milele amina
JF-Expert Member
- Aug 16, 2024
- 6,045
- 8,080
MBUNGE WA MOSHI AWA GUMZO MITAA YA MIEMBENI
UTANGULIZI
Katika hali isiyo ya kawaida Mbunge wa Moshi Mjini Mhe. Priscus Tarimo amekuwa gumzo katika mitaa mbalimbali ya Miembeni na Njoro baada ya kuhudhuria misiba miwili iliyokuwa jirani na kufanya jambo lililotafsiriwa kuwa sio la kiungwana.
Msiba wa kwanza ulikuwa maeneo ya Motherland kwa mama Aguu ambayo ni familia duni. Mhe. Mbunge alifika katika msiba huo na kupewa nafasi ya kutoa salaam sambamba na kutoa ahadi ya rambirambi ya shilingi laki moja (100,000/=)
Aidha baada ya hapo alielekea kwenye msiba kwa Adam Mamjombaa ni baba mlezi wa Mfanyabiashara maarufu mjini Moshi Nasib Gogo. Katika msiba huo alipata nafasi ya kutoa salaam na kutoa fedha taslim shilingi laki mbili na nusu. (250,000/=).
Kutoa 250,000/= taslim kwenye msiba wa watu wanaojiweza na kutoa ahadi ya 100,000/= kwa familia duni na inayohitaji msaada imetafsiriwa kuwa ni ubaguzi na unyanyapaa.
Akiongea kwa masikitiko makubwa mmoja wa waombolezaji mzee Hamis amesema ni nadra sana kwa Mbunge kuhudhuria misiba hasa ya watu duni ila leo tulifurahi kumuona akiwa kwenye msiba wa Mama Aguu ila kitendo alichokifanya cha kubagua misiba kwa kutoa ahadi na mwingine kutoa fedha taslim kimeniumiza sana moyo wangu na sisi wananchi tunaona ni bora asingefika au asingetoa salaam za rambirambi.
Naye bwana Abdul ambaye ni dereva bodaboda amesema ni bora mbunge angetoa laki moja kwa mama Aguu na laki moja na nusu kwa Adam kuliko kitendo alichokifanya cha ubaguzi ambacho kimesikitisha waombolezaji na wananchi kwa ujumla.
Kwa upande wao ndugu wa marehem wa Mama Aguu wamesikitishwa na hizo taarifa na kusema wao wana muachia akiamua kutoa atoe pia akishindwa aache kwani aliahidi kwa hiari yake.
Mmoja wa wenyeviti wa mitaa katika kata hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema Moja ya changamoto kubwa ya mbunge ni kutokuhudhuria misiba na leo imekuwa ajabu kuonekana akizika kwani amekuwa akijinasibu kwenye vikao kuwa yeye sio mbunge wa kuzika ana majukumu mengi nadhani ndio maana amefanya jambo la ajabu leo ambalo kila mtu amebaki midomo wazi.
Utakumbuka kuwa imebaki miezi takribani 5 bunge kuvunjwa hivyo wabunge wengi ndio wanarudi kwa wananchi sasa baada ya kupotea na kutoonekana kwa zaidi ya miaka 4 hali inayopelekea wapiga kura wao kutokuwaelewa na kushangaa siku zote walikuwa wapi.
Credit. Kinyura News
UTANGULIZI
Katika hali isiyo ya kawaida Mbunge wa Moshi Mjini Mhe. Priscus Tarimo amekuwa gumzo katika mitaa mbalimbali ya Miembeni na Njoro baada ya kuhudhuria misiba miwili iliyokuwa jirani na kufanya jambo lililotafsiriwa kuwa sio la kiungwana.
Msiba wa kwanza ulikuwa maeneo ya Motherland kwa mama Aguu ambayo ni familia duni. Mhe. Mbunge alifika katika msiba huo na kupewa nafasi ya kutoa salaam sambamba na kutoa ahadi ya rambirambi ya shilingi laki moja (100,000/=)
Aidha baada ya hapo alielekea kwenye msiba kwa Adam Mamjombaa ni baba mlezi wa Mfanyabiashara maarufu mjini Moshi Nasib Gogo. Katika msiba huo alipata nafasi ya kutoa salaam na kutoa fedha taslim shilingi laki mbili na nusu. (250,000/=).
Kutoa 250,000/= taslim kwenye msiba wa watu wanaojiweza na kutoa ahadi ya 100,000/= kwa familia duni na inayohitaji msaada imetafsiriwa kuwa ni ubaguzi na unyanyapaa.
Akiongea kwa masikitiko makubwa mmoja wa waombolezaji mzee Hamis amesema ni nadra sana kwa Mbunge kuhudhuria misiba hasa ya watu duni ila leo tulifurahi kumuona akiwa kwenye msiba wa Mama Aguu ila kitendo alichokifanya cha kubagua misiba kwa kutoa ahadi na mwingine kutoa fedha taslim kimeniumiza sana moyo wangu na sisi wananchi tunaona ni bora asingefika au asingetoa salaam za rambirambi.
Naye bwana Abdul ambaye ni dereva bodaboda amesema ni bora mbunge angetoa laki moja kwa mama Aguu na laki moja na nusu kwa Adam kuliko kitendo alichokifanya cha ubaguzi ambacho kimesikitisha waombolezaji na wananchi kwa ujumla.
Kwa upande wao ndugu wa marehem wa Mama Aguu wamesikitishwa na hizo taarifa na kusema wao wana muachia akiamua kutoa atoe pia akishindwa aache kwani aliahidi kwa hiari yake.
Mmoja wa wenyeviti wa mitaa katika kata hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema Moja ya changamoto kubwa ya mbunge ni kutokuhudhuria misiba na leo imekuwa ajabu kuonekana akizika kwani amekuwa akijinasibu kwenye vikao kuwa yeye sio mbunge wa kuzika ana majukumu mengi nadhani ndio maana amefanya jambo la ajabu leo ambalo kila mtu amebaki midomo wazi.
Utakumbuka kuwa imebaki miezi takribani 5 bunge kuvunjwa hivyo wabunge wengi ndio wanarudi kwa wananchi sasa baada ya kupotea na kutoonekana kwa zaidi ya miaka 4 hali inayopelekea wapiga kura wao kutokuwaelewa na kushangaa siku zote walikuwa wapi.
Credit. Kinyura News