Mchengerwa: Rais ameridhia kuipandisha hadhi Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji. Soko kubwa na Stendi kuanza kujengwa

Mchengerwa: Rais ameridhia kuipandisha hadhi Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji. Soko kubwa na Stendi kuanza kujengwa

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Kwa mujibu wa Waziri wa Tamisemi bwana Mohammed Mchengerwa amenukuliwa akisema kuwa Rais Samia Ameridhia Iliyokuwa Halmashauri ya Rufiji kupewa Hadhi ya Mji ambapo Jengo kubwa la Makao Makuu la zaidi ya Bilioni 10 litajengwa Ikwiriri.

Kana kwamba haitoshi,ikumbukwe kwamba Mkuranga imeomba kuwa Manispaa ambapo Stendi kubwa ya Mabasi inaendelea na Ujenzi.👇👇
=======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Kujenga soko kubwa la kisasa pamoja na Kituo kikuu cha Mabasi wilayani Rufiji Mkoani pwani mara baada ya kuipandisha hadhi wilaya hiyo na kuwa Halmashauri ya Mji wa Rufiji.

Kulingana na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara Ikwiriri wilayani humo, amesema utekelezaji wa miradi hiyo mikubwa unatarajiwa kuanza rasmi mwanzoni mwa Mwezi Novemba mwaka huu 2024.

Mhe. Mchengerwa amewaambia wananchi wa Rufiji kuwa ujenzi wa soko hilo litakalokuwa na maduka zaidi ua 122, Vizimba zaidi ya 100 na vibanda vya wafanyabiashara ndogondogo utagharimu fedha taslimu shilingi Bilioni 14 huku pia Serikali ya awamu ya sita ikiahidi kujenga Jengo la Utawala katika Halmashauri hiyo ya Mji litakalokuwa la Ghorofa tatu zenye Ofisi zaidi ya 50 na kugharimu takribani shilingi Bilioni 10.

My Take
Halmashauri zilizokidhi vigezo na kuwasilisha maomba mapema kabla ya kina Rufiji nazo zipandishwe hadhi pia mfano Mbalizi Kwa Mwamposa.


Pia soma: Rais Samia akataa ombi la kuipandisha hadhi Mbalizi kuwa Halmashauri ya mji
 
Kwa mujibu wa Waziri wa Tamisemi bwana Mohammed Mchengerwa amenukuliwa akisema kuwa Rais Samia Ameridhia Iliyokuwa Halmashauri ya Rufiji kupewa Hadhi ya Mji ambapo Jengo kubwa la Makao Makuu la zaidi ya Bilioni 10 litajengwa Ikwiriri.

Kana kwamba haitoshi,ikumbukwe kwamba Mkuranga imeomba kuwa Manispaa ambapo Stendi kubwa ya Mabasi inaendelea na Ujenzi.👇👇


View: https://www.instagram.com/reel/DBAieqbM8E5/?igsh=M3Vocm12cDdpNzMy

My Take
Halmashauri zilizokidhi vigezo na kuwasilisha maomba mapema kabla ya kina Rufiji nazo zipandishwe hadhi pia mfano Mbalizi Kwa Mwamposa.

Mmmmmm kweli mupe muruke.....nkweee ukweniii
 
Hii Nchi kweli umuhimu wa katiba mpya itakayopunguza mamlaka ya Rais.
Vipi kuhusu vigezo? Vigezo vya halmashauri kupandishwa hazi vizingatiwe na vionekeane kweli vimefuatwa.
Hili suala limekaa kiukakasi na kipendeleo hiyo rufiji niliyoiona wakati wa mafuriko bado sana
 
Kwa mujibu wa Waziri wa Tamisemi bwana Mohammed Mchengerwa amenukuliwa akisema kuwa Rais Samia Ameridhia Iliyokuwa Halmashauri ya Rufiji kupewa Hadhi ya Mji ambapo Jengo kubwa la Makao Makuu la zaidi ya Bilioni 10 litajengwa Ikwiriri.

Kana kwamba haitoshi,ikumbukwe kwamba Mkuranga imeomba kuwa Manispaa ambapo Stendi kubwa ya Mabasi inaendelea na Ujenzi.👇👇
=======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Kujenga soko kubwa la kisasa pamoja na Kituo kikuu cha Mabasi wilayani Rufiji Mkoani pwani mara baada ya kuipandisha hadhi wilaya hiyo na kuwa Halmashauri ya Mji wa Rufiji.

Kulingana na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara Ikwiriri wilayani humo, amesema utekelezaji wa miradi hiyo mikubwa unatarajiwa kuanza rasmi mwanzoni mwa Mwezi Novemba mwaka huu 2024.

Mhe. Mchengerwa amewaambia wananchi wa Rufiji kuwa ujenzi wa soko hilo litakalokuwa na maduka zaidi ua 122, Vizimba zaidi ya 100 na vibanda vya wafanyabiashara ndogondogo utagharimu fedha taslimu shilingi Bilioni 14 huku pia Serikali ya awamu ya sita ikiahidi kujenga Jengo la Utawala katika Halmashauri hiyo ya Mji litakalokuwa la Ghorofa tatu zenye Ofisi zaidi ya 50 na kugharimu takribani shilingi Bilioni 10.

My Take
Halmashauri zilizokidhi vigezo na kuwasilisha maomba mapema kabla ya kina Rufiji nazo zipandishwe hadhi pia mfano Mbalizi Kwa Mwamposa.


Pia soma: Rais Samia akataa ombi la kuipandisha hadhi Mbalizi kuwa Halmashauri ya mji
Rasilimali za Nchi zinaelekezwa maeneo walipo Viongozi wa karibu na Mkuu wa Nchi. Kila Mtu akipata cheo ndio maendeleo yanaelekezwa huko. Kwani hakuna kanuni au sheria hadi suala lishinikizwe kutokana na cheo?
 
Rasilimali za Nchi zinaelekezwa maeneo walipo Viongozi wa karibu na Mkuu wa Nchi. Kila Mtu akipata cheo ndio maendeleo yanaelekezwa huko. Kwani hakuna kanuni au sheria hadi suala lishinikizwe kutokana na cheo?
Hili sio la ajabu Kwa hapa Tanzania.Nimeona Leo huko Kagera watu wanaliwa pesa zao za fidia kisa tuu Waziri wa Ujenzi ni WA huko.

Maeneo mengine wamesubiria Hadi wamekata tamaa
 
Hii Nchi kweli umuhimu wa katiba mpya itakayopunguza mamlaka ya Rais.
Vipi kuhusu vigezo? Vigezo vya halmashauri kupandishwa hazi vizingatiwe na vionekeane kweli vimefuatwa.
Hili suala limekaa kiukakasi na kipendeleo hiyo rufiji niliyoiona wakati wa mafuriko bado sana
Kuna halmashauri za miji zina vigenzo vya kuwa Manispaa lakini vimepigwa pin lakini kwa vile kule Mbunge ni mkwe chap
 
Back
Top Bottom