Mbwa wana uwezo wa kuwaona Wachawi?

Duh, mkuu kama hutojali muulize Sheikh, Je hao majini wanaenda kwenye misikiti hii hii ya wanadam au wana misikiti yao? Na kama ni hii hii ni kwa nini wasiwe na ya kwao wategemee misikiti inayojengwa na wanadam?
Kwa uwelewa na aina ya mazingira ya kimaongezi tuliyokuwa nayo wakati namuuliza hili jambo, ilionesha ni kama adhana kwao pia ni wito au kumbusho la majini wazuri nao wakwaswari kama wafanyavyo binadamu. Kiufupi aliniambia kuna majini wacha Mungu na majini chukizo/mabaya, sasa kwamba wanaenda kuswari wapi nitamtafuta nimuulize mkuu
 
chukua matongotongo ya mbwa jipake usoni utawaona wachawi live bila chenga

angalizo
wachawi nao watakuona kwahiyo inabidi uwe tayari kwa lolote
asante kwa mbinu mkuu.

JAMANI, AMBAYE SIYO MWOGA AJARIBU HII MBINU halafu alete mrejesho kama ni kweli
 
Mbwa anaona walozi vizuri tuu. Watu wengi wanaishi na Mbwa na hawajui ishara zao za ndani. Mbwa ni mlinzi,, mbwa ni alarm, mbwa ni Mnajimu wa kiasi cha juu sana, mbwa ni muonaji wa hatari zinazoonekana na sizizoinekana, mbwa anaweza kupa ishara ya mtoto alietumboni ni wa jinsia gani, mbwa anaweza kumpenda mtu na akamlinda na hatari. Mbwa anaweza kukuwindia wanyama au ukaenda nae kuwinda na akakulinda. Mbwa anakupa taarifa ya "strangers" wote waliokuja usiku kama ni walozi, kenge, nyoka na kama wamejificha ndani Mbwa atakupa taarifa mpaka walipojificha.. Jifunze kukaa na mbwa wako na ujifunze maarifa ya mbwa. Ndio maana wazee zamani unakuta anampenda mbwa na wanapendana piga mbwa uone kama uhami nyumbani.
 
elezea na paka basii
 
Mbwa watano mbona wengi sana wote wa nini ,

Wawili tu wanatosha
kwa ujumla napenda mbwa, na naweza kuwa nao hata 10. Ila kwa case hii ni kwamba walikua wawili tu, akazaa watoto 8 (ni rottweiler). Kati ya hao watano nilishawauza na watatu bado wapo.
 
Ndio maana waislam hawawapendi mbwa
 
Na ndo maana yuko kwenye kundi la wanyama walinzi wanaona hata kwenye giza totoro but hawa wanaowala mbwa ni mitamaa yao tuu na ulafi wa asili
Hufahamu kula nyama ya mbwa au punda husababisha resistance kali kwa issue za ulozi
 
Badilisha godoro lako.........utanishukuru baadaye........ulitaka mbwa aseme au kama sio kubweka😂😂😂!!!!!!!
au abadili uelekeo wa kulala, miguu na kichwa?...
 
Mkuu, wanyama wengi huona vitu vingi ambavyo wanadamu hawawezi kuona kutokana na muundo wa macho yao. Wanyama wengi macho yao ni compound lenses na hivyo they can perceive a lot of visible light tofauti na wanadamu ambao macho yetu si compaund lens, wajuaji wanasema we can only perceive 5% of visible light na ndiyo sababu hatuna uwezo wa kuona invisible things kama mapepo nakadhalika.....

Hata ukisikia wanasema eti mtu ametumia madawa anaweza akaona mapepo au wachawi au vitu vya ajabu ambavyo wengine hawawezi kuona, ukweli ni kuwa anakuwa ametumia dawa (or cultivation resource) ya kuongeza uwezo wa macho yake wa kuona/kuhimili mwanga mkali. Bahati mbaya dawa kama hizo si rahizi kuzipata, wanaozijua ni wachache. It is forbiden science ambayo ndiyo tunaiita uchawi.
 
Mbwa ukiishi nae vizuri anakupa kila kitu yaani, alarm, alert, kunusa hatari n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…