Wana JF
Wakati tunaenda kuchagua wabunge ni vizuri tukijadili nani anatufaa na tunahitaji nini kutoka kwa hawa tunaowaajiri.
Kwa mtazamo wangu mimi nafikiri Mbunge ni kama meneja wa mahali husika na hivyo anahusika moja kwa moja na kuibua mikakati ya maendeleo mahali husika.Haimlazimu mbunge wa mahali husika kuwa tajiri wa mali aidha utajiri unaotakiwa ni wa mawazo yatakayoleta tofauti.Sasa wabunge wetu wanawaza tofauti ukienda kwenye vijiji vyetu sasa hivi utakuta vumbi kibao,kila mbunge anakimbilia kulima barabara (na sio kutengeneza) muda huu wa mwishoni ili aweze kuwahadaa wananchi.Hali kama hiyo inanipa maswali mengi ya kujiuliza! Utakuta wananchi mafua kibao kisa vumbi.Kwa kiwango cha ulipuaji wa namna hiyo kunasababisha barabara kuharibika baada ya muda mfupi baadae.Barabara hata isipowekwa lami lakini ikachimbwa,kuwekwa maji na kushindiliwa vizuri inaweza kuchukua muda kuharibika na kupunguza matatizo kwa wananchi.
Tunategemea kwenda kusikiliza wagombea ubunge wakijinadi ili wapati wakati mwingine wa kutawala.Ni lazima kuwa makini.Ni vizuri kuwahoji ni nini hasa wamechangia kuibua maendeleo katika sehemu husika.Inasikitisha sehemu kama moshi vijijini mbunge hasemi lolote kunusuru mradi mkubwa wa umwagiliaji wa lower moshi,yupo kimya akianza kuongea atakuta wengine wameshaongea na pengine wameshaeleweka.Tunataka mikataba na wabunge akiahidi kitu kiwekwe kwenye maandishi.Kwa jinsi hii ungekuta kuna kesi kibao mahakamani dhidi ya wabunge walaghai.
Inakuwaje mbunge anashindwa hata kuwakusanya vijana kuwachochea waanzishe mikakati yao wenyewe ya kukusanya mitaji na baada ya muda wanaweza wakaanza kitu fulani au kutumia nguvu zao wenyewe labda kufyetua matofali then wakauza vizuri tu.Ipo miradi mingi tu cha kujiuliza nani akiopata ubunge anakaa karibu na wananchi? Kila mtu anakimbilia dar es salaam.
tusipojitahidi kuwa makini nchi hii itajeuzwa ya kuongeaongea tu na vitendo never.Ubunge ni ajira na mwajiriwa lazima awajibike.
Wakati tunaenda kuchagua wabunge ni vizuri tukijadili nani anatufaa na tunahitaji nini kutoka kwa hawa tunaowaajiri.
Kwa mtazamo wangu mimi nafikiri Mbunge ni kama meneja wa mahali husika na hivyo anahusika moja kwa moja na kuibua mikakati ya maendeleo mahali husika.Haimlazimu mbunge wa mahali husika kuwa tajiri wa mali aidha utajiri unaotakiwa ni wa mawazo yatakayoleta tofauti.Sasa wabunge wetu wanawaza tofauti ukienda kwenye vijiji vyetu sasa hivi utakuta vumbi kibao,kila mbunge anakimbilia kulima barabara (na sio kutengeneza) muda huu wa mwishoni ili aweze kuwahadaa wananchi.Hali kama hiyo inanipa maswali mengi ya kujiuliza! Utakuta wananchi mafua kibao kisa vumbi.Kwa kiwango cha ulipuaji wa namna hiyo kunasababisha barabara kuharibika baada ya muda mfupi baadae.Barabara hata isipowekwa lami lakini ikachimbwa,kuwekwa maji na kushindiliwa vizuri inaweza kuchukua muda kuharibika na kupunguza matatizo kwa wananchi.
Tunategemea kwenda kusikiliza wagombea ubunge wakijinadi ili wapati wakati mwingine wa kutawala.Ni lazima kuwa makini.Ni vizuri kuwahoji ni nini hasa wamechangia kuibua maendeleo katika sehemu husika.Inasikitisha sehemu kama moshi vijijini mbunge hasemi lolote kunusuru mradi mkubwa wa umwagiliaji wa lower moshi,yupo kimya akianza kuongea atakuta wengine wameshaongea na pengine wameshaeleweka.Tunataka mikataba na wabunge akiahidi kitu kiwekwe kwenye maandishi.Kwa jinsi hii ungekuta kuna kesi kibao mahakamani dhidi ya wabunge walaghai.
Inakuwaje mbunge anashindwa hata kuwakusanya vijana kuwachochea waanzishe mikakati yao wenyewe ya kukusanya mitaji na baada ya muda wanaweza wakaanza kitu fulani au kutumia nguvu zao wenyewe labda kufyetua matofali then wakauza vizuri tu.Ipo miradi mingi tu cha kujiuliza nani akiopata ubunge anakaa karibu na wananchi? Kila mtu anakimbilia dar es salaam.
tusipojitahidi kuwa makini nchi hii itajeuzwa ya kuongeaongea tu na vitendo never.Ubunge ni ajira na mwajiriwa lazima awajibike.