The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Ikiwa ni msimu wa sita kwa Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Akson kugawa bima na mahitaji muhimu kwa kaya 1500 sawa na wazee 9000 wa Jiji la Mbeya, Dr Tulia amewataka wenyeviti wa mitaa ya Halmashauri ya Mbeya kuendelea kuwaibua wenye uhitaji ili wasaidiwe na taasisi hiyo pamoja na wadau mbalimbali.
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mbeya Juma Zubeir Homera amemshukuru Mkurugenzi wa Tulia Trust Dkt Tulia Ackson kwa kuziunganisha wilaya zote za Mkoa wa Mbeya kwa kuwapatia misaada kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba watu wenye mahitaji maalumu.
Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hata hivyo baadhi ya viongozi akiwemo Chifu wa Mkoa wa Mbeya Rocket Mwashinga na Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Kefas Mwasote wameeleza namna Dkt Tulia anavyowapambania na kuwathamini wakazi wa Mbeya.
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mbeya Juma Zubeir Homera amemshukuru Mkurugenzi wa Tulia Trust Dkt Tulia Ackson kwa kuziunganisha wilaya zote za Mkoa wa Mbeya kwa kuwapatia misaada kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba watu wenye mahitaji maalumu.
Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hata hivyo baadhi ya viongozi akiwemo Chifu wa Mkoa wa Mbeya Rocket Mwashinga na Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Kefas Mwasote wameeleza namna Dkt Tulia anavyowapambania na kuwathamini wakazi wa Mbeya.