Pre GE2025 Mbunge David Silinde: Anaetamani kugombea jimbo la Tunduma aje, tutamnyoosha kuliko kipindi chochote

Pre GE2025 Mbunge David Silinde: Anaetamani kugombea jimbo la Tunduma aje, tutamnyoosha kuliko kipindi chochote

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mbunge wa Jimbo la Tunduma, David Silinde, amewapa ujumbe mzito wanaotamani kugombea nafasi yake katika Uchaguzi Mkuu ujao, akisisitiza kuwa maendeleo makubwa yaliyofanyika chini ya uongozi wake yanampa uhakika wa ushindi mkubwa yeye na Rais Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza jana Februari 22, 2025, mbele ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, Fadhili Mganya, katika ukumbi wa High Class Tunduma, Silinde alisema yeyote anayejiona kichwa ngumu anakaribishwa kuwania, lakini atakutana na uhalisia wa siasa za Tunduma.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"Hakuna cha kubahatisha hapa! Kila kata tumetekeleza miradi mikubwa, tumeshajenga shule 27,tuna shule za ghorofa za kutosha tena bila kuchangisha mwananchi hata shilingi moja. Hivi kweli mtu anaweza kupita hapa bila kuona maendeleo? Tunduma tunatembea kifua mbele!" alisema huku akishangiliwa.

Silinde aliwataka wanaojipanga kugombea kujiandaa vizuri kwani wapiga kura wa Tunduma hawadanganyiki na kwamba CCM chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaungwa mkono kwa nguvu kubwa.

Kauli yake ilizua shangwe ukumbini kwa zaidi ya dakika mbili, ishara kuwa wanachama wa CCM wana imani kubwa na kazi yake jimboni humo.
1740304783088.png
 
Mbunge wa Jimbo la Tunduma, David Silinde, amewapa ujumbe mzito wanaotamani kugombea nafasi yake katika Uchaguzi Mkuu ujao, akisisitiza kuwa maendeleo makubwa yaliyofanyika chini ya uongozi wake yanampa uhakika wa ushindi mkubwa yeye na Rais Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza jana Februari 22, 2025, mbele ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, Fadhili Mganya, katika ukumbi wa High Class Tunduma, Silinde alisema yeyote anayejiona kichwa ngumu anakaribishwa kuwania, lakini atakutana na uhalisia wa siasa za Tunduma.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"Hakuna cha kubahatisha hapa! Kila kata tumetekeleza miradi mikubwa, tumeshajenga shule 27,tuna shule za ghorofa za kutosha tena bila kuchangisha mwananchi hata shilingi moja. Hivi kweli mtu anaweza kupita hapa bila kuona maendeleo? Tunduma tunatembea kifua mbele!" alisema huku akishangiliwa.

Silinde aliwataka wanaojipanga kugombea kujiandaa vizuri kwani wapiga kura wa Tunduma hawadanganyiki na kwamba CCM chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaungwa mkono kwa nguvu kubwa.

Kauli yake ilizua shangwe ukumbini kwa zaidi ya dakika mbili, ishara kuwa wanachama wa CCM wana imani kubwa na kazi yake jimboni humo.View attachment 3246299
well done,
well said ndugu waziri :KasugaYeah:
 
Tatizo ndani ya CCM kuna wanaotaka hiyo nafasi yake pia. Ukimtoa Rais Samia wengine wote wajipange sana kutetea viti vyao. Kura za maoni kwa mwaka huu hazitakuwa rahisi kwa madiwani na wabunge... PATACHIMBIKA. Mwaka 2020 kuna wenye sifa wengi majina yalikatwa kibabe. Tuiombee CCM
 
Back
Top Bottom