Mbowe anakosa sifa muhimu ya kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA. Ajiuzulu nafasi yake kwa maslahi ya chama na Taifa kwa ujumla

Mbowe anakosa sifa muhimu ya kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA. Ajiuzulu nafasi yake kwa maslahi ya chama na Taifa kwa ujumla

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Uadilifu ni sifa kuu na ya msingi anayopaswa kuwa nayo kiongozi yeyote yule wa Taasisi ya uma.

Chadema kama chama kingine cha siasa ni Taasisi ya uma kwa kuwa imesajiliwa kwa kufuata sheria za nchi zinazoongoza vyama vya siasa hapa nchini kwa maana hiyo haikwepi kuwa na vigezo muhimu vya taasisi yeyote ya uma ikiwa na kigezo nilichokitaja awali cha uadilifu wa viongozi wake.

Jana siku ya tarehe 4/03/2022 DPP Kupitia kifungu cha 91 Cha Sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai aliamua kufuta mashitaka ya Ugaidi dhidi ya Mwenyekiti wa Chadema na wenzake watatu.

Kwa kupitia kifungu hicho tafsiri yake ni kwamba pale ambapo itaonekana inafaa DPP anaweza yarejesha mashitaka hayo.

Hiyo inamaana kwamba kesi iliondolewa mahakamani bila ya Mbowe kutoa utetezi wake mahakamani na hatimaye mahakama kutoa maamuzi kuhusiana na tuhuma hizo.

Kwakua hakuna hukumu yeyote ile ya mahakama iliyosema kwamba Mbowe hajafanya alichotuhumiwa nacho au kakifanya na kwakua bado. DPP anaweza kurejesha tena kesi mahakamani basi kiufundi tunasema kwamba tuhuma dhidi ya Mbowe zinabakia pale pale.

Kwakua tuhuma bado zipo kwakua hakuna rekodi ya mahakama inayomsafisha Mbowe na tuhuma dhidi yake basi kwa manufaa mapana ya Chadema na Taifa kwa ujumla inampasa Mbowe kujiuzulu nafasi yake ya Uwenyekiti na kukaa mbali na siasa za kiushindani.

Inampasa Mbowe kujiuzulu kwani anakosa sifa muhimu ya uadilifu kwani tuhuma dhidi yake ni kubwa na hatarishi kwa ustawi wa Taifa lolote na haitakuwa afya kwa chama kuongozwa na kiongozi ambaye anaishi na tuhuma hizo.

The good things could have been to let Mbowe testify and the court to rule as to whether Mbowe is guilty or not but so far as we speak the allegations have not been cleared against him thus he must resign.
 
The good things could have been to let Mbowe testify and the court to rule as to whether Mbowe is guilty or not but so far as we speak the allegations have not been cleared against him thus he must resign.
Kwa hiyo unamlaumu Mbowe kwa vile hakutoa utetezi wake?

Mkuu 'Stroke', wakati mwingine kujitoa ufahamu na kupoteza muda kwa kuandika andiko lote hili uliloweka hapa ni aibu kwa mtu kama wewe..

Ni kipi kinachokupa msukumo wa chuki kiasi hiki!

Unaandika kuhusu "uadilifu", hivi unafahamu maana ya neno hili? Tukirejea katika maandishi yako ya utetezi wa viongozi uliyoyaweka humu JF, tutapata tafsiri nzuri ya "uadilifu" unaotaka Mbowe auonyeshe?

Nimekuwa nikifuatilia misimamo yako kadhaa juu ya taifa letu na kukubaliana nawe, hasa kwenye siku hizi za karibuni. Lakini maandishi ya aina hii uliyoweka hapa yanaonyesha kuna kasoro hata kwenye yale ninayodhani unayaaamini juu ya nchi yetu. Nadhani kuna chuki ndani yake.
 
Kwa hiyo unamlaumu Mbowe kwa vile hakutoa utetezi wake?

Mkuu 'Stroke', wakati mwingine kujitoa ufahamu na kupoteza muda kwa kuandika andiko lote hili uliloweka hapa ni aibu kwa mtu kama wewe....
Tuhuma ya Ugaidi bado inabakia pale pale.

Hakuna mahakama iliyomsafisha mbowe.

Unaweza usinielewe sasa ila kwa baadae utakuja kunielewa kwamba.

Rekodi za mahakama zinatambua kwamba mbowe alikutwa na kesi ya kujibu ila hakutoa utetezi wake dhidi ya madai hayo na hivyo hakuna hukumu ambayo inasema kwamba Mbowe sio gaidi.

Tuhuma dhidi yake hazijaondolewa kwa rekodi ya mahakama inabakia hivyo.
 
Huyu anaweza akawa Dr Mhogo?
Nimesikitishwa sana na andiko lake hili la chuki.
Mkuu hata ufanye jambo gani.

Rekodi za mahakama bado zinabakia kwamba Mbowe alikutwa na kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma za ugaidi.

Hakuwahi kujitetea.

Hakuna hukumu ya mahakama inayosema sio gaidi.

Kwa hizo facts sioni namna anafaa kuendelea na nafasi yake.
 
Mkuu hata ufanye jambo gani.

Rekodi za mahakama bado zinabakia kwamba Mbowe alikutwa na kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma za ugaidi...
Mwambie Mwenyekiti wako; umuonye juu ya kukutana na mtu asiye mwadilifu.

Hii mada imekutoa kwenye reli kwelikweli mkuu na kukufanya uonekane kivingine kabisa kuliko ulivyoanza kuonekana.
 
Uadilifu ni sifa kuu na ya msingi anayopaswa kuwa nayo kiongozi yeyote yule wa Taasisi ya uma.

Chadema kama chama kingine cha siasa ni Taasisi ya uma kwa kuwa imesajiliwa kwa kufuata sheria za nchi zinazoongoza vyama vya siasa hapa nchini kwa maana hiyo haikwepi kuwa na vigezo muhimu vya taasisi yeyote ya uma ikiwa na kigezo nilichokitaja awali cha uadilifu wa viongozi wake....
Ndio Ile certificate ya Law from Zoom College imekufikisha hapo?

Sent from my SM-J700F using JamiiForums mobile app
 
Wewe na wenzako kajifunze DPP akishasema hana nia ya kuendelea na kesi automatic jaji anaifuta ile kesi moja kwa moja na hautishitakiwa tena na kesi ya namna il.

Ukiona mtu ameachiwa na mahakama akakamatwa tena palepale ujue shitaka dhidi yake litabadilika sio lile alilokamatw nalo awali.
Uwe unafuatilia sharia za nchi hasa za uendeshaji wa kesi.

Kwa sasa sheria imepitungwa na bunge kuwa mtuhumiwa akiachiwa huru na mahakama hatakiwi kukamatwa tena na polisi .
Acha kula ugoro usiku na kuanza kupiga chafya hovyo kanisani
 
Mkuu hata ufanye jambo gani.

Rekodi za mahakama bado zinabakia kwamba Mbowe alikutwa na kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma za ugaidi...
Sasa hili kosa la DPP kwa nini unalihamishia kwa Mbowe? Mbowe alikuwa tayari kuanza utetezi wake, kwanini DPP akasema hana nia ya kuendelea na hiyo kesi?

Sawa hakuna hukumu ya mahakama inayosema Mbowe sio gaidi, basi wewe tuwekee hiyo hukumu ya mahakama inayosema Mbowe ni gaidi.

Kusema Mbowe amechafuka kwa tuhuma ambazo hazijathibitishwa kwa hukumu ya mahakama ni kichekesho, kwa mtindo huo kila mtu anaweza kuchafuliwa kwa tuhuma za kutengeneza, hili haliwezi kuruhusiwa kwa taifa la wanaojitambua.
 
Back
Top Bottom