Mbunge wa Kawe Askofu Gwajima ataka Masheikh wa Uamsho waachiwe na Sheria za uhujumu uchumi zirekebishwe

Gwajima hajui kitu kuhusu ugaidi atulie tu mashekhe waonje hatma yao
 
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Mchungaji Dkt. Josephat Gwajima, amesema, kuna idadi kubwa ya watu wako mahabusu kutokana na suala la utakatishaji wa fedha ambao wako waliobambikiziwa kosa hilo na watumishi wasio waaminifu wa vyombo vya dola na kuomba suala hilo liangaliwe kwa kina.

"Kuna watu wengi sana Naibu Spika wako ndani, wako mahabusu maelfu ya watu kwa sababu ya hili suala la utakatishaji fedha kubambikiziwa na watu wasio waaminifu katika vyombo vyetu vya Dola"

"Mpaka leo kwa mujibu wa takwimu kuna watu 1,701 ambao wako mahabusu kwa sababu ya ama kwa ajili ya utakatishaji fedha Money laundering au kwa sababu ya uhujumu uchumi"

"Unakuta mtu anakwenda kwa mfanyabiashara kukusanya mapato au kudai mapato au malimbikizo ya mapato anakwenda na 'charge' kabisa kwamba usiponipa fedha kadhaa tayari nina hati hii hapa nakuwekea Money laundering au nakuwekea Economic Sabotage"

"Haileti "sense" kwanini wale Masheikh wa uamsho wako ndani mpaka leo, leo ni miaka 9. Najaribu kuwaza ingekuwa mimi, Baba au ndugu yangu ambaye ambaye mpaka leo miaka 9 yupo ndani, itakuwaje baada ya miaka 20 mkagundua hawana hatia mtawalipa nini kwa miaka waliyopoteza"

"Nashangaa kwanini Masheikh tu ndio wako ndani kwa kesi za ugaidi, hakuna gaidi mwingine ambaye sio sheikh, naomba tuangalie kwa undani sana namna ya ku-handle suala hili, sisemi wana hatia au hawana hatia, sijadili kosa lao lakini basi wangehukumiwa ikajulikana"
 
Safi sana askofu rashidi
 
Gwajima mara hii kasha sahau viongozi wenzake (wakristo) waliokuwa wakipigwa risasi, makanisa kuchomwa na kutupiwa mabomu Zanzibar, Arusha, Dar, Kagera, nakadhalika
 
Nashangaa kwanini Masheikh tu ndio wako ndani kwa kesi za ugaidi, hakuna gaidi mwingine ambaye sio sheikh, naomba tuangalie kwa undani sana namna ya ku-handle suala hili, sisemi wana hatia au hawana hatia, sijadili kosa lao lakini basi wangehukumiwa ikajulikana"[emoji1541][emoji1541][emoji1541]
Kinyonga katika ubora wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…