimbo zina hit, sasa hawa kina mboso, lavalava wakiimba nyimbo mnazo zitaka mnasema hawajui kuimba sasa nyie mnachotaka ni nini????
 
Binadamu ni viumbe vya Ajabu sana, Nyimbo anazoimba diamond siku izi mnasema amebaki kuimba matusi ,, Na nyimbo zina hit, sasa hawa kina mboso, lavalava wakiimba nyimbo mnazo zitaka mnasema hawajui kuimba sasa nyie mnachotaka ni nini????
Mkuu wewe unaona mbosso na diamond wanaimba style sawa??
Mbosso anaimba kwaya sio kwaya taarabu sio taarabu nachi sio nachi yaani kifupi haeleweki
 
Watu wanatatizo na mahadhi ya nyimbo anazoimba Mboso lakini naamini wanakubali kipaji chake. Haiwezekani WCB wote wakaimba nyimbo zenye mahadhi yaleyale...Chibu na Konde Boy wamejipambanua kwa kuimba nyimbo zenye kuchezeka zaidi kutokana na beats zake. Mboso na Lavalava wanaimba mahadhi ya taratibu na ujumbe wake unafika polepole....tumuunge mkono kijana kaamua kuacha ukabaji atafute ridhiki halali
 
Huyu Mboso tatizo hana style nyimbo zake zote zinafanana....ukisikiliza kuanzia watakubali mpaka hii mpya unaweza kudhani ni muendelezo wa nyimbo moja kuanzia Sauti,style mpaka uandishi
 
Huyu Mboso tatizo hana style nyimbo zake zote zinafanana....ukisikiliza kuanzia watakubali mpaka hii mpya unaweza kudhani ni muendelezo wa nyimbo moja kuanzia Sauti,style mpaka uandishi
Kama Aslay na beka fleva wote hawabadiliki.
 
Mbosso nampenda,

Lavalava ana kipaji,sana tu,ingawa mtunzi wa nyimbo zake haeleweki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…