Mbunge wa Sumve, Kasalali Kasalali Mageni: Mawaziri wanatupa ahadi hewa tu, Wananchi wa Sumve hatuna lami hata Mita moja

Mbunge wa Sumve, Kasalali Kasalali Mageni: Mawaziri wanatupa ahadi hewa tu, Wananchi wa Sumve hatuna lami hata Mita moja

DodomaTZ

Member
Joined
May 20, 2022
Posts
84
Reaction score
118

Mbunge wa Sumve, Kasalali Mageni amechangia Bungeni Jijini Dodoma, leo April 4,2024 ambapo katika mchango wake amemuomba Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuzungumza na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa kutekeleza majukumu yao ya kuwezesha suala la maendeleo ya kujengwa Barabara ya lami katika jimbo lake Sumve.

Kasalali amesema kuwa Wananchi wa jimbo lake wanachotaka kwa sasa ni suala la barabara ya lami na sio jambo lingine.

Kasalali amesema ameshajaribu kuzungumza na mawaziri hao lakini bado wamekuwa wakimpa maneno mengi bila kuwa na utekelezaji jambo hilo.
 
Jinga kabisa, miaka 4 alikuwa kimya. Si hawa waliokuwa wanasema hapa kazi, mama anaupiga .
Leo analalamika nini
 
Mwanza hatuna wabunge, Wamekaa tu wanajali maslahi yao. Barabara ya Kitangiri kwenda Mihama inahitaji Lami, ni mbovu haina mfano. Mvua zikinyesha tu haipitiki na ni mjini Kabisa.
 
Hapo ndio kazi ilipo. Umedanganywa ukidanya, mbaya niwewe uliedanhanywa
 
Back
Top Bottom