Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MBUNGE SUBIRA MGALU AKABIDHI VYEREHANI 130 VYA MILIONI 32.5
Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Subira Mgalu ameendelea kutekeleza azma yake ya kuwaimarisha kiuchumi Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) katika Wilaya za Mkoa wa Pwani, ambapo amekabidhi vyerehani 20 wilayani Kisarawe na kutimiza idadi ya vyerehani 130 vyenye thamani ya shilingi milioni 32.5 ambavyo ashavigawa katika Mkoa wa Pwani.
"Haijapata kutokea tangu uhuru kuwepo kwa mifumo ya kuhudumia wagonjwa wa dharura kuanzia ngazi za wilaya, wodi za dharura zinatarajiwa kutoa mchango wa kupunguza vifo vya mama wajawazito na majeruhi karibu kwa 40%, sasa safari za rufaa kwenda Muhimbili zimepungua sana, ahsante Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yako, afya ni mtaji" - Mhe. Subira Mgalu (Mb)
"Wodi za dharura zimeweza kupunguza vifo vya Mama wajawazito na watoto kwa asilimia 40, safari za kwenda Muhimbili zimepungua" - Mhe. Subira Mgalu
Mhe. Subira Mgalu katika ziara yake amesema ameridhishwa na kazi ya Uboreshaji Miundombinu ya Afya Hospital ya Wilaya Kisarawe ambayo ni kazi nzuri ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi, Awamu ya Sita
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-04-27 at 20.08.53(1).jpeg55.1 KB · Views: 1 -
WhatsApp Image 2023-04-27 at 20.08.53.jpeg52.6 KB · Views: 5 -
WhatsApp Image 2023-04-27 at 20.08.54(1).jpeg53.1 KB · Views: 1 -
FuurjbLWcAEsk1g.jpg64.7 KB · Views: 1 -
FuuriX8WcAEwa59.jpg64.5 KB · Views: 1 -
FuurjE3XwAUSL4l.jpg61.8 KB · Views: 1 -
WhatsApp Image 2023-04-27 at 20.08.57(1).jpeg49.6 KB · Views: 1