The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amesema kuwa hospitali zote za umma na binafsi zinapaswa kuwahudumia wajawazito na wagonjwa wa dharura bila masharti ya malipo ya awali.
Ametoa kauli hiyo bungeni Ijumaa, Januari 31, 2025, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonest, kuhusu changamoto za wanawake wanaoshindwa kupata vifaa vya kujifungua.
"Tunatoa maelekezo mahususi kwamba mama na mtu yeyote wa dharura akifika hospitalini ni lazima apate huduma kwanza. Si sahihi kuulizwa fedha au chochote kabla ya kupatiwa matibabu," amesema Dkt. Mollel.
Hata hivyo, ameeleza kuwa gharama za huduma kwa akina mama na watoto zinaendelea kuwa changamoto kubwa kwa serikali. Amesema kwa mwaka 2024, gharama hizo zilifikia Shilingi bilioni 227, wakati bajeti ya huduma zote za afya ilikuwa Shilingi bilioni 200.
"Tunajitahidi kuweka mizania, lakini ukweli ni kwamba baadhi ya wananchi hawajali maandalizi ya afya zao. Unakuta mtu huyo huyo hana bima ya afya lakini anachangia mamilioni kwenye harusi, halafu akifika hospitali anataka huduma bure. Serikali imetumia Shilingi bilioni 661 kwa msamaha wa huduma za afya mwaka juzi, lakini tukubaliane kuwa kupanga ni kuchagua," amesisitiza.
Soma: Naibu Waziri Godwin Mollel amuunga mkono Chalamila kuhusu wajawazito: Unakuta mtu hana bima lakini anachangia Milioni kwenye harusi!
Kauli hiyo ya serikali imekuja baada ya Mbunge Anatropia Theonest kulifikisha bungeni sakata la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye alinukuliwa akisema "wajawazito wasiotaka kununua glavu wakajifungulie nyumbani".
Mbunge huyo ameeleza kuwa kauli kama hizo kutoka kwa viongozi wa serikali zinakatisha tamaa na zinaweza kuchangia vifo vya wajawazito.
"Wakati mwingine kukosa vifaa husababisha maambukizi na hata vifo wakati wa kujifungua. Ni nini kauli ya serikali kwa wanawake hawa, lakini pia kwa viongozi waliopaswa kuwasaidia badala ya kuwakatisha tamaa?" amehoji Anatropia.
Akijibu hoja hiyo, Dkt. Mollel amesema kauli za viongozi mara nyingi hupotoshwa kwa kuchukuliwa vipande vidogo vya mazungumzo yao, hivyo ni muhimu kuelewa muktadha wa kile kilichosemwa kabla ya kutoa hitimisho.
See translation
Ametoa kauli hiyo bungeni Ijumaa, Januari 31, 2025, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Anatropia Theonest, kuhusu changamoto za wanawake wanaoshindwa kupata vifaa vya kujifungua.
"Tunatoa maelekezo mahususi kwamba mama na mtu yeyote wa dharura akifika hospitalini ni lazima apate huduma kwanza. Si sahihi kuulizwa fedha au chochote kabla ya kupatiwa matibabu," amesema Dkt. Mollel.
Hata hivyo, ameeleza kuwa gharama za huduma kwa akina mama na watoto zinaendelea kuwa changamoto kubwa kwa serikali. Amesema kwa mwaka 2024, gharama hizo zilifikia Shilingi bilioni 227, wakati bajeti ya huduma zote za afya ilikuwa Shilingi bilioni 200.
"Tunajitahidi kuweka mizania, lakini ukweli ni kwamba baadhi ya wananchi hawajali maandalizi ya afya zao. Unakuta mtu huyo huyo hana bima ya afya lakini anachangia mamilioni kwenye harusi, halafu akifika hospitali anataka huduma bure. Serikali imetumia Shilingi bilioni 661 kwa msamaha wa huduma za afya mwaka juzi, lakini tukubaliane kuwa kupanga ni kuchagua," amesisitiza.
Soma: Naibu Waziri Godwin Mollel amuunga mkono Chalamila kuhusu wajawazito: Unakuta mtu hana bima lakini anachangia Milioni kwenye harusi!
Kauli hiyo ya serikali imekuja baada ya Mbunge Anatropia Theonest kulifikisha bungeni sakata la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye alinukuliwa akisema "wajawazito wasiotaka kununua glavu wakajifungulie nyumbani".
Mbunge huyo ameeleza kuwa kauli kama hizo kutoka kwa viongozi wa serikali zinakatisha tamaa na zinaweza kuchangia vifo vya wajawazito.
"Wakati mwingine kukosa vifaa husababisha maambukizi na hata vifo wakati wa kujifungua. Ni nini kauli ya serikali kwa wanawake hawa, lakini pia kwa viongozi waliopaswa kuwasaidia badala ya kuwakatisha tamaa?" amehoji Anatropia.
Akijibu hoja hiyo, Dkt. Mollel amesema kauli za viongozi mara nyingi hupotoshwa kwa kuchukuliwa vipande vidogo vya mazungumzo yao, hivyo ni muhimu kuelewa muktadha wa kile kilichosemwa kabla ya kutoa hitimisho.
See translation