Mbunge ashauri Serikali kuweka mtaala wa kufundisha Watoto kalenda ili kuzuia Mimba za Utotoni

Mbunge ashauri Serikali kuweka mtaala wa kufundisha Watoto kalenda ili kuzuia Mimba za Utotoni

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532

Mimba pc

Dodoma. Mbunge wa Kigoma Kusini nchini Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nashon Bidyangunze ameshauri Serikali kuweka mtaala ambao utawafundisha watoto kufahamu vyema kalenda.

Nashoni ameyasema hayo Oktoba 24, 2021 wakati akizungumza katika semina ya kuangalia namna bora ya kuboresha huduma za afya iliyoandaliwa Taasisi ya Benjamin Mkapa na kuwahusisha wajumbe wa kamati mbili za Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na Utawala na Serikali za Mitaa.

Akichangia mjadala huo Bidyangunze amesema kwa mujibu wa mwezeshaji katika semina hiyo kuwa watoto 8,000 wanapata ujauzito karibu kila mwaka nchini.

“Nilikuwa natafakari katika eneo hilo la watoto wanapata mimba basi Serikali iweke mtaala ambao unawafundisha watoto kujua kalenda. Kwa sababu huwezi kuzuia hili jambo la watu wawili kukutana faragha kujamiana,” amesema.

Amesema kwa kuwa sio rahisi kulizuia hilo basi kuwepo na elimu itakayofundisha masuala ya uzazi ili kuwapa watoto ufahamu ni wakati gani mimba inaweza kuingia.

“Yes (ndio) wakijua hili la kalenda basi mimba zitapungua, lakini bila elimu unakutana naye leo kumbe ndio siku ya mimba. Kumbe angesubiri kidogo asingepata mimba. Ukweli unabakia pale pale,” amesema mbunge huyo.

Amesema hata Serikali ilipofikia mahali pakutambulisha suala la matumizi ya kondomu kuna watu walishangaa na kuhoji kuwa ni vipi Serikali inahamasisha kujamiana, lakini jambo hilo lilikuwa lina maana kwamba kondomu ikitumika itasaidia watu wasipate magonjwa,” amesema Bidyangunze.

Chanzo: Mwananchi
 
Asisahau pia kukwea kileleni itakuwa ni rahisi(yaani watarahisishiwa) maana tayari watakuwa wanajua jinsi ya kukwea siku salama.
 
Katika sayansi ya maumbile na makuzi mtoto anaweza kupata mimba? Mtoto hawezi kupata mimba, hao wanaopata mimba si watoto ni watu wazima ila siasa tu zimeamua waitwe watoto
 
Kwani haifundishwi secondary? Nakumbuka sisi tulifundishwa. Au anaongelea shule ya msingi?
 
Kwani haifundishwi secondary? Nakumbuka sisi tulifundishwa. Au anaongelea shule ya msingi?
Sijui kasoma shule gani huyu mbunge.

Reproducrion ya form 3 ina cover vizuri hii elimu ya Uzazi kwa qa kike na kiume. Kama anataka elimu ifundishwe chini ya hapo, kwangu ni big no. Wawaache wa ujaribu moto.

By the way Morogoro kuna wazazi hua wanawapandikiza mabinti zao Vijiti mapema kabisa wasipate mim.... [emoji1787][emoji1787]
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]NTAKUJA kuniambia ngono zitakua hovyo hovyo hii ngozi nyeusi inashida
 
Mambo ya uzazi mbona yanafundishwa kuanzia shule za msingi? Hao watoto wanaopata mimba ni wageni wa tendo la ndoa, ni mara yao ya kwanza kujaribu na hapohapo wanapata mimba, hawajui kujikinga
 
Yupo sahihi,lakin wataalam wetu hata wao kalenda hawaijui vzur

Kuna ambao wanasema mwanamke akkaribia kwenye sku zake anakuwa salama,kuna wengine wanasema mwanamke akkaribia kwenye sku zake anaweza kupata mimba
 
Yupo sahihi,lakin wataalam wetu hata wao kalenda hawaijui vzur

Kuna ambao wanasema mwanamke akkaribia kwenye sku zake anakuwa salama,kuna wengine wanasema mwanamke akkaribia kwenye sku zake anaweza kupata mimba
Nani alikupa hii taarifa? Ana utaalamu wa nn?

[emoji849][emoji849]
 
Sikubaliani naye hata kidogo. Watoto wataanza kuijaribu kanuni ya kalenda.
Unacho waza vice versa yake ndio inaishi mtaani kiasi cha kupelekea majuto, vilioz "watoto wa mtaani", single mothers, n.k

"Tafakari Chukua hatua.."
 
Mimi naona cha muhimu kuwafunza wazazi kuwalea watoto wao kwa maadili.. Maana these days maadili yamepolomoka unakuta mtoto anavaa sex cloth.. Yaani all things is about sex.. na wazazi wanaona tu na wametulia.. Hiyo kalenda bado haiwezi kusaidia kama wazazi wako ivo.. Hata ivyo iyo elimu inafundishwa sanaa mashuleni lakin ndo kwanza mimba zinaongezeka.. Hapo ndo sasa inabidi serikali, wazazi walitazame upya hili swala
 
Uzinzi/uasherati ni roho kamili na si tabia kama wanavyojua wengine, it is like a demon walking behind your shadow during the day and during nights it does follow your smell.

Hii sio kitu ya mtaala wala nini, kuna nchi kuna adhabu za wanawake kupigwa mawe mpaka kifo lakini umewahi jiuliza kwanini uzinzi/uasherati unaendelea katika hizo sehemu
 
vipi kuhusu maambukizi mengine ya magonjwa ya ngono kalenda itasaidia pia?
 
Back
Top Bottom