Mbunge Nicholaus Ngassa: Mkandarasi zingatia ratiba ya utekelezaji wa mradi

Mbunge Nicholaus Ngassa: Mkandarasi zingatia ratiba ya utekelezaji wa mradi

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
MBUNGE NICHOLAUS NGASSA: "MKANDARASI ZINGATIA RATIBA YA UTEKELEZAJI WA MRADI" - JIMBO LA IGUNGA

Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa, amemtaka Mkandarasi wa Mradi wa Usambazaji wa Maji ya Ziwa Victoria kwenye Vijiji vya Kata za Mwamashiga, Mbutu, Isakamaliwa, Kining'inila, Mwamashimba, Mwamakona, Igurubi na Kinungu kuzingatia muda na ratiba ya utekekelezaji wa mradi kama ilivyopangwa kwenye Mkataba.

Mheshimiwa Ngassa (MB) ametoa rai kwa mkandarasi Leo tarehe 20 Februari 2023 baada ya kufanya Ziara kwenye eneo la utekekelezaji wa mradi na kuona maendeleo ya mradi.

Aidha Mheshimiwa Ngassa (MB) ameendelea kutoa shukrani kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kutoa Fedha kwa mkandarasi anaetekeleza mradi mkubwa wa Usambazaji wa Maji ya Ziwa Victoria kwenye Jimbo la Igunga. Mradi unatarajiwa kukamilika Mwezi Disemba 2023.

"Kazi na Maendeleo"

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga

WhatsApp Image 2023-02-20 at 16.15.57(1).jpeg

WhatsApp Image 2023-02-20 at 16.15.58(1).jpeg

WhatsApp Image 2023-02-20 at 16.15.58(2).jpeg
 
Wabunge waliopita kwa Udikteta wa jiwe wala hata hawajulikani. Huyu ndiyo kwanza namsikia.
 
Back
Top Bottom