CCM = Chama Cha M........... ulikuwa hujui tu!.Hiyo itakua ilipangwa ili asiwe bungeni wakati taarifa ya serikali kuhusu gharama za visimbusi inawakilishwa asikuwepo kuhoji.Spika anatoa report ati kaavamiwa na majambazi,mmmm CCM wamekua majambazi sasa
atakuwa amejipiga ili apate kura za huruma....
Mungu yupi??????Pole sana jembe mungu yuko na ww
Mungu yupi??????
Pinda ameruhusu ni kufanyiana timing sasa
Hata mimi nahisi hivyo hivyo.Du isije ikwa ndo utekelezaji wa Agiza la Pinda, Kumbukeni usikuule wa kutekwa kwa Dr. Ulimboka alisema "Liwalo na liwe"
Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.
Heshima yoyote wewe ndiyo unayempa kichwa aonekane ana heshima,watu wengine waliisha mgundua siku nyingi.Mkuu,
Wewe ni mtu mwenye heshima sana hata kama unatumia ID nyingi. Kupotosha mambo kwa makusudi kwa staili hii kunakupunguzia heshima na credibility. Hiyo kauli machali hakuitoa, vinginevyo niletee hansard ya Bunge.
Kama umona mimi nina ushetani,basi nakukabidhi kwa shetani akushughulikie.Toka lini ukamjua MUNGU?, endelea na ushetani wako.
JUNE 20, 2013
Habari zilizoifikia Maisha Times muda huu kutoka Dodoma zinaripoti kwamba Mbunge wa Kasulu mjini kupitia tiketi ya Chama cha NCCR Mh. Moses Machalli amevamiwa na kupigwa na watu wasiojulikana katika eneo la, tukio hilo limetokea jioni hii wakati Mh. Machalli akiendesha gari lake mita kadhaa kutoka ilipo nyumba anayoishi baada ya kuwapigia honi vijana kadhaa waliokuwa wakitembea katikati ya barabara ili wasogee pembeni naye aweze kupita kitendo ambacho kilionekana kuwaudhi na kuwakera vijana hao ambao walianza kuipiga na kuigonga kwa nguvu bodi ya gari ya Mh. Machalli jambo ambalo lilimfanya Machalli kusimamisha gari na kushuka ili kujua kulikoni hali iliyopelekea vijana hao kumtolea matusi kadhaa ya nguoni na pindi machalli alipowajibu kwa hasira ndipo kipigo kikali kilipoanzia.
Shuhuda wetu aliyekuwa jirani na eneo la tukio anasema kwamba Mh. Machalli amepigwa na vijana zaidi ya nane jambo ambalo lilipelekea hata yeye kushindwa kumsaidia kwa kuhofia kuunganishwa katika kipigo.
Maisha Times itazidi kukuhabarisha zaidi kuhusiana na tukio hili kadiri habari zitakavyozidi kupatikana.
Imechapishwa na Mkamis
Tuanze na wenye mgogoro na bwana Machali ili tuweze kuwabaini mapema wahusika wa hilo tukio.
Kumbukumbu zangu; mchango wa mwisho wa bwana Machali bungeni ulikuwa ukiitaka serikali ichunguze suala la Arusha, na kama CHADEMA ikibainika imehusika basi kifutwe haraka sana.
Je, CHADEMA na kichapo alichopata Machali vina mahusiano?