mchakato wa katiba Mpya

Mr zam

Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
11
Reaction score
1
Jamani wana JF, mchakato wa katiba mpya unategemea kupelekwa bungeni katika kikao kijacho cha bunge kwa mujibu wa taarifa ya mwisho wa mwezi wa March ya Mheshimiwa raisi lakini inakuaje yale makongamano, semina nk yanayotoa ufahamu wa namna ya undwaji wa katiba hiyo mpya ili umuakisi kila mtanzania kwa hadhi yake hayaanzi kutolewa au mpaka waanza vyama vya upinzani?
 
Mkuu muswada unaotarajiwa kuletwa bungeni, pamoja na mambo mengine unapashwa kutoa utaratibu rasmi utakaotumika siyo tu katika kukusanya maoni ya wananchi, lakini pia namna maoni hayo yatakavyoratibiwa na hatimaye kujumuishwa katika rasimu ya katiba itakayoandikwa kufuatia ukusanyaji wa maoni hayo. Hivyo kwasasa kazi ilyoko mbele ya sisi zote wenye mapenzi mema na taifa ili, ni kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba sheria itakayotungwa na bunge baada ya kuwasilishwa kwa muswada huo inatoa fursa na uhuru wa kweli kwa raia wote kushiriki katika mchakato uandikaji wa katiba mpya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…