Ile report imejaa Usanii na Upotoshaji MKUBWA. Polisi wanasema Majirani hawakusikia kelele za mtu kuvamiwa/ kushambuliwa na Mhe. alikuwa amelewa CHAKARI!
Hapa hakuna weledi wowote ulotumika zaidi ya maoni ya Wabunge wa CCM Bungeni
Kuwa chakari haiwezi kuwa ndiyo kigezo Cha mtu KUUMIA kwa kuanguka. Je, Raia hawezi kushambuliwa akiwa chakari?
Lakini pia K Polisi hawajatueleza Mhe. Mbowe alikuwa amekunywa aina gani ya kilevi? Je, haiwezekani akawa akitiliwa kilevi Maalumu(madawa ya usingizi au kulevya)?
Mbona Mzee Mangula walisema kanyweshwa SUMU na mpaka sasa hawajatuambia Ni sumu gani na Nani alimwekea kwenye chakula au kinywaji?