Mchezaji wa zamani wa Simba SC, Damian Mrisho 'Kimti' afariki Dunia

Mchezaji wa zamani wa Simba SC, Damian Mrisho 'Kimti' afariki Dunia

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
IMG-20200303-WA0017.jpg


Damian Mrisho Kimti aliyekuwa akicheza katika nafasi ya ushambuliaji wa pembeni (Winger), alisifika kwa uwezo mkubwa wa kupiga chenga, mashuti makali na umahiri mkubwa wa kupachika mabao

Alikuwepo katika kikosi cha Simba kilichocheza fainali ya Kombe la CAF dhidi ya Stella Abidjan mnamo Novemba 29, 1993 katika Uwanja wa Uhuru, ambapo Simba ilipoteza kwa kufungwa goli 2-0

Baada ya kustaafu kucheza soka la ushindani, alikuwa akijishughulisha na kazi ya ualimu akifundisha somo la Kifaransa katika shule mbalimbali ikiwemo St. Mery ya Tabata

Kikosi cha Simba kilichotamba katika michuano hiyo ya Kombe la CAF mwaka 1993 chini ya Mfadhili Mkuu, Azim Dewji kilihusisha Wachezaji Kasongo Athumani, David Mihambo, Michael Paul ‘Nylon’, Twaha Hamidu na Mavumbi Omar

Wengine ni Often Martin, George Lucas ‘Gazza’, Mbuyi Yondan, Suleiman Pembe, Ramadhani Lenny, Edward Chumila, Hussein Marsha na Mwameja Mohammed

Aidha, alikuwepo Duwa Said (Hakucheza michuano hiyo kwa sababu hakusajiliwa alikuwa anacheza Ligi ya Tanzania Bara pekee), Iddi Selemani ‘Meya’, Damian Kimti na Deo Mkuki
 
Daah! Namkumbuka enzi za utotoni kuna jamaa alikuwa anaitwa Ibrahim (Ibu) alikuwa anampenda sana mpaka nae tukamwita Kimti mpaka leo!

R.I.P. KIMTI, tuliokuwepo enzi zile tulifurahia sana burudani yako!
 
Kipindi huyu Bwana anacheza kuna msimu akazifunga karibia timu zote zilizocheza na Simba mfululizo mechi kadhaa hivi. Basi timu mojawapo katika hizo ikaanzisha zengwe kua jamaa ni mrundi. Kusikia hivyo timu Zingine nazo zilizofungwa na huyu jamaa zikaunga hao mpaka FAT kukata rufaa.

Sasa kufika kule FAT kila timu ikiulizwa ushahidi wa urundi wa jamaa wanajibu wamesikia sikia tu mitaani watu wakisema sema (Bendera Fata Upepo).

R.I.P "Kimti"
 
Pumzika kwa Amani mchezaji wa Mnyama, tarehe 8/3/2020 tutakuenzi kwa kipigo cha Haja kwa Watani zenu ili Upumzike kwa amani.
 
Hivi hizi stori kuwa alikuwa Mrundi ,zilianzaje ,kabla ya Simba alikuwa wapi...RIP
 
Kipindi huyu Bwana anacheza kuna msimu akazifunga karibia timu zote zilizocheza na Simba mfululizo mechi kadhaa hivi. Basi timu mojawapo katika hizo ikaanzisha zengwe kua jamaa ni mrundi. Kusikia hivyo timu Zingine nazo zilizofungwa na huyu jamaa zikaunga hao mpaka FAT kukata rufaa.

Sasa kufika kule FAT kila timu ikiulizwa ushahidi wa urundi wa jamaa wanajibu wamesikia sikia tu mitaani watu wakisema sema (Bendera Fata Upepo).

R.I.P "Kimti"
Kimti alijiunga Simba akitokea burundi
 
Daah! Namkumbuka enzi za utotoni kuna jamaa alikuwa anaitwa Ibrahim (Ibu) alikuwa anampenda sana mpaka nae tukamwita Kimti mpaka leo!

R.I.P. KIMTI, tuliokuwepo enzi zile tulifurahia sana burudani yako!
Hamjasema kuhusu utata wa uraia wake...
 
Sasa nani atathibitisha wakati muhusika namba 1 amefariki dunia
Hakuna haja ya kuthibitisha,.nilileta hii makusudi ili kuwafahamisha mashabiki oya oya wa siku hizi namna fitina za usimba na uyanga zilivyokuwa zikitawala wakati huo...hata said maulid alivyohamia yanga alituhumiwa kuwa so raia...Kama Niko sahihi mkasa wa said maulid ni sababu mmojawapo iliyosababisha afisa mmoja wa uhamiaji kuhamishwa kutoka makao makuu kwenda mikoani
 
Back
Top Bottom