Mbwa asili wa Tanzania hawaumwi kirahisi, rahisi kuwanunua na kuwahudumia, wanaishi muda mrefu. Tuache ushamba wa kupenda mbwa wa nchi za nje?

Mbwa asili wa Tanzania hawaumwi kirahisi, rahisi kuwanunua na kuwahudumia, wanaishi muda mrefu. Tuache ushamba wa kupenda mbwa wa nchi za nje?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Wana kinga asili nzuri dhidi ya magonjwa

Ni nadra sana kukuta hawa mbwa wetu wamepelekwa hospitalini kutolewa minyoo (de -worming), hata wengi tunaowafuga hawajawahi kuchomwa sindano yoyote tangu wazaliwa lakini wanadunda.

Kuwalisha kwa gharama nafuu
Hata ukiwachanganya ugali na dagaa kwa fresh tu, wanabonda vizuri tu.

Gharama rahisi ya kuwanunua
Hata ukiwa na elf kui yako unapata mbwa wako, si kama wengine inabidi uwe na laki 3

Ulinzi
Jichanganye uruke fensi usiku halafu ile umegusa sakafu ukutane nae mbwa aloefunzwa ulinzi (achana na wale koko wa mitaani), yani ukiachana na jinsi atakavyoku henyesha, ana sauti ya juu ya kubweka kwa nguvu sana kumstua mfugaji

Wanaishi muda mrefu
Nawajua watu wanafuga hawa mbwa tangu nikiwa shule ya msingi na sasa nimemaliza chuo nina kazi yangu lakini nikirudi kwetu kusalimia nawakuta mbwa wa majirani bado wapo fiti
 
Nenda kale jalalani kama kichaa uone kama hautadhurika. Na kichaa ni binadamu kama wewe.
 
Back
Top Bottom