Mchanganuo wa biashara ya kuingiza faida ya 150,000/= kwa siku/ 4,400,000 kwa mwezi

api umeshakamilisha theory, ingia kwenye kutenda alaf uje ulete mrejesho
 
Kama kawaida wazee wa kukosoa tuponhapa sio kwa nia mbaya ni kwaajili ya kujenga na kuangalia mambo kwa upana zaidi.

Matumizi ya Chakula na mafuta 25,000 kwa siku, ina maana kwa pikipiki zote tatu? Kama ni hivyo basi kila pikipiki moja na dereva wake watatumia 8,300. Dereva tuseme ale 3000 asubuhi buku mchana 2000. Inabaki 5000. Haya 5000 unaweka mafuta ya lita ngapi ya kutosha kusambaza trey 45 za mayai? Au hayo mafuka yatakuwa karibu karibu?

Hapo hatujamhesabu meneja wa masoko uju

Mwisho kabisa ukasema faida ya mwezi ni 155,000 × 31 = 4,805,000
Ukasema hii 4805000 ni faida kwa mwezi . Nikwambie tu ndugu hiyo ni faida tarajiwa sio faida halisi, faida tarajiwa haina uhusiano wa moja kwa moja na faida halisi itakayopatikana hasa kwenye biashara. Kwanini? Kwanza sio kila mwezi una siku 31, mwezi wa pili una siku 28-29
155,000 × 29 = 4,495,000 mpaka hapo kuna 310,000 imepungua.

Pili mambo mengi hutokea hata katikati kabla ya kufika mwisho wa mwezi, siamin kama wasambazaji wataweza kusambaza idadi hiyo hiyo trey 45 kila siku kwa miezi yote. Kuna mtu kuumwa, kufiwa, pikipiki kuharibika, service, dharura zengine kibao.

Kingine, ulinena vyema kuwa tafuta eneo lenye mzunguko wa biashara mfano sokoni au stand upange frame, shida ikaja bei ya frame na kulipa kwa miezi mitatu. Sehemu kama sokoni au stand ni vigumu kulipa kodi ya miezi mitatu labda kama wanakujua, au ni mpangaji wa muda mrefu. Sehemu kama hizo zina ushindani mkubwa na uhitaji mkubwa wa frame. Mfano K/koo ilifikia hatua ili upate frame lazima uhonge hela mtu akuachie frame yake aliyopanga, akikuachia ndo upatane na mwenye pango ulipe kodi. Sasa sehemu ya hivyo nani atakubali umlipe kwa miezi mitatu? Kodi elfu 80

Pikipiki used, tena ya laki 8 tegemea kukuharibikia kila mwezi, sijaona mahali uneweka pesa ya kuzitengeneza? Hela ya emergency sijaona mahali umetaja. Au hizi pikipiki hazitaharibika mwezi mzima? Acha kuharibika hutafanyia service?

Hujaweka gharama za kufata hayo mayai kwa wafugaji hujaweka gharama ya kila trey moja utanunua kiasi gani. Umesema tu tenga 3.5M kama mtaji wa mayai. Ungeleta mchanguo wake ingekuwa vyema sana kama ukivyofanya kwingineko

Mwisho kabisa: ukachukua 4,805,000 ambayo ndo faida yako kwa mwezi ukasema ukitoa matumizi ya mishahara pamoja na hasara inabaki 4,400,000. Ina ya kwamba mishahara pamoja na hasara ni 405,000. Jumla ya wafanyakazi ulionao ni wanne kwahiyo kila mmoja utamlipa 101,250/=

Nikuulize tu wewe kama ndo ungekuwa mmoja kati ya hao wafanyakazi ungekubali kulipwa laki moja alafu unajua kabisa boss wako anapata faida zaidi ya Millioni 4?? UNGEKUBALI?

Kwa hali ya sasahivi ilivyo nani atakubali kulipwa 1012,50. Kazi uliyowapa ina masharti magumu, kwa siku anatakiwa auze sio chini ya trey 45 alafu mshahara umlipe laki? 45×30 = 1,350

Yaani kwa kila trey moja unamlipa atakayouza utamlipa 75/=

UKIMPATA HUYO MFANYAKAZI NIITE MBWA NIMEKAA PALE.. [emoji117][emoji117]


ALL IN ALL business inaonekana nzuri, sina uzoefu nayo lakini inaonekana inalipa ila sio kwa kiwango hicho ulichotuambia kijana.
 
Yaani unanunua pikipiki kisa mayai? Kwa soko lipi? Jaribu kwanza hata tray 10 ukimaliza ndani ya siku leta mrejesho
 
Wazo la hii biashara ni zuri, linatekelezeka, mayai ni bidhaa inayohitajika na hutoka haraka. Ila mleta uzi amekuwa mno too optimistic, gharama haziwezi kuwa kidogo namna hiyo inabidi ajitahidi kukisia gharama kiuhalisia zaidi jambo litakalosababisha pia faida kuwa ni ya kawaida siyo kubwa kama alivyosema. Hii biashara ili ikupe faida kubwa inataka uuze kwa wingi(volume) kusudi faida ya kawaida utakayoipata iweze kukua upesi na kuonekana.

Kuna hatar mbalimbali pia za mradi huu zinazoweza kutokea na kubwa zaidi ni Ushindani mkali, kumbuka mayai ni bidhaa common mno mtaani, watu wengi hasa wa kawaida hata asiyekuwa na elimu kubwa anaweza kuanzisha biashara ya mayai, karibu kila duka la rejareja linauza mayai na kuna wasambazaji wa mayai kwa baiskeli au pikipiki maaarufu kama Wakurya ukiacha vioski vya kuuza mayai jumla, Woote hawa kumbuka ni washindani wako wa moja kwa moja na ni lazima utafute kitu cha ziada utakachokuja nacho sokoni kusudi uweze kuwapiku vinginevyo hizo trei 45 kwa siku hao vijana hawataweza kufikisha na mwishowe utawaona wabaya bure.

Hatari nyingine ninayoiona kama waliotangulia walivyosema ni ubabaishaji wa vijana wa kazi kuongopa vitu kadha wa kadha ili wajinufaushe mfano kuchomoa spea za pikipiki na kuziuza kisha wanabandika mbovu, kuiba mayai na kusingizia bahati mbaya yalivunjika nk. ni lazima ucalculate risk zote hizi na jinsi utakavyoweza kukabiliana nazo otherwise hii business siyo mbaya ukiamua kuifanya kwa dhati inaweza kukulipa vizuri tu kwani ina uhitaji mkubwa katika jamii
 
Hata wale matikiti nao Wana mahesabu heka Moja ukizidisha mara sijui ni ni milioni na ukifikisha sokoni sijui faida ?
[emoji16] Vodacom yenyewe Ina M-pesa lakini inaumiza kichwa kupata faida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…