Pre GE2025 Mbunge Musukuma atumia zaidi ya Tsh bilioni 1 kununua ambulance, gari la Polisi na kujenga kituo cha Polisi Geita Vijijini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Joined
Nov 19, 2024
Posts
94
Reaction score
307
Mbunge wa Jimbo la Geita, Joseph Musukuma, leo Machi 6, 2025, ameonesha magari 10 ya kubebea wagonjwa pamoja na moja kwa ajili ya Jeshi la Polisi, ambayo atawakabidhi wananchi wa jimbo lake ili kuboresha huduma za afya na usalama wa jamii.

Musukuma amesema magari hayo yatanufaisha wananchi wa Geita Vijijini, ambayo ina jumla ya kata 15, ambapo kila kata itanufaika na gari moja la kubebea wagonjwa. Aidha, ameeleza kuwa atagharamia mishahara ya madereva pamoja na matengenezo yote ya magari hayo. Wananchi watakaohitaji huduma watapaswa kuwasiliana na Katibu wa Chama kwa ajili ya uratibu wa usafiri.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Soma Pia: Kuelekea 2025 - Orodha ya CV za Wabunge kwa mwaka 2020 - 2025 kutoka kila mkoa Tanzania


Mbunge huyo pia amefichua kuwa gharama za mradi huo, ikiwemo ujenzi wa kituo cha Polisi cha kisasa kitakachokabidhiwa kwa Jeshi la Polisi, zimefikia zaidi ya shilingi bilioni moja.

Your browser is not able to display this video.


- Pre GE2025 - Musukuma: Milango iko wazi kwa yeyote mwenye nia ya kugombea ubunge katika jimbo Geita Vijijini
 
Vituko juu ya vituko,
Wagonjwa wafanye mawasiliano na Katibu wa CCM, haya ni maelekezo ya hovyo kutokea. Kwa maana hiyo magari hayo ni mali ya CCM au ni magazi yametolewa kwa wananchi. Kampeni zingine za kijinga. Ukiambiwa wewe ni darasa la saba, unakwenda kununua udaktari wa heshima. Watanzania tutafika mbinguni tuko hoi sana.
 
Hela ya serikali inanunua mitungi ya gesi ya kuhonga masikini, bajeti ya Ambulance inatoka mifukoni mwa watu!
Unafikiri kupanda hizo ambulance πŸš‘ ni bure πŸ˜„ bado watu watapigwa hela πŸ˜„

Ova
 
 

Attachments

  • 20250210_112920.jpg
    586.9 KB · Views: 1
Acheni uongo!! magari hutolewa na serikali au wadau kwa Halmashauri (wakurugenzi) kisha wabunge huyadaka kwa ajili ya maonyesho kwa wananchi wakiwadanganya kuwa wao (wabunge) ndo wameyaleta hayo magari. Mali zote katika Halmashauri ziko chini ya DED. Ila watanzania wengi ni wajinga.
 
Ni kwa fedha zake za mfukoni au kwa fedha zinazotokana na mfuko wa jimbo lake?

Mungu amubariki sana; tuendelee kumuombea!
 
Hata angesema walio wahitaji wa ambulance wawasiliane na mwenyekiti wa Serikali ya mtaa; bado ungesema kuwa mwenyekiti huyo ni wa Serikali ya CCM

Tuache ubabaishaji kwenye vitu serious kama hivi; mtu kajitoa billion nzima wakati mimi hapa nilipo sina hata million moja ambayo naweza kuitoa.

Wewe unayo angalau hata million moja tu unayoweza kuwasaidia watu hao aliowasaidia Mh Mbunge huyu?
 
Na huo ndiyo ukweli, aonyeshe risiti amenunua wapi na lini?
 
Na hiyo siyo fedha ake ni ujanja ujanja kutoka kwa wadau na matapeli mengine ya mali za umma
 
Katika nchi inatakataka madarakani ni msukuma huyu.

Yani anajua kudakia mambo,kuropoka na kuingilia kitu kama chawa
 
Lile deni lake ameshalilipa?
 
πŸ™πŸ»πŸ™πŸ» Musukuma mwenyez mungu akujalie, zaidi ujekua raisi, wa nchi
 
Kazi ya Ubunge na Siasa ukiwa huko juu inalipa kweri kweri !
Ila ukiwa chini chini utaambulia kapelo T-shirt na buku buku za double kiki ili ukatumwe kumdhalilisha hata Mzee Eti tu kwa sababu anakosoa hao Wanasiasa na mipesa yao πŸ˜³πŸ™„ !
Wajinga ndio waliwao 😱 πŸ‘
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…