Mbunge wa Kawe Askofu Gwajima ataka Masheikh wa Uamsho waachiwe na Sheria za uhujumu uchumi zirekebishwe

Mbunge wa Kawe Askofu Gwajima ataka Masheikh wa Uamsho waachiwe na Sheria za uhujumu uchumi zirekebishwe

Course Coordinator

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2019
Posts
1,742
Reaction score
3,224
Mimi siongezi neno hapa

Mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima amelishauri Bunge kuwa Sheria kandamizi zilizotungwa mwaka 2019 ikiwemo Sheria ya Uhujumu Uchumi na Utakatishaji fedha zifanyiwe Marekebisho kwani kuna Maelfu ya watu Wamebambikiwa kesi hizo mpaka sasa Wanasota Mahabusu bila kujua hatma yao.

Aidha, Gwajima amesema haoni sababu ya Masheikh wa UAMSHO kuendelea kusota Mahabusu kwa miaka 9 bila kujua hatma yao

"Kuna Masheikh wa Uamsho wapo Mahabusu mwaka wa 9 sasa, hebu imagine ni Baba yako anasota Mahabusu kwa miaka 9 bila kujua atahukumiwa lini na vipi ikibainika hawana hatia mtawalipa nini?. Simaanishi hawana hatia au wanayo nashauri ni vyema wahukumiwe wajue moja.

Arusha kuna Masheikh 64 wanasota Mahabusu kwa kesi ya Ugaidi, najiuliza hivi hii nchi Magaidi ni Masheikh tu Hakuna watu wengine"Josephat Gwajima.

Ahsante Gwajima kwa kuliona hili.
 
Mashehe walifungwa na Magufuli?

..mbona Magufuli aliwatoa babu seya na papii waliokuwa wamehukumiwa kwa kulawiti watoto wa shule?

..je, babu seya na papii alifungwa na magufuli?

..je, walawiti watoto wa shule waliopatikana na hatia ni bora kuliko mashekhe ambao hawajapatikana na hatia na uchunguzi wa tuhuma dhidi yao umekwama?

Cc tindo
 
Hao jamaa serikali kuwashikilia bila kuwafikisha mahakamani ni kama kuwaogopa, wanaogopa sheria inaweza kuwaachia huru watu ambao ni "threat" kwenye jamii.

Aina ya mahubiri waliyokuwa wanayafanya ndio inayowagarimu, na hili limesababisha hata marais "wenzao" wasiwaachie huru. Tuliona watu wakimwagiwa tindikali bcoz of them, na walipokamatwa hali ikatulia.
 
Back
Top Bottom