Mchanga na kokoto za kujengea

Mchanga na kokoto za kujengea

liolio

Member
Joined
Mar 14, 2013
Posts
40
Reaction score
8
Ndugu zangu wana jf naombeni ushauri. Kwa ufupi nataka kufanya biashara ya kusambaza mchanga na kokoto, ila kabla ya kuanza ningependa kujua yafuatayo
. Biashara hii ipoje?
. Sehemu ya kupata malighafi
. Masoko yake yapoje?
. Mtaji kiwango cha chini cha kuanzia

Tafadhali sana naomba ushauri wenu...!!
 
Mtaji wa kuanzia una sh ngapi? Una malori mangapi na ya ujazo gani? Una eneo la kuhifadhi hizo kokoto hapa mjini? Kokoto zinapatikana lugoba na msolwa. Wengi wanaosaga huuza moja kwa moja kwa wateja.
Mtaji wa chini ni milioni kumi kama una malori ya uhakika
 
Ndugu zangu wana jf naombeni ushauri. Kwa ufupi nataka kufanya biashara ya kusambaza mchanga na kokoto, ila kabla ya kuanza ningependa kujua yafuatayo
. Biashara hii ipoje?
. Sehemu ya kupata malighafi
. Masoko yake yapoje?
. Mtaji kiwango cha chini cha kuanzia

Tafadhali sana naomba ushauri wenu...!!
Mkuu hii ni biashara ya wenye ubavu wa fweza na vifaa pamoja na logistical management.
Kwa kuanzia uwe na ingalau malori mawili au matatu ya tani 25.
Tani mpja ya kokoto kule Lugoba ni Tshs 35,000
Kwa kawaida tani hiyo inasafirishwa kwa Tshs 20,000 mpaka Dar.
Hivyo basi gari moja kufikisa Dar ni Tshs 1,375,000 kabla ya kodi na ushuru.
Gari moja yaweza fanya tripu moja kwa siku

Hivyo basi ukiwa na gari mbili unsongea turnover ya Tshs 2, 750,000 kwa siku moja,
Mahesabu haya hujaweka, trafiki njiani, wizi wa dereva(mafuta na kokoto),posho ya dereva, wear and tear ya gari, na overwight ya mizani( fine mbaya sana hapa)

Ukiyaweza hspo ingia ngoma ucheze.
 
Ahaa hah asante sana Masopa. Na masoko yake yapoje kwa huo mchanga nitakao uleta Dar.
 
Pembe unaweza niambia kuwa hao wateja wananunua kwa sh ngapi. Sio lazima iwe specific hata kwa avarage tuu.
 
Back
Top Bottom