Mbunifu wa mavazi wa Kitanzania ampata Afisa aliyemuibia Begi la Nguo

Mbunifu wa mavazi wa Kitanzania ampata Afisa aliyemuibia Begi la Nguo

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1677177534256.png

Mbunifu wa kike wa Kitanzania anayeishi Houston nchini Marekani amedai kuwa nguo zinazovaliwa na afisa wa zamani wa Wizara ya Nishati (DOE) Sam Brinton zilikuwa kwenye mzigo wake uliopotea katika uwanja wa ndege huko Washington, D.C. mnamo 2018.

Asya Khamsin, ambaye ametengeneza brand yake ya nguo kwa miaka mingi, amesema hivi majuzi aliona ripoti kwamba Brinton alishtakiwa kwa kuiba mizigo katika viwanja vya ndege na kugundua kuwa afisa huyo wa zamani alionekana amevaa nguo zake katika picha kadhaa.

Khamsin amesema alikuwa amepakia nguo hizo kwenye begi ambalo lilitoweka Machi 9, 2018, kwenye Uwanja wa Ndege wa Kitaifa wa Ronald Reagan Washington.

Khamsin ameongeza kuwa alisafiri kwa ndege hadi Washington, D.C. kuhudhuria hafla ambayo alialikwa kuweka mavazi yake kwenye maonyesho. Hata hivyo, kutoweka kwa begi lake kulimzuia kushiriki.

Hii sio mara ya kwanza kwa afisa huyo kukumbwa na tuhuma za wizi wa mizigo katika viwanja vya ndege, kwa mujibu wa mtandao wa Fox News, October mwaka jana alishikiliwa akituhumiwa kwa wizi wa begi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Saint Paul uliopo Minneapolis na kuachiwa bila dhamana huku mwezi December mwaka jana alituhumiwa kwa kuiba begi katika uwanja wa kimataifa Harry Reid ulioko Nevada, akiachiwa baada ya kuwekea dhamana ya dola za Marekani 15,000 (shilingi milioni 35).
 
hyu mwenye kipara kama mwanaume nina mashaka naye hyu ...kesharudisha kadi yetu ya wanaume
 
hyu mwenye kipara kama mwanaume nina mashaka naye hyu ...kesharudisha kadi yetu ya wanaume
Hao ndo wale mabepari anaowapigania,,............hadi walimpa na uwaziri kabisa
 
Back
Top Bottom