Mbowe ataka rasilimali watu ikomboe Afrika kiuchumi

Mbowe ataka rasilimali watu ikomboe Afrika kiuchumi

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na akiwa Afrika ya Kusini, Mbowe Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Vyama vya Demokrasia Afrika (DUA), ametoa wito huo nchini Afrika Kusini, akifungua kongamano la kujadili usalama na ulinzi, demokrasia na biashara barani humo, lilikoandaliwa na DUA.

Mbowe amesema idadi ya watu wa Afrika haijatumika vyema kuwa mtaji wa kusukuma maendeleo, badala yake imekuwa mzigo kwa maendeleo ya watu na bara Hilo.

Amesema Afrika inapaswa kuendeleza watu wake kuwa rasilimali ambayo ni bora kuliko maliasili inayoweza kupatikana.
popote.
Aidha, Mbowe amezitaka vyama wanachama wa DUA kuweka mikakati ya kutumia rasilimali ardhi ya Afrika kuleta maendeleo.

“Mtazamo wangu ndugu washiriki ni kwamba, kama tunataka kulibadilisha bara letu, lazima tufikiri na kujikita katika kuwaelimisha watu wetu na si pungufu ya hapo,” amesema Mbowe na kuongeza:

“Ulaya na Amerika wana watu wachache lakini wao ndiyo mihimili ya dunia kwa sababu ya mtaji wa rasilimali watu.”
 
ingelikuwa ivo basi India ingekuwa nchi tajiri duniani.
 
Unamwelimisha vipi mtu kwa Kumtukana. Na kumdalilisha?

Negative reinforcement inayohubiriwa na Makada wake hapa nchini na mitandaoni itaja leta taharuki zaidi kuliko tija wanayoitafuta kwa mbinubhasi kama hizo.
Anyways, ni Mwanasiasa.
 
1683154693467.png
 
Back
Top Bottom