Mchezaji Akataa Milioni 100 za Azam ataka Milioni 250 kumvua gwanda

Mchezaji Akataa Milioni 100 za Azam ataka Milioni 250 kumvua gwanda

Smart codetz

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2023
Posts
218
Reaction score
875
Note 📝 NAHODHA wa JKT Tanzania, Edward Songo amesema uwepo wachezaji wa kigeni Championship, umeisaidia kuipa thamani kubwa ligi hiyo na inakuwa rahisi kwao kuonekana na timu za Ligi Kuu.

Akijitolea mfano baada ya kufanya vizuri msimu uliopita ambapo alikuwa kinara wa mabao 16 na sasa ana 11 kwamba alifuatwa na Azam FC iliyokuwa inahitaji huduma yake ila alishindwana nao.

Songo alisema Azam ilimwekea dau la usajili la Sh100 milioni na mshahara wa Sh.3 milioni, lakini aliona sio pesa inaoweza kumvua magangwa ya jeshi na aliamini hiyo pesa anaweza akapata mkopo serikalini kwa muda mfupi.

"Niliwaambia nahitaji Sh.250 milioni, lakini hatukufikia mwafaka, yote katika yote nilionekana kwenye Ligi ya Championship ndio maana nasema kwa sasa ina thamani kubwa na ina mashabiki; Aliongeza "Angalau maisha ya wachezaji wanaweza wakapata kitu, kikubwa ni wao wenyewe kuipa thamani kazi zao.

05045642-FF4D-4E68-9703-2230ED5DBAE4.jpeg

 
Watu hawaelewi kuwa huyo ni mwajiriwa serikalini idara ya ulinzi na usalama, hivyo ili kumfanya aachane na mshahara, posho na mafao yake huko baada ya kusitaafu lazima ahitaji hela nyingi.

Angekuwa sio mwajiriwa wa serikali, hata milioni tano ya usajili asingeikataa.
 
Watu hawaelewi kuwa huyo ni mwajiriwa serikalini idara ya ulinzi na usalama, hivyo ili kumfanya aachane na mshahara, posho na mafao yake huko baada ya kusitaafu lazima ahitaji hela nyingi.

Angekuwa sio mwajiriwa wa serikali, hata milioni tano ya usajili asingeikataa.
Na ndo nilivyo elewa mie hapa.
 
Akakataa one hundred million!!

Mtu mwenyewe yuko championship

Kamba hii
we kumbe zumbu bata sasa mtu atoke kwenye ajira ya kudumu kisa milion 100 hlf acheze miaka mitatu tu atemwee wakati jeshini yupo mpaka anastafu ukijumlisha mashahara na mafao nanposho ni zaidi ya izo milion 100
 
Back
Top Bottom