Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Mhe. Suma Fyandomo amesema kwa sasa mtu akifika katika Jiji la Mbeya hajui mjini ni wapi kutokana na mpangilio wa jiji hilo.
"Wananchi wa mkoa wa Mbeya, kiu yao wanatamani kuona jiji lile linafanana na majiji mengine," amesema Fyandomo akisema sasa hivi haijulikani mjini ni wapi.
Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025 na kuongeza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni ujenzi holela, na kwamba ikitatuliwa wakazi wa Mbeya watakuwa wameheshimishwa.
Ameongeza kuwa ni muhimu jiji hilo likawa lenye hadhi inayokubalika ikifahamika kwamba ndipo anapotoka Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Mabungeni Duniani, Dkt. Tulia Ackson
"Wananchi wa mkoa wa Mbeya, kiu yao wanatamani kuona jiji lile linafanana na majiji mengine," amesema Fyandomo akisema sasa hivi haijulikani mjini ni wapi.
Amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha wa 2024/2025 na kuongeza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni ujenzi holela, na kwamba ikitatuliwa wakazi wa Mbeya watakuwa wameheshimishwa.
Ameongeza kuwa ni muhimu jiji hilo likawa lenye hadhi inayokubalika ikifahamika kwamba ndipo anapotoka Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Mabungeni Duniani, Dkt. Tulia Ackson