Mchezaji gani aliyestafu ungependa arudi uwanjani

kaka ni mrokole mkuu labda ndo maana alifanikiwa huwa hana makuu kabisa huyu jamaa.
 
Louis Saha.

Huyu bwana nahisi alionesha 1/4 tu ya kipaji chake sababu ya kuwa majeruhi mara kwa mara hasa akiwa pale Man U.

Kwa mujibu wa Wyne Rooney ni kwamba Saha ndiye favorite player wake ambaye amewahi kucheza naye.
hata mm huyu jamaa nilikuwa na muhofia sana pale alipokuwa hata akiingia dk ya 85 lazima mabeki wajipange
 
Mohamed chuma wa mtwara beki miaka 15 taifa starz na mashindano ya ndani hakuwahi kupata kadi nyekundu.
Jari litmannen chuma cha ajax hiki hakikuwa na mchezo na kuzifumania nyavu.
Litmanen na Ajax ile ya akina De Boer brothers, Patrick Kluivert, Finidi George, Edwin Van Der Sar wanabeba Uefa Champions League chini ya Jemedari Louis Van Gaal.
 
Suker aling'aa World Cup ya mwaka 1998 pale Ufaransa.

Walishika nafasi ya tatu kama sikosei kulikuwa na fundi wa mpira aliyeitwa Zvonomir Boban jamaa alikuwa analijua kabumbu haswa ndio maana sikushangaa Haruna Moshi alipoiga jina la Boban.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…