Elections 2010 Mchagueni Slaa: (mashairi)

Elections 2010 Mchagueni Slaa: (mashairi)

Umenena Kaburunye, neno lako ni sawia
Umegongelea kwenye, kichwa na kwenye mkia
Umewatoneshe penye, donda wanaugulia
Dokta ndiye daktari, wa Kuponya Tanzania

Jibaba Bonge kamili, hoja yako ni murua
nimekubali mswahili, sistimu kuifumua
ni ukombozi wa pili, hapana kusuasua
Dokta ndiye daktari, wa kuponya Tanzania

Ogah jembe makini, umelonga kwa hisia
kwayo yako tathmini, Ikulu tutaingia
CCM haijiamini, ndo mana wanalia
Dokta ndiye daktari, wa kuponya tanzania.

Anysile mtaalamu, sina cha kuongezea
Yako ni nyingi ilimu, jinsi ulivyoelezea
Tutaishika hatamu, CCM tajiondokea
dokta ndiye daktari, wa kuiponya tanzania

Wambugani ncha kali, mzalendo mtanzania
tungo zako za akili, zenye uchungu na nia
wasikika toka mbali, kila pembe ya dunia
dokta ndiye daktari wa kuiponya Tanzania

Kamanda Kidundulima, umetuonyesha njia
Kamwe haturudi nyuma, wito tunaitikia
Kina baba kina mama, na vijana wote pia
dokta ndiye daktari, wa kuponya Tanzania

Unatisha sana Nyunyu, ulosema yaningia
we ni mvua si manyunyu, hazina ya Tanzania
tutawakwanyua kwanyu, kura sitowapigia
dokta ndiye daktari wa kuponya Tanzania

Golder maji ya dhahabu, nawe nakukubalia
yafaa tuwaadhibu, kura kutowapatia
kwani wametughilibu, miaka mingi twaumia
dokta ndiye daktari wa kuponya tanzania
 
Umenena Kaburunye, neno lako ni sawia
Umegongelea kwenye, kichwa na kwenye mkia
Umewatoneshe penye, donda wanaugulia
Dokta ndiye daktari, wa Kuponya Tanzania

Jibaba Bonge kamili, hoja yako ni murua
nimekubali mswahili, sistimu kuifumua
ni ukombozi wa pili, hapana kusuasua
Dokta ndiye daktari, wa kuponya Tanzania

Ogah jembe makini, umelonga kwa hisia
kwayo yako tathmini, Ikulu tutaingia
CCM haijiamini, ndo mana wanalia
Dokta ndiye daktari, wa kuponya tanzania.

Anysile mtaalamu, sina cha kuongezea
Yako ni nyingi ilimu, jinsi ulivyoelezea
Tutaishika hatamu, CCM tajiondokea
dokta ndiye daktari, wa kuiponya tanzania

Wambugani ncha kali, mzalendo mtanzania
tungo zako za akili, zenye uchungu na nia
wasikika toka mbali, kila pembe ya dunia
dokta ndiye daktari wa kuiponya Tanzania

Kamanda Kidundulima, umetuonyesha njia
Kamwe haturudi nyuma, wito tunaitikia
Kina baba kina mama, na vijana wote pia
dokta ndiye daktari, wa kuponya Tanzania

Unatisha sana Nyunyu, ulosema yaningia
we ni mvua si manyunyu, hazina ya Tanzania
tutawakwanyua kwanyu, kura sitowapigia
dokta ndiye daktari wa kuponya Tanzania

Golder maji ya dhahabu, nawe nakukubalia
yafaa tuwaadhibu, kura kutowapatia
kwani wametughilibu, miaka mingi twaumia
dokta ndiye daktari wa kuponya tanzania

Mkuu wee ni mkali........hands down!
 
Chadema ni chama bora

1. Juma la lala slama, ni tamati ya kampeni,
Hatunayo la kusema, tuhakiki vituoni,
Na kutumia hemkima, kuchagua kwa makini,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.

2. Slaa tumchague, fikira zake makini,
CCM mtulie, CHADEMA ya amani,
Katu wasitusumbue, CHADEMA ni tumaini,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.

3. Rais toka CHADEMA, Ikulu na aingie,
Ufisadi utakoma, rushwa atukingie,
Jamii pate huduma, mapato atujazie,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.

4. Anena mengi mazuri, aingie Magogoni,
Kweli Slaa hodari, mafisadi kabaini,.
Ni wezi wamekithiri, dola ipo likizoni,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.

5. CHADEMA chama bora, CCM ni utani,
Na tusifanye papara, maisha yakawa duni,
Sote tuwe na busara, kurejesha tumaini,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.

6. CCM ni maafa, maisha yabaki duni,
Nchi haina sifa, wazidi umaskini,
Yaporomokoa taifa, CHADEMA tuchagueni,
CHADEMA ni chama bora, sote ushindi tuipe.
 
Back
Top Bottom