Mchango wa mtihani wa moko STD IV Tshs 15,000 siyo sahihi!

DAKA MTUMBA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2014
Posts
1,288
Reaction score
801
Mwanangu anasoma shule ya msingi AIRWING-BANANA-UK.Leo karudishwa nyumbani eti akafate pesa ya mtihani wa MOKO ambayo ni tshs 15,000.
Ndugu zangu si serikali inasema elimu ya msingi ni kwa watanzania wote na ni bure?sasa hili la mchango na kupigwa bakora limekaaje?Nadhani kesho naenda kukomesha hii tabia,becouse binti yangu kaambiwa kama kesho ataenda bila pesa basi ataoga fimbo!!!!
 

napita
 
ulitaka walimu walipwe shilingi ngapi kwa kazi hiyo? wacha kiherehere cha kwenda shule
 
Uamuzi ni wako, ulipe afanye mtihani, usilipe hatafanya mtihani..
 
If you think education is expensive,try ignorance
 
If you think education is expensive,try ignorance

lipa pesa hyo mtoto afanye mtihani! kutunga mtihani @ 1000 x mitihani 5 = 5000. kuchapa na kuprint 1000x mitihan 5 =5000. Hiyo 5000 nyingine ni ya posho za waalimu na usafirishaji wa mitihan na kusahihisha pamoja na matokeo plus corrections! ebu tuwaonee huruma walimu wetu plz. LIPA HYO PESA MTOTO AFANYE MTIHAN
 
Last edited by a moderator:
Maajabu duniani yanazidi kuongezeka, mpaka mtu anauwezo wa kuandika uzi humu Jf lakini hajui maana, umuhimu, na gharama za Mock si maajabu haya!!!!!!!!! Huyu amelewa pombe zikiisha atatuomba radhi kwa usumbufu !
 
Maajabu duniani yanazidi kuongezeka, mpaka mtu anauwezo wa kuandika uzi humu Jf lakini hajui maana, umuhimu, na gharama za Mock si maajabu haya!!!!!!!!! Huyu amelewa pombe zikiisha atatuomba radhi kwa usumbufu !

Mi naona tatizo si kulipa hizo buku 15 bali ni huu usanii wa hawa wahuni wanaojiita Nambari wani wanaoimba kila kukicha eti elimu inatolewa "Bure kabisa"!
Hivi kwa nini watanzania tumegeuzwa misukule ya majambazi hawa?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
hujawazoea na uongo wao tu? mara ngapi wametangaza kuwa wazee watatibiwa bure? je, implimentation ikoje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…