Mbwana Samatta huenda akasajiliwa na timu ya Middlesbrough ya Uingereza mwezi January.

Mbwana Samatta huenda akasajiliwa na timu ya Middlesbrough ya Uingereza mwezi January.

Bora abaki Genk anacheza Europa anaoneka vizuri na timu kubwa kuliko aende Middlesbrough iliyo second division na hakuna mechi za kimataifa.
 
Utoke timu inayocheza uefa uropa uende timu ya daraja la pili? Hahahaaa Hesabu zinagoma kabisa. Genk inaongoza ligi kwa muda mrefu sasa ko we unasema genk ni sawa na timu ya daraja la pili?
 
Lakini kwa umri wake sasa yupo kwenye "peak" hivyo si vibaya akijiongeza kabla ya kufikia 30
Kumbe ni championship, aliposema daraja la kwanza nilidhani league one. Champioship sio mbaya, anaweza akapanda nayoo, wako wa nne.
 
Utoke timu inayocheza uefa uropa uende timu ya daraja la pili? Hahahaaa Hesabu zinagoma kabisa. Genk inaongoza ligi kwa muda mrefu sasa ko we unasema genk ni sawa na timu ya daraja la pili?
Akichukua kikombe msimu huu kama middlesbrough inamuhitaji aende, middlesbrough wako ktk nafasi nzuri kurudi ligi kuu na pia mshiko utaongezeka.
 
Mi naona asubili usajili mwezi wa tano,wakati huo akaze buti achukue golden boot na ajitahidi sana awe kwenye orodha ya wafungaji bora Europa league,hii itaongeza thamani yake katika usajili.BTW kwa sasa analipwa bei gani?
 
Samatta sizani kama atakubali kwenda, jamaa anajiamini na anajeuri, Simba aliwafanyiaga jeuri walivyo kataa kutimiza matakwa yake, pia Katumbi alikua mgumu kumwachia bila kukomaa asingetoka Mazembe. Anaweza asiende timu kubwa sana ila atakomaa aende ligi kubwa siyo kurudi nyuma. Kwangu bora abaki Genk mpaka ligi ishe kwa speed ya Genk mwakani watacheza champions league na dirisha kubwa anaeza pata timu nzuri zaidi. Ukizingatia kuna uwezekano akawa top scorer wa ligi yao.
 
Utoke timu inayocheza uefa uropa uende timu ya daraja la pili? Hahahaaa Hesabu zinagoma kabisa. Genk inaongoza ligi kwa muda mrefu sasa ko we unasema genk ni sawa na timu ya daraja la pili?
Kwa mfano wewe ndio unachezea Yanga inayoongoza ligi ya Tanzania halafu club ya Aston Villa inayoshiriki ligi ya Championship kule Uingereza ikakuhitaji utaacha kwenda kisa unachezea timu inayoongoza ligi?! Point yangu tafuta kigezo kingine cha kumshauri Samata asiende Middles ila sio hicho ulichoandika.
 
Nasikia jamaa jana katupia mbili tena huko ubelgiji.
 
Samatta sizani kama atakubali kwenda, jamaa anajiamini na anajeuri, Simba aliwafanyiaga jeuri walivyo kataa kutimiza matakwa yake, pia Katumbi alikua mgumu kumwachia bila kukomaa asingetoka Mazembe. Anaweza asiende timu kubwa sana ila atakomaa aende ligi kubwa siyo kurudi nyuma. Kwangu bora abaki Genk mpaka ligi ishe kwa speed ya Genk mwakani watacheza champions league na dirisha kubwa anaeza pata timu nzuri zaidi. Ukizingatia kuna uwezekano akawa top scorer wa ligi yao.

Uko sawa ila pia inategemea na Genk kama wanataka kutengeneza faida ikiwa watamuuza kwa milioni 7 au 8.

Angalia walimsajili kwa kiasi gani kutoka TP Mazembe.
 
View attachment 975661

Mshambuliaji wa kimataifa wa taifa Stars na KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta yumo kwenye orodha ya wachezaji wanaotakiwa kusajiliwa na timu ya Middlesbrough ya Uingereza mwezi ujao.

Meneja wa timu hiyo ya mhimili wa pili wa ligi kuu ya Uingereza au Tier two iliyo na makazi na uwanja wake wa Riverside Tony Pulis, amevutiwa na mshambuliaji huyo ambae mpaka sasa amefunga magoli 75 kwenye mechi zote alizocheza.

Timu ya KRC Genk imeweka thamani ya pauni za Uingereza milioni kati ya 7 hadi 8 ili kumwachia mchezaji huyo aende nchiniu Uingereza.

Samatta ameonyesha umahiri mkubwa katika kufunga magoli ambapo mpaka sasa amefunga magoli 12 katika mechi 18 ambazo timu yake KRC Genk imecheza katika ligi ya Ubelgiji ya Belgian Jupiler Pro League.

Samatta alitengeneza jina lake katika timu ya TP Mazembe ya Congo DRC tangu mwaka 2011 hadi 2016 ambapo mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 160 katika mechi 103 alizochezea timu hiyo.

Alijiunga na KRC Genk mwaka 2016 ambapo mwaka huohuo alitwaa taji la mwanasoka bora wa Afrika akifunga magoli 55, usaidizi assists mara 14 katika mechi 151 alizochezea Genk.

Meneja Tony Pulis anaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji huyo katika kuboresha safu yake ya ushambuliaji wa timu hiyo katika duru la pili la mzunguko wa ligi hiyo ngumu ya daraja la pili ijulikanayo kama Championship.

Samatta huenda akaziba nafasi ya mshambuliaji Rudy Gestede ambae huenda nae akasajiliwa na timu ya Celtic ya Scotland baada ya kushindwa kuonyesha makucha yake kwa Middlesbrough.

Hata hivyo pia timu za ligi kuu ya Uingereza nazo zimekuwa zikiwatuma maskauti wao kwenda kumuangalia Samatta akicheza mechi mbalimbali za hivi karibuni.

Timu za Everton, West Ham United, Burnley na Brighton & Hove Albion zote zinaangalia kujiimarisha katika mzunguko wa pili wa ligi hiyo ambao umeanza katika kipindi hiki cha siku kuu ya Christmas.

Endapo Genk watakuwa tayari kumwachia mchezaji huyo kupitia kifungu maalum kiitwacho "release clause" ambacho huwekwa kwenye mkataba, basi Samatta ataingia Uingereza mwezi ujao wa January.

Mwezi January dirisha la usajili hufunguliwa tena kwa usajili mdogo ambapo timu mbalimbali hujaribu kusajili wachezaji wengi wa gharama nafuu kulingana na mahitaji.

Eti samata alitengeneza jina lake TP MAZEMBE.. hakuna ulipoitaja simba..kwa hiyo usipoitaja simba unapata faida gani kwa mfano!! Hizi ni akili za AKILIMALI
 
Eti samata alitengeneza jina lake TP MAZEMBE.. hakuna ulipoitaja simba..kwa hiyo usipoitaja simba unapata faida gani kwa mfano!! Hizi ni akili za AKILIMALI
Duh kwa hiyo hilo nalo linahitaji mjadala?! Simba ilimtambulisha Mazembe ikamtengenezea jina.
 
Samatta akomae hapo hapo Genk na pia azidishe tu kujituma,kumbuka Genk ndio team iliyowatoa kina De bruyne,Banteke na Thibaus courtois.
 
K
View attachment 975661

Mshambuliaji wa kimataifa wa taifa Stars na KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta yumo kwenye orodha ya wachezaji wanaotakiwa kusajiliwa na timu ya Middlesbrough ya Uingereza mwezi ujao.

Meneja wa timu hiyo ya mhimili wa pili wa ligi kuu ya Uingereza au Tier two iliyo na makazi na uwanja wake wa Riverside Tony Pulis, amevutiwa na mshambuliaji huyo ambae mpaka sasa amefunga magoli 75 kwenye mechi zote alizocheza.

Timu ya KRC Genk imeweka thamani ya pauni za Uingereza milioni kati ya 7 hadi 8 ili kumwachia mchezaji huyo aende nchiniu Uingereza.

Samatta ameonyesha umahiri mkubwa katika kufunga magoli ambapo mpaka sasa amefunga magoli 12 katika mechi 18 ambazo timu yake KRC Genk imecheza katika ligi ya Ubelgiji ya Belgian Jupiler Pro League.

Samatta alitengeneza jina lake katika timu ya TP Mazembe ya Congo DRC tangu mwaka 2011 hadi 2016 ambapo mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 160 katika mechi 103 alizochezea timu hiyo.

Alijiunga na KRC Genk mwaka 2016 ambapo mwaka huohuo alitwaa taji la mwanasoka bora wa Afrika akifunga magoli 55, usaidizi assists mara 14 katika mechi 151 alizochezea Genk.

Meneja Tony Pulis anaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji huyo katika kuboresha safu yake ya ushambuliaji wa timu hiyo katika duru la pili la mzunguko wa ligi hiyo ngumu ya daraja la pili ijulikanayo kama Championship.

Samatta huenda akaziba nafasi ya mshambuliaji Rudy Gestede ambae huenda nae akasajiliwa na timu ya Celtic ya Scotland baada ya kushindwa kuonyesha makucha yake kwa Middlesbrough.

Hata hivyo pia timu za ligi kuu ya Uingereza nazo zimekuwa zikiwatuma maskauti wao kwenda kumuangalia Samatta akicheza mechi mbalimbali za hivi karibuni.

Timu za Everton, West Ham United, Burnley na Brighton & Hove Albion zote zinaangalia kujiimarisha katika mzunguko wa pili wa ligi hiyo ambao umeanza katika kipindi hiki cha siku kuu ya Christmas.

Endapo Genk watakuwa tayari kumwachia mchezaji huyo kupitia kifungu maalum kiitwacho "release clause" ambacho huwekwa kwenye mkataba, basi Samatta ataingia Uingereza mwezi ujao wa January.

Mwezi January dirisha la usajili hufunguliwa tena kwa usajili mdogo ambapo timu mbalimbali hujaribu kusajili wachezaji wengi wa gharama nafuu kulingana na mahitaji.
Kutoka Genk kwenda Middlesbrough timu ya Daraja la pili. Hapana kwa kweli.
 
Back
Top Bottom