Pre GE2025 Mbunge wa Ushetu apiga magoti kuomba maji ya ziwa Victoria. Waziri amjibu "Samia ametoa pesa mkandarasi anakuja"

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kupiga Magoti na kuogelea kwenye mavi ya kuku kipi Bora? Na Kwa pesa gani? πŸ˜‚πŸ˜‚
Binafsi siwezi kujishusha kiasi hicho, katika vitu ambavyo nilishawahi kugoma hata kipindi nipo shule ni kupigishwa magoti, nilikuwa tayari nipewe adhabu hata ya kuchapwa viboko lakini si kupiga magoti hadharani.
 
Kiufupi anaupiga mwingi sana.

Ujinga ni kudhani Mama anaweza maliza matatizo yenu yaliyowashinda Kwa miaka zaidi ya 60 ndani ya miaka 4.
Hilo ni lako mimi naona hajafanya chochote zaidi ya kuimbiwa nyimbo ambazo yeye hazipendi kuzisikia maana anajua anaingizwa chaka na machawa ili hali ana kazi kubwa mbeleni!
 
Hilo ni lako mimi naona hajafanya chochote zaidi ya kuimbiwa nyimbo ambazo yeye hazipendi kuzisikia maana anajua anaingizwa chaka na machawa ili hali ana kazi kubwa mbeleni!
Sasa chuki zako binafsi Wala hazimzuii Samia kuchanja mbugha.

Kwa taarifa Yako tuu hakuna Rais anaweza mfikia Samia kwenye delivery Kwa sekta zozote unazozijua wewe hapa Tanzania Kwa mda miaka 3 hii amekuwa game changer across sectors

View: https://www.instagram.com/p/C14tp1po_de/?igsh=dmdpMmwxOGttcDhk
 
Siasa ngumu sana! Yaani Mwanaume kabisa, tena Mbunge anapiga Magoti ili kuomba kitu! Huko ni kujidhalilisha na kujishusha thamani, Wapiga kura wake lazima wamdharau kwa hilo.
Ukiwa na akili timamu na kujaa aibu,na kujiongeza thamani utasikia tu mbunge alipwa milioni 12 .Siasa ndio mchezo wake jitoe akili unufaike
 
Mbona neno chuki unalipenda sana unaakisi udhaifu wako ulipo dunia hii ukweli unakuweka wazi kuchanganua vitu sio lazima wote wafuate mkumbo wako hata kama unawaingiza chaka!
 
Mbona neno chuki unalipenda sana unaakisi udhaifu wako ulipo dunia hii ukweli unakuweka wazi kuchanganua vitu sio lazima wote wafuate mkumbo wako hata kama unawaingiza chaka!
Wewe ni hater ,wewe huoni unachoandika? Unaona kina uhalisia?
 
Mbunge wa Jimbo la Ushetu Emmanuel Cherehani Mkoani Shinyanga amemuangukia Waziri wa Maji Jumaa Aweso akimuomba maji kwani Amesema Wilaya Majimbo yaote ya Mkoa wa Shinyanga yamefikiwa na Mji ya kutoka Ziwa Victoria isipokuwa Jimbo lake.
ni kujiaibisha, huyu ni Mbunge kweli ama wale wale feki walipitishwa kwa mkondo wa jiwe. Serikali ndiyo inakusanya kodi na inawajibika kuwapa wananchi wake maji wala si hisani ya Rais.
 
Hizi tabia za viongozi kupiga magoti ni ushamba uliopitiliza. Ni sanaa ya kitoto ya kutafuta huruma ya wananchi..!
 
Ninapendekeza uwepo uzi maalum wa yanayojiri kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani
 
Siasa ngumu sana! Yaani Mwanaume kabisa, tena Mbunge anapiga Magoti ili kuomba kitu! Huko ni kujidhalilisha na kujishusha thamani, Wapiga kura wake lazima wamdharau kwa hilo.
Mwanaume wa kanda ya ziwa kufanya hivi kwa kweli sijamuelewa.
 
Siasa ngumu sana! Yaani Mwanaume kabisa, tena Mbunge anapiga Magoti ili kuomba kitu! Huko ni kujidhalilisha na kujishusha thamani, Wapiga kura wake lazima wamdharau kwa hilo.
Maboya sana haya .yana wana siasa wa kiume wanavyo nyenyekea ili bidi wavalishwe Madela wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…