Mch. Mwasapile vs. Mch. Rwakatale

Samahani sana mkuu yaani "babu" unataka kumfananisha na Yesu????????? Khaaaaa yaani wewe jamaa wa ajabu sana unamfananisha Messi na Ngasa?! Yesu ni world ICON huwezi kumfananisha na mtu wa kawaida mkuu..............

Aah kaka? Hajawafananisha bwana, amekosoa doubt ya Judy kwenye masharti kwa kuonesha kuwa hata Yesu alikuwa na masharti. Right Moh'd?
 
Imani yako ndio itakayokuponya kama huamini hulazimishwi kuamini waacheni wale waaminiyo waendelee na imani yao.

Mungu akubariki sana na uwe na amani siku hii ya leo
 
Kama wanapona kweli basi tumpe nafasi maana kwanza kajionyesha hamaindi pesa ,na gurani inasema kila gonjwa mungu kaweka tiba,tutajua tu kama ni mambo za kinaijeria ama ni vipi after yote bible ilisema siku za mwisho watatokea manabii wengi wakifanya kuponya kwa uwezo wa yesu ambaye siku ya mwisho wakitaka kufunguliwa mlango wa peponi watasema tuliponya kwa jina lako naye yesu atawambia ONDOKENI SIWAJUI ni unabii unatimia kutakuwa na matetemeko(japan,ireland)tetesi za vita-mashariki ya kati.
Mwisho uko karibu zaidi udhaniavyo kuna watu wametabili disemba 2012 mambo yanayotokea sasa yananifanya niwaze sana hebu google 2012 end of world usome mwenyewe.hata wimbi la uarabuni linaloendelea wanasema ni maandao ya the return of mahd,yani masiha alieahidiwa kama ni kweli tuna mwaka mmoja tu na nusu TUBU.and google that upime mwenyewe
 
Jambo hili usiliangalie kitheolojia liangalie kiroho, ukiliangalia kitheolojia hutapata majibu, maana mpaka sasa theolojia imeshindwa kutoa majibu mengi ikiwa ni pamojana chanzo cha Mungu ni nini? theologia imekuwa ikipinga baadhi ya mambo ya kiroho kitu kinachowafanya baadhi ya watumishi mara wanapobobea katika elimu ya theologia wamwache Mungu na kufanya mambo ambayo yapo kinyume na mafundisho ya kiroho. Nafikiri wewe ni baadhi ya wanatheolojia wengi ambao hawana nguvu za roho mtakatifu bali wamejawa na udadisi na maswali ili kujipa upenyo wa kupinga uwezo wa Mungu. Mzee yule kama angejiita ni mganga wa kienyeji kusingekuwa na swali watu wangeenda kisirisiri kujipatia dawa, kwakuwa amesema dawa hiyo ameoteshwa na Mungu watu hawaamini maana wengi wanamashaka na uwezo wa Mungu, hii ni hatari na aibu sana. Inapotokea mtu anayemjua Mungu tena Mtu mwenye imani akahoji uwezo na sababu za dawa hiyo kuoteshwa mzee huyo tu ni kujaribu kuhoji utendaji wa kazi za Mungu ambapo kiimani ni sawa na ujinga au ushamba wa kiimani.
 
Kama wanapona kweli basi tumpe nafasi maana kwanza kajionyesha hamaindi pesa ,na gurani inasema kila gonjwa mungu kaweka tiba,tutajua tu kama ni mambo za kinaijeria ama ni vipi after yote bible ilisema siku za mwisho watatokea manabii wengi wakifanya kuponya kwa uwezo wa yesu ambaye siku ya mwisho wakitaka kufunguliwa mlango wa peponi watasema tuliponya kwa jina lako naye yesu atawambia ONDOKENI SIWAJUI ni unabii unatimia kutakuwa na matetemeko(japan,ireland)tetesi za vita-mashariki ya kati.
Mwisho uko karibu zaidi udhaniavyo kuna watu wametabili disemba 2012 mambo yanayotokea sasa yananifanya niwaze sana hebu google 2012 end of world usome mwenyewe.hata wimbi la uarabuni linaloendelea wanasema ni maandao ya the return of mahd,yani masiha alieahidiwa kama ni kweli tuna mwaka mmoja tu na nusu TUBU.and google that upime mwenyewe
 
Nenda ukanywe kombe kwa imani utapona, peleka kitambaa kwa Rwakatale kwa iman utapona.

"The secret of the word of God"
If u know the word of God u can use it to cure and raise dead bodies .
Believe me the power of the word of God is very strong if u know how to use it.
 

is that the power of the word of God, or the power of a dream?
 
sasa tena ameibuka Mch. Mwasapile akidai kupata ndoto juu ya mti ambao unapochemshwa, kikombe kimoja tu cha maji yake kinatosha kutibu magonjwa sugu kama ukimwi, kisukari, kansa, pumu nk. hapa pia sioni msingi wa kitheolojia.

Judy hoja yako naipata but suala la imani ni gumu sana.....

Hata babu asingetumia maji bado wengine tungehoji kama kweli ni mungu kwa nini watu walazimike kusafiri mpaka loliondo. Kwa nn wasitume hizo 500 kwa mpesa then babu awatibu au kuwafanyia maombi remotely. Mungu anhidwa nn. Ukianza kujiuliz maswali kwenye IMANI hayaishi.

Imani yeyote hawezi kukosa maswali na hakuna imani inayoweza kupata majibu kama ya kisayayansi na kihesabu.

Kuhusu huyu babu ni uzembe wa serikali kila kukicha watu wanazidi kujiuliza maswali sbabu wamekaa kimya.

  • waliotumia dawa wapo
  • maji yapo
  • walio tayari kutumia dawa wapo
  • maabara zipo
Sasa tuweke imani ya dini pembeni kwa nn serekali hawatoi jibu fasta japo la awali na la kisayansi tujue? Itaachukua hata miezi mwilili huku kila kukicha wanasiasa na watu tunakuja na theory mpya kila siku.

Babu kapigwa stop nami naunga mkono hatua hiyo sababu idadi ya watu iliyokuwa inamiminika ni kuwba. Lakini imsingi hata kina Sheikh yahya ni kina babu wa dar es salaam Tofautini kuwa ni idadi ya watu tu.

Babu anaweza kusema kinchotibu si maji bali ni imani lakini hata yeye babu hajui chemical conntet ya yale maji yake .inawezekana ni kweli maji ndo yanatibu na si imani. wa kutibitisha haya ni serikali.


Serikali itoe jibu mapema watu wasibaki gizani.
 
jamani ebu acheni mungu aitwe mungu, kwani analopanga yewe au kufikiria, kwa mwanadamu sio rahc, so miujiza au imani hutolewa kwa njia nyingi ili kupima imani ya w2, bt cha muhmu sio marumbano, bali tuamini kuwa miujiza ya mungu yawezekana. Na hutokea kwa aina nyingi.
 
Miss Judith, kuna tatizo kubwa sana kichwani kwako. Labda nikusaidie tu ni kuwa Biblia inasena "zijaribuni kila roho kama zimetoka kwa Mungu ama la". Hivyo fanya Homework, ijaribu wewe hii Roho iliyopo kwa Babu kisha njoo hapa utuambie kama imetoka kwa Mungu ama la usisubiri msaada kutoka kwetu tuombe kwa niaba yako. Nenda, ijaribu, njoo tueleze au piga goti omba ufunuliwe kisha njoo utueleze. Huu ndio msaada wangu kwako dada!
 

Sio kwenye biblia tu wapo pia wasiojua Quraan na wapo wasiojua ABC za siasa lakini utakuta anakoboa pumba tu!

Sijui kama tutafika na tukifika tunatakuwa taabani..............
 
Dada Judy hongera kwa wazo uko sahihi sana maana neno la mungu lina fundisha tusiziamini kila roho bali tuzichunguze Kama kweli zinatokana na mungu, inamaana mungu alishajua shetani atacopy vitu vyake na atavifanya kwa wanadamu na wanadamu wafikirie ni mungu na kumbe siye mungu,

Hii tabia ya watu kusikia miujiza na kuikimbilia na baadae kuja kuiponda imekuwa kitu cha kawaida sana kwa dunia ya sasa imezidi, mama Rwekatare, Kakobe, Ngurumo ya upako nk. walipaparikiwa sana na walipata wafuasi wengi sana ila baada ya muda walipondwa sana na wote walikuwa wanatumia bible kufanyia miujiza kwahiyo navyoona huu ndio huohuo mtiririko unaendelea sana sana napenda kuwashauri hivi technic zote anazozitumia mungu kwa wanadamu shetani keshaziiga na yeye antumia hizozo anatuchezea tuu akili zetu kwhiyo tunapaparika tuu bure vitabu vya dini vinatuongoza vizuri sana ila tunavisoma Kama vya hadithi hatuelewi tumebakia kukariri mistari ya bible 'we have to study and to learn the bible and not read' umizeni vichwa kumjua mungu Kama mnavyoumiza kufaulu mitihani sio kukupaparikia miujiza acheni uvivu wa kumuomba mungu wenyewe.

Wagonjwa nawataka radhi sio kwamba wagonjwa msiende loliondo nendeni mkanywe dawa kupona kweli mtapona ila sio kwasababu umepona ufikirie ndio mungu amekuponya 'hata Yesu walimwendea wakamwambia kumbuka bwana tulitumia jina lako kuponya magonjwa na wagonjwa walipona lakini aliwaambia tokeni kwangu siwajui' Nani vigumu kweli kumwambia mgonjwa asiende loliondo aijalishi anaeponya ni shetani au ni mungu cha msingi amepona au vipi wanajamii
<p> </p>
<p>&nbsp;</p>
 
Miss Judith, msingi wa tiba ya babu ni imani yako katika "kristu" na hivyo ni ibada yako katika kupata tiba. Uliwahi kuona ibada yoyote inaendeshwa na kisha maswali yanafuata?:smash:
 
hapo umenena vema, by the way nasikia babu ametabiri kifo chake, atakufa siku ya jumatatu ya pasaka.
 


aurgument yako ni sawa lakini:-

katika Yohana 5 - Bwana Yesu aliwakuta wagonjwa wakisubiri birika lichemke na anayeingia wa kwanza anapona. KWANINI YESU ALIINGILIA KATI??? AKAMPONYA YULE MGONJWA WA MIAKA 38 - AKAMWAMBIA WATAKA KUWA MZIMA?? JITWIKE GODORO LAKO UENDE - mbona hakumsaidia kuingia kwenye lile birika maji yanapochemka????? INAONYESHA YESU NI ZAIDI YA MAJI KUCHEMKA - YESU NI ZAIDI YA KIKOMBE CHA BABU - katika Biblia - TUMEPEWA JINA LA YESU, TUMEPEWA DAMU YA YESU - kwa ajili ya uponyaji - na chochote tutakachokiombea ili nguvu za MUNGU ZIWE NDANI YAKE e.g. kitambaa etc.
TUKUMBUKE KUWA YESU - ALIKUJA KUTAFUTA KILICHOPOTEA, ALIKUJA KUFUNGUA WALIOFUNGWA NA MINYORORO YA DHAMBI
DAWA YA BABU UNAPOKUNYWA ................UNAAMBIWA HABARI YA KUTUBU DHAMBI NA KUZIACHA??? HABARI ZA UTAKATIFU??? AU NI UPONYAJI TU???? ANGALIZO::: TUSIPONE MIILI YETU TU ........BALI ROHO ZETU PIA ZIPONE..... IMANI HUJA KWA KUSIKIA NENO LA KRISTO - JE KWA BABU NENO LIPO???

sipingi dawa hiyo kwenye kikombe ..........ila PAMOJA NA KUNYWA ... BADO WALIOPONA WANA SAFARI NDEFU ..... KUMWAMINI MWENYE KUTIA NGUVU KATIKA HUO MTI .......................nawasilisha!!!!!
 
Judy,

Uwezo na Utendaji kazi wa Mungu hauwezi kuchunguzika kwa uwezo wa Kibinadamu. Je, kuamini ni mpaka angeshuka MUNGU mwenyewe na kuitoa dawa hiyo? Je, ni kwanini sisi wanadamu na hasa watz tuwagumu wa kuamini au ndo kile kizazi cha imani haba?

Bi Judy, kumbuka hata BWANA YESU alipokuja na kuponya watu magonjwa kwa ishara na miujiza mbalimbali bado wapo ambao hawakumuamini je, itakuwa mwanadamu aliyepewa uwezo na mamlaka na MUNGU? Kumbuka Imani ni kuwa na hakika na mambo yajayo na nibayana ya mambo yasiyoonekana.

Tutaendelea kusitasita hadi lini? Ila tukumbuke.....people are still coming from different corners to be healed....
 
Hii hoja aliyoanzisha Judy ni ya msingi sana ingawa jibu la mwisho ni 'inabidi uwe na imani'
 
Mungu ana njia nyingi za kutenda miujiza, tusiamini kuwa njia pekee ya kuombewa na kuponywa ni kuwekewa mikono tu. Wenzangu hapo juu wametoa mifano mingi ya namna Mungu alivyotenda miujiza mingi kwa namna tofauti. Kumbuka Naaman alivyoambiwa na Elisha akaoge mto yordan na kuponywa ukoma, fimbo ya Musa ilivyogeuka kuwa nyoka, haya yote yakitokea leo sidhani kama utaamini ni Mungu yule yule anatenda hata leo.

Kusema haya sihalalishi kila kinachotokea leo kuwa ni cha Mungu. Biblia inasema zipimeni hizo roho. Kama huwezi kuzipima hizo roho katika ulimwengu wa kiroho, usijaribu kuzipima kwa nguvu na msukumo wa hisia, utajikuta unaishia kuanzisha dhehebu lako.

Ubarikiwe mpendwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…