Pre GE2025 Mbunge yeyote anayerudi jimboni leo miaka zaidi ya 5 imepita kutembelea jimbo asichaguliwe tena

Pre GE2025 Mbunge yeyote anayerudi jimboni leo miaka zaidi ya 5 imepita kutembelea jimbo asichaguliwe tena

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni njia ipi sahihi ya kumuondoa Mbunge ambae hajafanya chochote bungeni kwake zaidi ya miaka 5 imepita?

Je ni kura ya maoni?
 
1720882596536.png

Katika sababu hizo tatu wananchi wana muda wa kuwafikiria wagombea ubunge wao kwa kuangalia sababu ya tatu (Issue Voting)yaani masuala ya kupiga kura kulingana na sababu mbalimbali ikiwemo mbunge amefanya nini bungeni.

Hiyo ni kwasababu tayari wananchi (kwenye factors mbili za mwanzo) wana ukaribu mno na chama cha mgombea au binafsi wanamhusudu hivyo hata kwa mabaya yake.

Hilo ndo la kuliondoa.
 
View attachment 3041433


Mbunge Damas Ndumbaro karudi jimboni kwake Songea leo kuwasalimia wananchi wake miaka mingi imepita tangu achaguliwe ubunge.

Mbunge huyu katoa zawadi, kaongozana na wataalam na watu wengine wengi tu muda alowakusanya haujulikani akiwa na msafara wa magari yasozidi 10!

Je, Mbunge huyu aweza kutatua tatizo lolote jimboni kwake miezi zaidi ya mwaka imebakia ufanyike uchaguzi mkuu ujao wa 2025?

Jimbo lake la Songea Mjini halina barabara za lami na pia kata ya Mletele hadi Mdundiko hakuna maji , je wananchi hawa wamekuwa wakioga wapi, kutawadha wapi na kunywa maji yepi?

Pia tatizo la barabara limewafanya wananchi wawe na wakishindia pombe kwa kukosa shughuli za kufanya za kiuchumi (mobility issues) jambo linodumaza maendeleo ya jimbo hilo.

Mbunge Damas Ndumaro hafaikabisa kuendelea kuwa mbungewa jimbo hilo baada ya miaka migni kupita jimbo halina maji wala barabara nzuri ya lami. Na kutoa kiasi cha fedha 500k hakutasaidia chochote kukamilisha utandazaji wa bomba la maji kutoka Mdundiko hadi Mletele.

Wananchi wana haki ya msingi kabisa ya kutomchagua mbunge huyo na badala yake wachague watu mbadala na kama hawapo basi wananchi hao wasipige kura.

Je, ni Makonda na Silaa ndo walowakumbusha wabunge kama Ndumbalo kuanza kwenda majimboni kwao kusikiliza shida za wananchi wao walowachagua miaka minne au mitano ilipita?

Chondechonde wananchi tuamke mbunge anapoingia jimboni kuanzia sasa hivi na hajafanya chochote basi asichaguliwe ili kuwafunza wabunge hao kwamba wanawajibika kuwepo bungeni kila mara.

Pia kuanzia sasa ni vema wabunge wote wakawa na ofisi (surgery) kwa ajili ya kuonana na wananchi wao wenye shida na matatizo mbalimbali.

Na fedha za kujengea ofisi zao zitokane na malipo yao wenyewe ambayo hukunja na kubakia nje ya majimbo yao.
Kazi ya mbuzi ni kuchagua mbuzi mwenzao hivyo usishangae wakimchagua.
 
Wangoni na ccm ni kama samaki na maji. Huwambii kitu.
Sijui kama watakuelewa.
 
Wangoni na ccm ni kama samaki na maji. Huwambii kitu.
Sijui kama watakuelewa.
Tena kukiwa na shughuli huhamia mjini kutoka majumbani mwao.

Kazi kwelikweli, lakini ni ile genereation ya zamani ndo shida na ndo wenye ushawishi.

Kizazi cha sasa chahitaji elimu tu ya mpiga kura na haki zake pamoja na wajibu wake.
 
Inatakiwa kuwa hivyo. Ila wadanganyika tuna MATATIZO. Subiri utaona!
 
Viongozi wa ccm wenyewe wanakuambia upinzani wao upo kwenye chama chao tu,akipitishwa chamani basi huku kwingine akumsumbui!
 
Inatakiwa kupitishwa waraka kwa kila jimbo, mbunge ambaye hakuonekana jimboni katika kupush agenda za maendeleo, mbunge ambaye hakuwa na impact yoyote bungeni kuelezea kero za wananchi wake...huyo awekwe pembeni. Tungeanza japo hivyo, huenda watu wangeamka usingizini.
NAMI naongezea.
Ingewekwa Sheria Ili uweze kugombea ubunge, uwe unaishi/ umeishi Jimbo husika siyo chini ya miaka 10 mfululizo. Uwe na nyumba na wewe na familia Yako uishi Jimbo husika kwa kipindi tajwa hapo juu.
Ilivyo Sasa mtu anatoka huko anakuja kugombea hata hajui mahitaji ya wana Jimbo,hajawahi kushiriki MATATIZO ya kijamii,wananchi wana changamoto gani hajui halafu anapewa NAFASI ya kutatua changamoto ambazo hazijui.
 
Dr Damas buanaaa ana dhihaka sanaaa......hakuwa chaguo la wana Sonfea alitolewa huko number 6 ....akawa no 1
 
Back
Top Bottom