Mbunge Tauhida: Wasanii wasio na skendo wapewe "Pasipoti za Huduma" kuwarahisishia safari zao Kimataifa

Mbunge Tauhida: Wasanii wasio na skendo wapewe "Pasipoti za Huduma" kuwarahisishia safari zao Kimataifa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wadau huko Bungeni kuna mapendekezo ya Wasanii wapewe Service Passports

Mbunge wa Viti Maalum, Tauhida Nyimbo amependekeza Wasanii wa Tanzania ambao hawana skendo na wanaiwakilisha nchini kimataifa wapewe "Pasipoti za Huduma", ambayo hupatiwa Mkuu wa Mkoa, Msajili wa Mahakama ya Rufaa au Mahakama Kuu, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Kamishna katika Tume yoyote ya Serikali, Maafisa wa JWTZ wenye cheo cha Kanali au Brigedia Jenerali, Msaidizi Binafsi na Mshauri wa Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Zanzibar au Waziri Mkuu, Naibu Kamishna wa Magereza na Maafisa wengine.
Soma: Yanayojiri Bunge la kumi na mbili mkutano wa 17 kikao cha nne Novemba 1, 2024
 
Hili ni chepua la aina yake.
Na kwa mwendo huu ni kama naota vile lakini,
tusishangae hata 'MACHAWA' mbeleni huko wakapata Hati zenye hadhi ya 'KiDiplomasia'.
Nasema tu.
 
Back
Top Bottom