Pre GE2025 Mbunge wa Rorya, Jafari Chege amewawetaka wananchi wa Kata hizo kutambua dira ya maendeleo tangu walipokuwa, walipo sasa na wanakoelekea

Pre GE2025 Mbunge wa Rorya, Jafari Chege amewawetaka wananchi wa Kata hizo kutambua dira ya maendeleo tangu walipokuwa, walipo sasa na wanakoelekea

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Akizungumza na wananchi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM katika Kata 3 za Nyamagaro kyang'asaro na Nyamtinga, Mbunge wa Jimbo la Rorya, Jafari Chege amewawetaka wananchi wa Kata hizo kutambua dira ya maendeleo tangu walipokuwa, walipo sasa na wanakoelekea.

Chege ameendelea kuwapa ushirikiano wananchi wa Rorya na kuwaahidi makubwa kwani bado ana uwezo wa kuwahudumia na kuwatumikia wakazi wa jimbo lake kwani maendeleo ndio kipaumbele chake.

"Tunatambua umuhimu wa maendeleo na miradi mingi ya kimakakati inayoletwa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili yetu sisi wana Rorya hivyo tunapaswa kushukuru kwa kila hatua tunayopiga kwenda mbele kimaendeleo" Amesema Mbunge Chege

Source: Clouds Tv

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Back
Top Bottom