LGE2024 Mbunge Vuma Holle Aendelea Kuzisaka Kura Kwenye Mvua

LGE2024 Mbunge Vuma Holle Aendelea Kuzisaka Kura Kwenye Mvua

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE VUMA HOLLE AENDELEA KUZISAKA KURA KWENYE MVUA

Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini, Mhe. Augustine Vuma Holle ameendelea na Kampeni za kuwaombea kura wagombea wanaotokana na CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa Unaotarajiwa Kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024 wakati Mvua ikiendelea kunyesha.

Katika Kampeni zake, Mhe. Augustine Vuma amesema kuwa wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinajiandaa na suala la uchaguzi wa Serikali za Mitaa, wao vyama vya upinzani walikuwa wanahamasisha maandamano kwa wananchi na hivyo upinzani utaendelea kushindwa mbele ya CCM.

Akiwa katika Kata ya Buhoro (Kasulu Vijijini), Mhe. Vuma Holle amesema Tanzania imepiga hatua katika ujenzi wa Barabara za lami kutoka Kilomita 86,472 (Mwaka 2020) hadi Kilomita 91,532 (2023). Barabara za Changarawe Kilomita 893.04 (Mwaka 2020) hadi Kilomita 1042.43 (Mwaka 2023).

Aidha, Mbunge Vuma Holle amesema Hadi sasa jumla ya Vijiji 5,481 vimesambaziwa umeme na kufanya jumla ya vijiji 11,837 sawa na 96.37% kati ya Vijiji 12,318 vya Tanzania Bara.

"Kwa mambo mengi yaliyofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yanazidi kuweka imani kwa wananchi ya kuendelea kuipigia kura CCM na katika uchaguzi huu, CCM inaenda kushinda kwa kishindo nchi nzima" - Mhe. Augustine Vuma Holle, Mbunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.33.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.33.jpeg
    184.7 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.34.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.34.jpeg
    172.9 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.34 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.34 (1).jpeg
    142.4 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.35 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.35 (1).jpeg
    152.4 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.36.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.36.jpeg
    114.6 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.36 (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.36 (1).jpeg
    105.7 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.37.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-25 at 09.32.37.jpeg
    132.9 KB · Views: 2
Vupi hajalala chini na ku galagala kwenye matope???
 
Wabunge wasiojua kazi yao huwa wanatafuta kiki za kishenzi kama hizi. Kunyeshewa mvua, so what?
 
Vipi haja galagala chini kwenye matope huku akiahidi kuwaletea wananchi maendeleo????
Ccm bhana ati mtu ana ahidi kuwaletea wenzake MAENDELEO! ??? Maendeleo yanaletwa na mtu mmoja? Imekuwa chupa ya MAJI?
Maendeleo ni mchakato. Hayawezi kuletwa na mtu kama kikombe cha chai au bahasha
 
Back
Top Bottom