Mbunge wa viti maalumu CHADEMA, Sabriana Sungura ahamia CUF

Mbunge wa viti maalumu CHADEMA, Sabriana Sungura ahamia CUF

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1590850276916.png


Mbunge wa Viti maalumu Kigoma, Sabriana Sungura ameambatana sambamba na aliyekuwa Mbunge wa Bukoba Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Wilfred Rwakatale kuhamia chama cha Wananchi CUF.

Aidha, katika katika shamrashamra za Wabunge hao kupokelewa katika Chama cha CUF, Mh. Sabriana Sungura amesema ameamua kujiunga na chama hicho kwa lengo kupata haki sawa na furaha baada ya kuikosa kwa muda mrefu katika Chama Cha Demokrasia na Maendeleo,CHADEMA.

Amesem, katika chama hakukuwa na haki wala furaha badala yake kilitawaliwa na ubinafsi pamoja umimi.

” Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimetawaliwa na ubinafsi pamoja na umimi,kwani baada ya kufunga ndoa na mtu anayetoka katika Chama Cha Wananchi CUF nilinuniwa pamoja na kutegwa kwa madai kuwa natoa siri za chama,”amesema Sabrina.

Amesema kuwa, baada ya kuona hayo moja kwa moja kwa imani yake aliona jambo hilo ni la ubinafsi na kuamua kutazama pembeni.

Naye, Makamu Nwenyekiti wa CUF Bara, Maftah Nachuma, amesema chama hicho kimejipanga kuhakikisha kinashika dola pamoja na kurudisha heshima iliyokuwepo awali.

Amesema,ujio wa wabunge hao ni mzuri na umelenga kukifikisha Chama Cha CUF mbali kwa kuhakikisha itikadi ya haki sawa kwa wote inatekelezwa.

“Chama Cha CUF kimezaliwa upya Sasa kwa pamoja tunashiriki na kusimama imara kuhakikisha chama kinasonga mbele,”amesema Nachuma.

PIA SOMA - Wilfred Lwakatare arejea CUF baada ya kufutwa uanachama CHADEMA. Kutumika kuiangamiza CHADEMA
 
Huyu dada anafanana na Dr Sungura mkurugenzi wa vyombo vya habari vya CCM!
 
Hivi CDM ina siri gani hasa? Za kuua watu au mipango ya uasi?

Na zinaendeleaje kuwa siri kama kila mwanachama anazo?

Maana hadi diwani unakuta anatuhumiwa kuvujisha siri za chama!How?

Mke wa Kafulila kwa hali hii yupo mguu ndani mguu nje.
 
Hivi CDM ina siri gani hasa? Za kuua watu au mipango ya uasi?

Na zinaendeleaje kuwa siri kama kila mwanachama anazo?

Maana hadi diwani unakuta anatuhumiwa kuvujisha siri za chama!How?

Mke wa Kafulila kwa hali hii yupo mguu ndani mguu nje.
Kiongozi gani wa Chama aliwahi kusimama akasema diwani fulani anavujisha siri za chama?

Wewe sio kada haupo kwenye kamati kuu za chama siri za chama utazijulia wapi?
Jesca Kishoa yupo kama pambo tu jimboni kwake kule mwigulu hawezi kumtoa, hata akihama sawa tu hakuna anayejali
 
CCM wanachekesha sana,baada ya kuona watu wamewashtukia wananunua upinzani wakaamua kuwafanyia shopping NCCR,baada ya watu pia kushtukia NCCR ni mpango wa kando wameamua sasa hivi kuwanunua na kuwahamishia CUF.

Hongera CCM,sasa hivi mmekuwa na wake watatu ,CUF,NCCR na TLP.

CUF ni mke mkubwa wakati wowote yupo hata umtende ,TLP ni mke wa pili,hapendwi ila analazimisha mapenzi ,mke mdogo ni NCCR mageuzi kwa sasa mapenzi yapo on fire
 
Kiongozi gani wa Chama aliwahi kusimama akasema diwani fulani anavujisha siri za chama?

Wewe sio kada haupo kwenye kamati kuu za chama siri za chama utazijulia wapi?

Diwani wa Sombetini Ally Bananga anatuhumiwa na Godbless Lema kutoa siri za chama kutokana na urafiki wake na Msando.

Kwa hiyo mlinzi wa Dr Slaa bwana Khalid Kagenzi alikuwa anaingia kwenye kamati kuu za chama?

Au haujui kilichompata kwa tuhuma hizo hizo?
 
CCM wanachekesha sana,baada ya kuona watu wamewashtukia wananunua upinzani wakaamua kuwafanyia shopping NCCR,baada ya watu pia kushtukia NCCR ni mpango wa kando wameamua sasa hivi kuwanunua na kuwahamishia CUF.

Hongera CCM,sasa hivi mmekuwa na wake watatu ,CUF,NCCR na TLP.

CUF ni mke mkubwa wakati wowote yupo hata umtende ,TLP ni mke wa pili,hapendwi ila analazimisha mapenzi ,mke mdogo ni NCCR mageuzi kwa sasa mapenzi yapo on fire
Anayetoa shutuma anatakiwa athibitishe. Tupe picha au clip ya sauti watu wakinunuliwa. Nyie ndio huwa mnafungwa.
 
NCCR+ACT+CUF+CHAUMA =N.A.C.C

Chadema modern taarab itaendelea kuwa bendi ya mipasho.
 
CCM wanachekesha sana,baada ya kuona watu wamewashtukia wananunua upinzani wakaamua kuwafanyia shopping NCCR,baada ya watu pia kushtukia NCCR ni mpango wa kando wameamua sasa hivi kuwanunua na kuwahamishia CUF.

Hongera CCM,sasa hivi mmekuwa na wake watatu ,CUF,NCCR na TLP.

CUF ni mke mkubwa wakati wowote yupo hata umtende ,TLP ni mke wa pili,hapendwi ila analazimisha mapenzi ,mke mdogo ni NCCR mageuzi kwa sasa mapenzi yapo on fire
Yeah,
Wako kwa Mkopo kwenye hivyo vyama.
 
Diwani wa Sombetini Ally Bananga anatuhumiwa na Godbless Lema kutoa siri za chama kutokana na urafiki wake na Msando.

Kwa hiyo mlinzi wa Dr Slaa bwana Khalid Kagenzi alikuwa anaingia kwenye kamati kuu za chama?

Au haujui kilichompata kwa tuhuma hizo hizo?
Thibitisha madai yako Sir
 
Hana madhara...
Miaka yote nyumba Togo ilikuwa ofisi ya bavicha walikodi mnyika Kuingia akawa hamisha bavicha kwenye jengo lao
Ila ashukuru kwa kupata mjengo wake na akishukuru
Chama pia kwa kumbeba maana alikuwa hana A wala B....

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Nimeisikiliza hii video hadi machozi yanenitoka kwa huu unyanyasaji unaofanyika huko chadema,huyu Dada ni mbunge viti maalumu,anaitwa Sabrina Hamza Sungura toka kigoma,anadai chadema na uongozi wa juu umevuruga ndoa yake,Serikali yangu tukufu naiomba iingilie kati swala hili La chadema kuwanyanyasa wabunge wa kike,ikiwezekana. Mwenyekiti afunguliwe mashitaka ya uchanyanyasaji wa kijinsia


Video hii hapa >>

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom