Wadau huko Bungeni kuna mapendekezo ya Wasanii wapewe Service Passports
Mbunge wa Viti Maalum, Tauhida Nyimbo amependekeza Wasanii wa Tanzania ambao hawana skendo na wanaiwakilisha nchini kimataifa wapewe "Pasipoti za Huduma", ambayo hupatiwa Mkuu wa Mkoa, Msajili wa Mahakama ya Rufaa au Mahakama Kuu, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Kamishna katika Tume yoyote ya Serikali, Maafisa wa JWTZ wenye cheo cha Kanali au Brigedia Jenerali, Msaidizi Binafsi na Mshauri wa Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Zanzibar au Waziri Mkuu, Naibu Kamishna wa Magereza na Maafisa wengine.
Hili ni chepua la aina yake.
Na kwa mwendo huu ni kama naota vile lakini,
tusishangae hata 'MACHAWA' mbeleni huko wakapata Hati zenye hadhi ya 'KiDiplomasia'.
Nasema tu.