Mbunge Maganga avuruga Bunge ataka wahusika kashfa ya Bilioni 350 kwa Symbion wakamatwe haraka warejeshe fedha za watanzania

Mbunge Maganga avuruga Bunge ataka wahusika kashfa ya Bilioni 350 kwa Symbion wakamatwe haraka warejeshe fedha za watanzania

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
MBUNGE wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemus Maganga amesema watu wote waliohusika kwenye mkataba wa TANESCO na Symbion na kulisababisha Taifa hasara ya Bilioni 350 wakamatwe mara moja kwani watu wote waliohusika na kashfa hiyo wapo.

Maganga amesema hayo Novemba 4, 2022 bungeni Dodoma wakati akijadili Taarifa za Kamati za PAC, LAAC na PIC kuhusu Ripoti ya CAG ambapo amesema mkataba wa Tanesco na Kampuni ya Symbion ulioingiwa Septemba 2015 umeliingiza taifa kwenye hasara kubwa.

“Hawa watu wote wapo wakamatwe mara moja na hili zoezi ni dogo sana tukilikuza linakuwa kubwa lakini zoezi hili linaweza likamalizwa na mtu mmoja tena Waziri wa Mambo ya Ndani hili suala liko ndani ya uwezo wake mara moja tu akitangaza kesho waripoti Dodoma kwani shida iko wapi waripoti wenyewe kesho tuone trilioni zetu zote tukajenge barabara tufanye na mambo mengine maisha yaendelee” amesema Mhe. Maganga
 

Attachments

  • mbogwee.jpg
    mbogwee.jpg
    39.3 KB · Views: 6
Wabunge vijana wenye ari wachangamke , wasiwaogope hao vijana wapiga dili , kupitia wao Mungu atafanya kitu..ibueni uozo Taifa lione namna wasaliti walivyo , alaf sku yaja ambayo Mungu atawa_consume pamoja na kizazi chao
 
Nguvu iongezeke bado idadi ya wabunge kukemea huu uovu ni ndogo
 
MBUNGE wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemus Maganga amesema watu wote waliohusika kwenye mkataba wa TANESCO na Symbion na kulisababisha Taifa hasara ya Bilioni 350 wakamatwe mara moja kwani watu wote waliohusika na kashfa hiyo wapo.

Maganga amesema hayo Novemba 4, 2022 bungeni Dodoma wakati akijadili Taarifa za Kamati za PAC, LAAC na PIC kuhusu Ripoti ya CAG ambapo amesema mkataba wa Tanesco na Kampuni ya Symbion ulioingiwa Septemba 2015 umeliingiza taifa kwenye hasara kubwa.

“Hawa watu wote wapo wakamatwe mara moja na hili zoezi ni dogo sana tukilikuza linakuwa kubwa lakini zoezi hili linaweza likamalizwa na mtu mmoja tena Waziri wa Mambo ya Ndani hili suala liko ndani ya uwezo wake mara moja tu akitangaza kesho waripoti Dodoma kwani shida iko wapi waripoti wenyewe kesho tuone trilioni zetu zote tukajenge barabara tufanye na mambo mengine maisha yaendelee” amesema Mhe. Maganga
Labda kama watakamatwa na serikali ya kenya, kwa serikali hii ya ccm tutasubiri dana aisee
 
MBUNGE wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemus Maganga amesema watu wote waliohusika kwenye mkataba wa TANESCO na Symbion na kulisababisha Taifa hasara ya Bilioni 350 wakamatwe mara moja kwani watu wote waliohusika na kashfa hiyo wapo.

Maganga amesema hayo Novemba 4, 2022 bungeni Dodoma wakati akijadili Taarifa za Kamati za PAC, LAAC na PIC kuhusu Ripoti ya CAG ambapo amesema mkataba wa Tanesco na Kampuni ya Symbion ulioingiwa Septemba 2015 umeliingiza taifa kwenye hasara kubwa.

“Hawa watu wote wapo wakamatwe mara moja na hili zoezi ni dogo sana tukilikuza linakuwa kubwa lakini zoezi hili linaweza likamalizwa na mtu mmoja tena Waziri wa Mambo ya Ndani hili suala liko ndani ya uwezo wake mara moja tu akitangaza kesho waripoti Dodoma kwani shida iko wapi waripoti wenyewe kesho tuone trilioni zetu zote tukajenge barabara tufanye na mambo mengine maisha yaendelee” amesema Mhe. Maganga
Kwahiyo zinapoibiwa zinakuwa za watanzania , lakini zikijenga shule zinakuwa ni za Mama !
 
Kwanza hawa wote siyo wabunge. Hakuna aliyewachagua. Aliyewapa huo ubunge bandia hayupo Duniani.

Hili ni kundi la waovu lililotengenezwa na marehemu kwa dhamira ovu ya kubadilisha katiba ili awe Rais wa maisha.

Hakuna jema linalotegemewa kutoka kwa hawa waovu.

Wizi huo wa Symbion ni uovu, kupora haki ya wananchi kuchagua wawakilishi wanaowataka, ni uovu mbaya zaidi.

Mwaka 2025, haya majizi ya kura za uchaguzi 2025, iwe marafuku kwenda bungeni. Mtu pekee ambaye matendo yake yanamsafisha na uovu ule wa 2020, ni Rais Samia ambaye kwa matendo anaonesha alikuwa akiumizwa na uovu ule.
 
Back
Top Bottom