Mbunge wa Jubilee awasilisha muswada Mahakama ya Juu kumuondoa Jaji David Maraga aliyefuta matokeo ya Urais

Mbunge wa Jubilee awasilisha muswada Mahakama ya Juu kumuondoa Jaji David Maraga aliyefuta matokeo ya Urais

Kama Kuna kitu Wakenya wanachukia ni rais aliye na nguvu nyingi. Magufuli ni dictator na japo Wakenya wanampenda kwa kupunguza ufisadi, Wakenya hawawezi kuvumilia udikteta wa kukandamiza viombo vya habari na udikteta mwingi tu aliyonayo. Ana nguvu kupita kiasi na ndio maana T.Z mna Katiba useless kabisa na nyinyi mnashughulikiwa kama mahabusu. Hamuezi ongea, Hamuezi jitetea. Hata Chadema haikuenda mahakamani kwa sababu ya Katiba yenu iliyo na udikteta. Katiba yenu haiwatambui kama watu wenye haki bali kama mahabusu ambao hawaezi kujieleza. Hamna freedom of expression.
Sio kweli hayo unayosema, katiba yetu hii tunayoitumia sasa ilitungwa mwaka 1977, na kuanzia kipindi chote hich hadi leo Tanzania imeiacha kwa mbali sana Kenya katika kipengele cha demokrasia kwa viwango vya kimataifa(www.rsf.org), tangu dunia hii imeundwa hakuna hata mwaka mmoja ambapo takwimu za kimataifa zinaonyesha kwamba Kenya imeipita Tanzania katika demokrasia, hata baada ya Kenya kupata katiba mpya hiyo unayoisema inatoa demokrasia 2010, jaribu kupitia hiyo website niliyokupa hapo juu urudi miaka kumi nyuma utagundua huu ukweli ninaokuambia, ni kweli kwamba Magufuli anabinya kipengele cha freedom of political expression, lakini bado Tanzania ina uhuru zaidi katika maeneo mengine kuliko Kenya.

Kuhusu Kenya kuchukia zaidi kukosa uhuru wa kujieleza kuliko wanavyochukia Ukabila, rushwa, insecurity, kutokuwapo na usawa katika umilikaji wa ardhi, na kuwa na pengo kubwa kati ya matajiri na masikini, hilo ni chaguo la wakenya, hatuwezi kuwaingilia, ila sidhani kama wakenya wengi watakubaliana na wewe.

Kuhusu wapinzani kutokwenda mahakamani sio kwa sababu ya katiba, kumbuka hata NASA walishasema hawatoenda mahakamani kwa kuona kwamba wasingetendewa haki wakichukulia mfano wa hukumu ya uchaguzi wa mwaka 2013, walihisi hawakutendewa haki, sasa mbona Jubilee wanalalamika baada ya NASA kutumia haki yao ya kikatiba na mahakama kufanya kazi yake waliyopewa kwa mujibu wa katiba ya nchi?, tuseme hapo katiba ndiyo mbaya au ni watu kukosa imani na mahakama?
 
pengo lamasikini ni lazima na hata kwa bibilia yalikuwepo toka zaman. kenya wapo juu. watz, wengi tunataman sana kuwa wa kenya
Wewe ni maoni yako na hujazuiwa kwenda Kenya, na kuna wakenya wengi zaidi wanaotamani kuja Tanzania kuchangamkia fursa nyingi ambazo wewe huzioni, kuthibitisha hilo ni pale wakenya na serikali yao wanavyolalamikia serikali ya Tanzania kwa kuweka vikwazo kwa watu wengine wa nchi za EAC kuja Tanzania, wasingetamani kuja Tanzania wasingelalamika, Ethiopia imeweka vikwazo zaidi ya Tanzania lakini wakenya hawalalamikii Ethiopia kama wafanyavyo kwa Tanzania, jibu ni kwamba Tanzania ina fursa nyingi zaidi kuliko nchi zingine, wewe endelea kulalamika
 
Mbunge wa Jubilee nchini Kenya amewasilisha muswada katika Mahakama ya juu nchini humo kumuondoa madarakani Jaji Mkuu David Maraga aliyefuta matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo.

====================
A Jubilee MP has filed a petition seeking the removal of the Chief Justice over alleged gross misconduct following nullification of the presidential election results.


The Nyeri Town MP, Ngunjiri Wambugu, wants the Judicial Service Commission (JSC) to launch process to sack Chief Justice David Maraga for allegedly ‘orchestrating regime change’ plot over the nullification of President Uhuru Kenyatta’s win.

Speaking outside the Supreme Court after filing the petition before the JSC, Wambugu accused CJ Maraga of instituting a judicial coup by unduly influencing his fellow Supreme Court judges to nvalidate the re-election of President Uhuru Kenyatta.

The MP sensationally claims that CJ Maraga stopped Justice Mohamed Ibrahim from taking part in the NASA petition. Justice Ibrahim was taken ill during the NASA petition hearing and did not render a judgment on the case.


In his petition, Ngunjiri claims Maraga allowed civil activists opposed to the Jubilee government to fund the Judiciary through The International Development Law Organization (IDLO). Ngunjiri claims renowned legal scholar, Prof Makau Mutua, who is a vocal critic of President Kenyatta is an IDLO board member, an organization whose intent he claims is to subvert judicial independence.
Supreme Court ruling


On September 1, the Supreme Court nullified the re-election of President Kenyatta ruling that the electoral commission “failed, neglected, or refused to conduct the presidential election in a manner consistent with the dictates of the Constitution.”


Four Judges including the Chief Justice, Deputy Chief Justice Philomena Mwili, Smoking Wanjala and Isaac Lenaola invalidated the presidential election citing irregularities and illegalities in the transmission of results which was done manually and electronically.

However, Justices Njoki Ndung’u and JB Ojwang dissented. Justice Ibrahim did not deliver his judgment after having been taken ill on the second day of hearing.


Following the nullification of his win, President Kenyatta lashed out at the Supreme Court Judges calling them “wakoras” (thugs) but has since explained his outburst as “only human” at a meeting with Kisii leaders, the community from which Maraga comes from.


Kenyans are still eagerly waiting for the full Supreme Court judgement to understand the full basis on which the historic ruling was made. The judges have nine days to deliver the judgement.


Already, the electoral commission has set October 17 as the new date for the presidential election re-run even which the opposition NASA has threatened to boycott unless personnel changes are made at the Independent Electoral and Boundaries Commission are made, including the sacking of the chief executive officer Ezra Chiloba.


REACTIONS


Meru Senator Mithika Linturi (Jubilee) has distanced himself from Wambugu’s petition, saying the “independence of the Judiciary is not negotiable in terms of how they render judicial decisions.”


The petition has sent Kenyans on Twitter on spin pushing [HASHTAG]#MaragaPetition[/HASHTAG] top on Kenya trends.


Lawyer Donald Kipkorir termed the petition to remove Maraga for his fidelity to the Constitution “political terrorism.”


Source: Citizen Tv
Huu ni ujinga wa hali ya juu.If we keep up this corrosive culture of removing judges ,removing IEBC commissioners ,removing EACC heads ...believe me we will never achieve mature,professional and unduly influenced institutions.And this corrupting culture is coming from both sides of the political divide
 
katiba ya Kenya ilimtoa rais kabisa kwenye sector ya judiciary so the Kenyan president hana power ya kuteua au kumfuta kazi judge yeyote...rais hausiki kabisa kwenye idara ya judiciary, hiyo ni kazi ya judicial service commission
Na Judicial Service Commission hupatikana vipi kwa mujibu wa Katiba ya Kenya? Hv sio wateule wa Rais wale!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikweli Kenya sio Tanzania, katiba ya Kenya imepunguza nguvu sana za rais kiasi kwamba hawezi tena kupambana na rushwa, hawezi tena kupambana na mauaji holela yanayofanywa na vyombo vya dola, hawezi tena kupunguza insecurity kule Turkana na Mandera, hawezi tena japo kukemea ukabila uliotamalaki, hawezi tena kupambana na kuongezeka kwa pengo la masikini na matajiri, hawezi tena kushughulikia malalamiko ya ardhi katika jamii ya wakenya kama yalivyopendekezwa na tume ya wako, hiyo ndiyo katiba ya Kenya, kwahiyo kushindwa kwake kumuondoa CJ siojambo la msingi ukilinganisha na hayo mambo muhimu ambayo ninashangaa wakenya hawaoni mapungufu yake

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani Tanzania amna Mauaji akiri kisoda
 
Jubilee wanazidi kuleta aibu kila kuchao, ilihali hawajafanya chochote cha kusuruhisha matatizo ya vijana walio wengi napenda maendeleo ya jubilee lakini wakati huu mtanisamehe , sababu kura yangu hampati mara ya pili na simanishi nitawapa wapinzani lakini hio siku nitapumzisha mwili wangu nyumbani
 
Kwani Tanzania amna Mauaji akiri kisoda
Hakuna nchi isiyo na mauaji, ndiyo maana zimepangwa kwa madaraja, ukilinganisha Kenya na Tanzania katika mauji holela, Kenya ipo kiwango cha PhD na Tanzania ndiyo ipo mwaka wa kwanza kupata digirii ya kwanza
 
Huu ni ujinga wa hali ya juu.If we keep up this corrosive culture of removing judges ,removing IEBC commissioners ,removing EACC heads ...believe me we will never achieve mature,professional and unduly influenced institutions.And this corrupting culture is coming from both sides of the political divide
true dat
 
Hakuna nchi isiyo na mauaji, ndiyo maana zimepangwa kwa madaraja, ukilinganisha Kenya na Tanzania katika mauji holela, Kenya ipo kiwango cha PhD na Tanzania ndiyo ipo mwaka wa kwanza kupata digirii ya kwanza
Kwa mkondo mnaochukua mbona msifike tu? Hivi karibuni tz ndo mtakuwa mna PhD tatu tutaanza kuja darasani huko kwenu!
 
Jubilee wanazidi kuleta aibu kila kuchao, ilihali hawajafanya chochote cha kusuruhisha matatizo ya vijana walio wengi napenda maendeleo ya jubilee lakini wakati huu mtanisamehe , sababu kura yangu hampati mara ya pili na simanishi nitawapa wapinzani lakini hio siku nitapumzisha mwili wangu nyumbani
Utakuwa umefanya jambo lisilo la hekima jombaa, we siku ya kupiga kura amka mapema maliza jukumu lako kwa nchi yako afu nenda kapumzike. Tupia U.Kenyatta kura aisee we mwenyewe si unaona alivyo jaribu hiyo miaka minne?
 
Kwa mkondo mnaochukua mbona msifike tu? Hivi karibuni tz ndo mtakuwa mna PhD tatu tutaanza kuja darasani huko kwenu!
Sijambo la kulipinga hilo, kama hali itaendelea hivi hivi ilivyo tunaweza kuwafikia Kenya, ila lakushanga sijui Kenya hawapendi tuwafikie?, kwasabu wanaongeza kasi kila uchao[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Jubilee wanazidi kuleta aibu kila kuchao, ilihali hawajafanya chochote cha kusuruhisha matatizo ya vijana walio wengi napenda maendeleo ya jubilee lakini wakati huu mtanisamehe , sababu kura yangu hampati mara ya pili na simanishi nitawapa wapinzani lakini hio siku nitapumzisha mwili wangu nyumbani
Sasa io petition inahusiana vipi na jubilee?
 
Nikweli Kenya sio Tanzania, katiba ya Kenya imepunguza nguvu sana za rais kiasi kwamba hawezi tena kupambana na rushwa, hawezi tena kupambana na mauaji holela yanayofanywa na vyombo vya dola, hawezi tena kupunguza insecurity kule Turkana na Mandera, hawezi tena japo kukemea ukabila uliotamalaki, hawezi tena kupambana na kuongezeka kwa pengo la masikini na matajiri, hawezi tena kushughulikia malalamiko ya ardhi katika jamii ya wakenya kama yalivyopendekezwa na tume ya wako, hiyo ndiyo katiba ya Kenya, kwahiyo kushindwa kwake kumuondoa CJ siojambo la msingi ukilinganisha na hayo mambo muhimu ambayo ninashangaa wakenya hawaoni mapungufu yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Na wewe huoni mapungufu ya hoja yako ambapo una upotevu zaidi.Ni vizuri Kenya tumeweka nguvu kwa tume ambapo kuna "panel of experts" kuamua nani anayefaa kwa kazi tofauti yaani we invest in institutions not individuals.Hata Obama alipozuru Ghana alisema "Africa should invest in istitutions and not strongmen" sababu madikteta ndio wameharibu Afrika zaidi na uamuzi mbaya,utawala mbaya na kutojali au kujenga "rule of law" .Strongmen don't last ,but good decisions made by healthy institutions have a lasting legacy.
 
Na wewe huoni mapungufu ya hoja yako ambapo una upotevu zaidi.Ni vizuri Kenya tumeweka nguvu kwa tume ambapo kuna "panel of experts" kuamua nani anayefaa kwa kazi tofauti yaani we invest in institutions not individuals.Hata Obama alipozuru Ghana alisema "Africa should invest in istitutions and not strongmen" sababu madikteta ndio wameharibu Afrika zaidi na uamuzi mbaya,utawala mbaya na kutojali au kujenga "rule of law" .Strongmen don't last ,but good decisions made by healthy institutions have a lasting legacy.
Katiba nzuri ni ile inayotoa ufumbuzi wa matatizo yanayowakumba wananchi wa kawaida, ni ile ambayo itamuinua wananchi walio wengi hasa wale masikini. Matatizo ya msingi yanayozikabili jamii zetu hizi za afrika ni umasikini, ukosefu wa ajira, uhakika wa chakula, usalama, rushwa, matumizi mabaya ya fedha za uma na uzembe na matumizi mabaya ya ofisi za umma, hayo ndiyo hasa tunataka yapatiwe ufumbuzi kwamba, kabla hata hayo mambo ya kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani, kwani hayo hayana tija ya moja kwa moja kwa mwananchi wa chini.

Kinachojitokeza ni kwamba katiba ya Kenya imelenga zaidi kuwasaidia wanasiasa wasidhulimiwe kura zao, kuliko kutoa ufumbuzi wa matatizo ya wananchi wa chini masikini, kwa sababu tangu katiba hii ipatikane takribani miaka saba sasa hivi, rushwa ndiyo imeongezeka zaidi, ukosefu wa ajira ndiyo unazidi, usalama nchini ndiyo unazidi kuzorota, ugumu wa maisha ndiyo usisemi kitu, ukabila unakita mizizi, yaani yale matatizo ya wakenya masikini ndiyo yanaongezeka, lakini utasikia watu wakiisifia katiba, kwa sababu tu inatoa fursa nzuri kwa wanasiasa kufanya siasa wakiwa huru zaidi, basi katiba hii ni nzuri kwa wanasiasa lakini haimsaidii mwananchi wa kawaida
 
Back
Top Bottom