Pre GE2025 Mbunge wa Mbeya mjini Tulia Akson agawa Bima za Afya kwa Wananchi 9000

Pre GE2025 Mbunge wa Mbeya mjini Tulia Akson agawa Bima za Afya kwa Wananchi 9000

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Ikiwa ni msimu wa sita kwa Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Akson kugawa bima na mahitaji muhimu kwa kaya 1500 sawa na wazee 9000 wa Jiji la Mbeya, Dr Tulia amewataka wenyeviti wa mitaa ya Halmashauri ya Mbeya kuendelea kuwaibua wenye uhitaji ili wasaidiwe na taasisi hiyo pamoja na wadau mbalimbali.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mbeya Juma Zubeir Homera amemshukuru Mkurugenzi wa Tulia Trust Dkt Tulia Ackson kwa kuziunganisha wilaya zote za Mkoa wa Mbeya kwa kuwapatia misaada kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba watu wenye mahitaji maalumu.

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Hata hivyo baadhi ya viongozi akiwemo Chifu wa Mkoa wa Mbeya Rocket Mwashinga na Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Kefas Mwasote wameeleza namna Dkt Tulia anavyowapambania na kuwathamini wakazi wa Mbeya.

 
Nadhani kati ya wabunge wenye hali ngumu jimboni ni huyu Mmama. Anajua fika Sugu alipata umaarufu kabla yake.. Na alianza harakati akifanya mziki kama kazi. Halafu pia jinsi ina msumbua anaona wazi kupambana na kidume ujipange.. Ashukuru ni spika.. Unless ataangukia pua..
 
Nadhani kati ya wabunge wenye hali ngumu jimboni ni huyu Mmama. Anajua fika Sugu alipata umaarufu kabla yake.. Na alianza harakati akifanya mziki kama kazi. Halafu pia jinsi ina msumbua anaona wazi kupambana na kidume ujipange.. Ashukuru ni spika.. Unless ataangukia pua..
Hv sugu na akson nani yupo karibu zaidi kuleta maendeleo Mbeya?
nadhani ni Akson huo ndio ukweli. Sugu fisiemu watamnyima hela za maendeleo
 
Je! Kama siyo rushwa ni nini?
Je! Ni zawadi ama?
Je! Pesa ni yake binafsi ?
Je! Pesa ya ofisi ya bunge?
Je!pesa ya ofisi ya mbunge?
Je! Pesa hizo ni za umma?
 
Hv sugu na akson nani yupo karibu zaidi kuleta maendeleo Mbeya?
nadhani ni Akson huo ndio ukweli. Sugu fisiemu watamnyima hela za maendeleo
Imefikia hatua sasa haki ya jimbo inaonekana kama ni hisani toka kwa serikali, mambo ya hovyo sana
 
Hv sugu na akson nani yupo karibu zaidi kuleta maendeleo Mbeya?
nadhani ni Akson huo ndio ukweli. Sugu fisiemu watamnyima hela za maendeleo
Hujui kitu, Sugu alishajisalimisha ccm muda mrefu tu, na hana uwezo wa kupambana na tulia ackson, hata sugu mwenyewe analitambua hilo
 
Hv sugu na akson nani yupo karibu zaidi kuleta maendeleo Mbeya?
nadhani ni Akson huo ndio ukweli. Sugu fisiemu watamnyima hela za maendeleo
Mkuu wapi nimeandika Maendeleo!! Hoja yangu imejikita kwenye umaarufu ambao ndiyo nyenzo ya kwanza ya ushindi.. Soma uelewe kwanza...
 
Watengemeze mfumo wa kiserikali kwa wananchi wote na sio ku select wachache kisiasa
 
Back
Top Bottom