Mbowe hajawahi kung'ang'ania madarakani CHADEMA, madai ya hivi ni upotoshaji wa kisiasa tu.

Mbowe hajawahi kung'ang'ania madarakani CHADEMA, madai ya hivi ni upotoshaji wa kisiasa tu.

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Mbowe anaweza kulaumiwa kwa mambo yote lakini jambo moja kubwa ambalo hawezi kulaumiwa nalo ni kung'ang'ania au kukaa madarakani muda mrefu. Lissu mwenyewe ambaye ndiye mpinzani mkuu wa Mbowe katika nafasi ya mwenyeketi kwa sasa na anayetaka ukomo wa kushika madaraka ndani ya CHADEMA uwekwe anasema alishiriki kikamilifu kupendekeza na katika maamuzi ya kuondoa ukomo wa uongozi ndani ya CHADEMA mwaka 2006 kwa sababu ya uchanga wa chama na ukosefu wa viongozi wa kutosha katika kugombea na kushika nafasi za uongozi ndani ya CHADEMA.

Mara zote ambazo Mbowe amegombea uenyekiti wa CHADEMA hakujawahi kuwa na washindani wa maana kumpa changamoto katika uchaguzi. Lissu anasema Zitto, Kitilia na Chacha Wangwe(ambao waliwahi kuonekana kama wangempa changamoto) walikuwa wanataka kufanya mapinduzi ya uongozi ndani ya chama badala ya kufuata taratibu rasmi za wazi za chama za uchaguzi kama anavyofanya yeye sasa
 
Mbowe anaweza kulaumiwa kwa mambo yote lakini jambo moja kubwa ambalo hawezi kulaumiwa nalo ni kung'ang'ania au kukaa madarakani muda mrefu. Lissu mwenyewe ambaye ndiye mpinzani mkuu wa Mbowe katika nafasi ya mwenyeketi kwa sasa na anayetaka ukomo wa kushika madaraka ndani ya CHADEMA uwekwe anasema alishiriki kikamilifu kupendekeza na katika maamuzi ya kuondoa ukomo wa uongozi ndani ya CHADEMA mwaka 2006 kwa sababu ya uchanga wa chama na ukosefu wa viongozi wa kutosha katika kugombea na kushika nafasi za uongozi ndani ya CHADEMA.

Mara zote ambazo Mbowe amegombea uenyekiti wa CHADEMA hakujawahi kuwa na washindani wa maana kumpa changamoto katika uchaguzi. Lissu anasema Zitto, Kitilia na Chacha Wangwe(ambao waliwahi kuonekana kama wangempa changamoto) walikuwa wanataka kufanya mapinduzi ya uongozi ndani ya chama badala ya kufuata taratibu rasmi za wazi za chama za uchaguzi kama anavyofanya yeye sasa
Acha hadaa ,Mzee Mbowe anasema wazi hawezi ona chama chake kikichezewa
 
😂 😂 Basi na ccm haing'anga'nii madarakani
Lakini Mbowe hajaandikisha watoto wa shule wapige kura CHADEMA, lakini hajaweka wasiojiandikisha wapige kura,lakini hajaweka walimu na watendaji na mgambo na polisi na wakurugenzi wampitishe,hajaficha orodha ya wapig kura,hajatiki kura za kutumbukiza,waziri wa Tamisemi siyo mkwilima wa Mbowe,Tume ya uchaguzi na Tamisemi humtumikia Rais na si Mbowe. Huku ndiko kung'ang'ania madarakani.
 
Juzi juzi tu walikuwa wanaimba "tuvusheeee..... Mbowe tuvusheeee" kipindi hicho Chadema wamekabwa koo na jiwe, sasa hivi wanajifanya kusema eti Mbowe anakatalia madarakani
 
Back
Top Bottom