Mchezaji bora wa Mwezi Yanga kulamba milioni nne.

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2012
Posts
22,719
Reaction score
40,739
𝗣𝗥𝗘𝗦𝗦

“Baada ya kuingia mkataba na NIC, uongozi wa Yanga uliunda kamati maalum ya kufanya Tathmini ya mechi zote za mwezi husika na kutupatia majina matatu ya wachezaji watakaowania tuzo ya mchezaji bora kisha sisi tutayaanika kwa wananchi kwaajili ya kuwapigia kura”

“Yafuatayo ni majina matatu ambayo kamati imeyaleta kwa uongozi wa Yanga Kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Mwezi, nayo ni Stephane Aziz Ki, Dickson Job pamoja na Max nzengeli, majina haya yatapigiwa kura kupitia Application yetu ya YANGA APP.[emoji2398]Ali kamwe

“Tuzo ya Mchezaji bora wa NIC insurance imezingatia vitu vingi ikiwemo ubora wa NIC kama brand, ubora wa Yanga kwa pamoja na uwepo wa wachezaji wazuri watakaoleta mchuano mkali, hivyo zawadi ya mshindi itakuwa bora, mshindi wa tuzo hizi atapatiwa kiasi cha shilingi milioni 4”

“Lakini pia mbali na kiasi cha Fedha mshindi atapatiwa tuzo itakayomfanya mchezaji apate historia kubwa isiyofutika, wanauliza tuzo hizi tutaanza kuzitoa lini jibu lao ni kwamba, baada ya wananchi kupiga kura, tutatoa tuzo hizi siku ya Jumanne.
 
Hiyo tuzo ni ya konkoni kabsa labda wambanie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…